Kisa cha rafiki yangu wa Mafia

Kisa cha rafiki yangu wa Mafia

aise

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2018
Posts
5,175
Reaction score
16,488
Habari zenu wakuu, rafiki yangu wa mafia ananiambia hivi.

Mimi nimezaliwa na kukulia kisiwani mafia, shuleni kwetu tangia naanza darasa la awali mpaka namaliza darasa la saba, hapakuwahi kuwa na mwanafunzi mkristo, sote tuliwa wa imani ya uislamu. Aliwahi kuja mwalimu mmoja wa imani ya ukristo lakini hakukaa sana akaondoka.

Kwa ufupi sisi tangu utotoni katika ukuaji wetu tulifundishwa kwa msisitizo sana kuwa mtu ambaye si wa imani yetu, huyo mtu haifai hata kumsogelea kwa namna yoyote ile, mtu ambaye si muislamu ni sawa au ni zaidi ya nguruwe au mbwa. Mara kadhaa walipokuja watalii wa kizungu, hao ndiyo tuliaminishwa kabisa ni watu wanaopigana na Mungu anayetupatia uwezo wa kuishi. Alipopita mzungu tulikuwa tukitema mate kwa nyuma kuashiria ni kitu ambacho hata kukiona ni dhambi.

Mimi nilipomaliza darasa la saba nilitafutiwa uhamisho na nikahamia Vikindu, na hapo nilianza kidato cha kwanza. Kwakweli niliteseka sana siku za mwanzo pale shuleni, maana nyumbani Mafia nilifundishwa kuwa mtu asiye wa imani yangu ni haramu na haitakiwi hata nimsogelee.

Darasani nilipangwa dawati moja na mkristo, aliyeitwa Yohana Frank, kwakweli nilikaa naye kwa taabu sana nikiamini kukaa dawati moja na yeye natenda madhambi na nitaikosa pepo. Baada ya kuzoea mazingira ya shuleni nilipata rafiki wa imani yangu aliyeitwa Omari.

Cha kusikitisha huyo Omari alikuwa na marafiki wa imani ya kikristo, na walikuwa wakigawana vyakula pale shuleni. Mimi kwa mazingira niliyokulia na mafundisho niliyofundishwa tangu utotoni nilikuwa na wakati mgumu sana pale shuleni. Watu nilioaminishwa ni haramu na haitakiwi hata kuwasogelea, iweje leo nikae nao meza moja na kula pamoja nao?

Kwakweli nilikuwa nikijiuliza maswali mengi sana, na nikaanza kuyafikiria upya mafundisho yote niliyofundishwa tangu utotoni ikiwa yana mantiki au la! Nilianza kuifikiria imani yangu yote kwa ujumla. Mpaka leo nimeanza kufikiria kama kweli Mungu yupo? Huyu Mungu niliyefundishwa tangu utotoni yupo? na vipi kuhusu hawa miungu wa imani nyingine tofauti na imani yangu?
 
Nimejisikia vizuri sana aliposema ameanza kufikiria ikiwa kweli Mungu yupo?

Bila shaka hivi karibuni atatambua Mungu wa imani yake hayupo, wala Miungu wa imani nyingine tofauti na imani yake hawapo.
Namtakia kila la kheri.
 
Naona rafiki yako amekaa na Yohana dawati moja tayari Yohana ameshambatiza anaanza kui question iman yake.

Ila dini yoyote ile inayofundisha wafuasi wenzake kuwa wasioamini katika dini hiyo sio watu na wanastahili kuwa treated kama mbwa au nguruwe hiyo sio dini ya kweli.

Islamism inafeli hapo tu. Huwezi kumpa Mungu sifa zote halafu umuite mwenzako kufar/kafiri na eti utapata thawabu ukimuua kafir kisa haamini katika uislam.

Mna kazi sana wenye imani zenu. Bora tusioaminishwa uongo.
 
Sawa ndugu Yohana Frank. Nitaongea na Askofu Gwajima, rafiki yangu Mwamposa! Ili tuone namna ya kuja kufungua kanisa huko Mafia na tuwakombea hao Kondoo wote walio potea.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Jipange kisawasawa aisee..
Kuna wenzenu huku Unguja wao ndo mapadri lkn cha ajabu wao ndo walisilimu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi najiuliza tu, hawataki members wapya? Watawapataje wakiwaua.
Naona rafiki yako amekaa na Yohana dawati moja tayari Yohana ameshambatiza anaanza kui question iman yake.

Ila dini yoyote ile inayofundisha wafuasi wenzake kuwa wasioamini katika dini hiyo sio watu na wanastahili kuwa treated kama mbwa au nguruwe hiyo sio dini ya kweli.

Islamism inafeli hapo tu. Huwezi kumpa Mungu sifa zote halafu umuite mwenzako kufar/kafiri na eti utapata thawabu ukimuua kafir kisa haamini katika uislam.

Mka kazi sana wenye imani zenu. Bora tusioaminishwa uongo.
 
Ila dini yoyote ile inayofundisha wafuasi wenzake kuwa wasioamini katika dini hiyo sio watu na wanastahili kuwa treated kama mbwa au nguruwe hiyo sio dini ya kweli
Ungekuwa unaijua Mafia, ungempuuza...

Lakini kwavile umeamua kumwamini, sasa unaichukuliaje hiyo dini nyingine inayofundisha watoto kwamba wakikaa na Waislamu wanapata majini?!

Ina maana wewe maishani mwako hujawahi kukaa na Waislamu?

Na kama umewahi kukaa, ulishapata hayo majini?

Na kama hujapata, ina maana hiyo dini inasema uongo?

Na kama inasema uongo, ni dini ya namna gani hiyo?! Dini ya ukweli inaweza kufundisha uongo?!

Au tuseme katika maisha yako hujawahi kukaa na Mwislamu?! Inawezekana hivyo? Au ukigundua tu kwamba Mwislamu unamkimbia kwavile ulifundishwa (according to mtoa mada ambae umeamua kumwamini) ukikaa na Mwislamu utapata majini?!

Kama ndivyo, ni dini ya namna gani hiyo inayokufundisha kukaa na watu wa imani yako pekee?!
 
Ungekuwa unaijua Mafia, ungempuuza...

Lakini kwavile umeamua kumwamini, sasa unaichukuliaje hiyo dini nyingine inayofundisha watoto kwamba wakikaa na Waislamu wanapata majini?!

Ina maana wewe maishani mwako hujawahi kukaa na Waislamu?

Na kama umewahi kukaa, ulishapata hayo majini?

Na kama hujapata, ina maana hiyo dini inasema uongo?

Na kama inasema uongo, ni dini ya namna gani hiyo?! Dini ya ukweli inaweza kufundisha uongo?!

Au tuseme katika maisha yako hujawahi kukaa na Mwislamu?! Inawezekana hivyo? Au ukigundua tu kwamba Mwislamu unamkimbia kwavile ulifundishwa (according to mtoa mada ambae umeamua kumwamini) ukikaa na Mwislamu utapata majini?!

Kama ndivyo, ni dini ya namna gani hiyo inayokufundisha kukaa na watu wa imani yako pekee?!
Chige chige chige..nimekuita mara tatu. Ni kitabu cha dini gani kimeandikwa kuwa watoto wao wakikaa na waislamu wanapata majini?
 
Chige chige chige..nimekuita mara tatu. Ni kitabu cha dini gani kimeandikwa kuwa watoto wao wakikaa na waislamu wanapata majini?
Vuta pumzi taratiiiiibu, kisha nisome kwa vituo... neneo kwa neno!! Bila shaka utanielewa ukifanya nilivyokushauri!!
 
Naona rafiki yako amekaa na Yohana dawati moja tayari Yohana ameshambatiza anaanza kui question iman yake.

Ila dini yoyote ile inayofundisha wafuasi wenzake kuwa wasioamini katika dini hiyo sio watu na wanastahili kuwa treated kama mbwa au nguruwe hiyo sio dini ya kweli.

Islamism inafeli hapo tu. Huwezi kumpa Mungu sifa zote halafu umuite mwenzako kufar/kafiri na eti utapata thawabu ukimuua kafir kisa haamini katika uislam.

Mka kazi sana wenye imani zenu. Bora tusioaminishwa uongo.
Mtume muhamad (s.a.w) alikuwa anaishi na asiye muislam ndani kwake hakumuua ndio iwe sisi? Jombaa kama vitu huelewi ni bora kuuliza na sio kukurupuka
 
Huko mafia nasikia kama si mwislam hukai walai.Watumishi wengi wa umma huishia kuhamia maana nasikia ubaguzi ni kiwango kikubwa mno
Uongo mtupu

Airport na Bandari vyote vipo mjini, kwahiyo uwe umeingia kwa boti au kwa ndege, kama safari yako inaishi mjini basi unatembea tu unless uwe unaenda vitongoji vilivyo nje kidogo!!

Huyo mleta mada ama nae ni MUONGO au ni mtu kutoka vijijini, na wala asiseme "kwetu Mafia tunafundishwa...." bali aseme "kwenye familia yao wanafundishwa..."

Sijaenda Mafia muda mrefu sana lakini hapa nitaizungumzia Mafia ya wakati huo ambayo pengine ndiyo tungesema ni hatari zaidi kwa watu wa dini zingine!

Ilikuwa ukiteremka airport na kutembea umbali mfupi, unakutana unakutana na NMB. Kutoka NMB, hatua chache mbele unakuta mkungu na chini yake kuna uwanja! Kusini Mashariki ya Uwanja kuna kanisa, nadhani la KKKT! Kanisa hili limezungukwa na makazi ya Waislamu na watu wanafanya ibada kama kawaida!

Kwenye Uwanja twaja, watu wanatumia sana kufanya mahubiri. Home kwetu ni town kabisa kiasi kwamba nikisimama karibu na dirisha naona kila kinachooendelea hapo uwanjani! Uwanja ule ni kawaida sana tena sana kukuta Wahubiri wa Kikristo wakitoa mahubiri yao na wengi wanatoka bara!

Kuna wakati walikuja Wahubiri wa Kikristo ambao lau kama pale ingekuwa ni Dar es salaam, wallah kingenuka kwa sababu yale hayakuwa mahubiri bali kashfa za Uislamu! Lakini walikaa Mafia wiki mzima na wakaondoka bila bughudha yoyote!

And what's even more interesting, ukiwa hapo uwanjani unawasikia watoto wa madrasa wakisoma kwa sababu Madrasa ipo hapo ukishamaliza tu uwanja!!! Huu uwanja nao, umezungukwa na makazi ya Waislamu!!

Sina uhakika kama hadi sasa yupo lakini wakati ule, ilikuwa ukipita tu ile madrasa, mbele kidogo unakutana na baa ya dada mmoja alikuwa anaitwa Hellen Lyimo!! Yaani umbali mfupi kutoka ilipo madrasa unakutana na baa ambayo mmiliki wake ni Mkristo!!

Hiyo ndo Mafia mnayodanganyana kinyume chake!! Uongo ambao kwa kawaida unaenezwa na watu wenye chuki tu za kidini!!!
 
Back
Top Bottom