Kisa cha RC Namfua na Watawa huko Kilimanjaro

Kisa cha RC Namfua na Watawa huko Kilimanjaro

Wildlifer,

..Kilimanjaro wana bahati hawakupitiwa na operesheni vijiji.

..Wako wanaodai kuna RC ambaye alimuonya Mwalimu Nyerere kuhusu hatari au madhara ya kupeleka operesheni vijiji Kilimanjaro.

..Sijui kama ktk makbrasha kuna taarifa za kilichosababisha operesheni vijiji isitekelezwe Kilimanjaro ambacho unaweza ku-share na sisi.
Katika Soma soma yangu, nilipata kuona mahala andiko hili limenukuliwa; [emoji116]

Mushi, A. Sangale, “The Problems of Starting Ujamaa Villages in Kilimanjaro District".

Ni utafiti kutoka UDSM, bahati mbaya nimepekenyua sana mtandaoni sijabahatika kuupata.
 
Ninakumbuka zamani kuna mwizi aliiba vikombe vya madhabahuni akijiua ni dhahabu, ni kweli vile vya zamani vilikua ni pure gold. Padre alisali novena na kuomba misa. Jamaa aligeuka chizi na kusema mpaka sehemu alipoviuza.
Novena yenye kujibu maombi ya papo kwa papo ni Novena ya Mt. Rita wa Kashia.
Hii usiiombe ukiwa huna uhakika na ufanyacho.
Sky Eclat uko sahihi
 
Albadiri ni shirki tu wala usiwatetee hao masheikh kisa unawajua iyo ni ushirikina tu

Kma ukibisha niletee ushahidi kua Mtume katuamrisha tufanye ivo
Siyo shirk masheikh wanafanya sana. Tena sana tu sasa hapo unataka kusema nini. Acha hizo. Albadil ni kuyaomba majin yakafanye kazi flani ya kumuadhibu mtu mkorofi
 
Hii ya Dr Kleruu ni kweli tupu.
Namkumbuka mke wake na watoto walikuwa wakiishi pale Shanty Town.
Mama ni kama akili haikuwa sawa kwa miaka mingi!
 
Hii hapa hiyo novena, hii ni zaidi ya mganga.
Sema wengi tunaishindwa kwa sababu ya masharti yake, japo wapo wanaofikia malengo Chizi Maarifa
IMG_20240214_092420_139.jpg
 
Wildlifer,

..Kilimanjaro wana bahati hawakupitiwa na operesheni vijiji.

..Wako wanaodai kuna RC ambaye alimuonya Mwalimu Nyerere kuhusu hatari au madhara ya kupeleka operesheni vijiji Kilimanjaro.

..Sijui kama ktk makbrasha kuna taarifa za kilichosababisha operesheni vijiji isitekelezwe Kilimanjaro ambacho unaweza ku-share na sisi.
Enzi za mwalimu kulikuwa na mambo ya kiwaki sana. Operesheni vijiji, azimio la Arusha, chama kushika hatamu na mambo mengine ya hovyo mno
 
Albadiri ilipigwa pale tanga baada ya shekhe kuibiwa nazi shambani.hadi punda aliebeba aliaga dunia.sikumbuki jina la yule sheikh lakini ilitokea balaa kubwa sana kwa wakati ule.mashekhe wale wa zamani ndio waliweza kuisoma albadiri na kuleta matokea papo hapo.wa sasa hivi nao vibaka sana wakipiga albadiri itaanza na wao ndo iende kwa wengine
Duh!...
 
Salaam wanahistoria!

Leo nilikuwa mahala fulani napiga soga na kiongozi mmoja wa Kanisa Katoliki. Soga zetu ziligusa maeneo mengi hasa Historia ya Tanzania wakati wa utawala wa Mwalimu. Kwa sababu ya utofauti mkubwa wa kielimu, umri na uzoefu wa maisha, nilikuwa msikilizaji zaidi huku nikimchokoa zaidi.

Alinieleza kuwa changamoto kubwa ya utawala wa Mwalimu, ilikuwa ni kulewa madaraka kwa wengi wa viongozi wake hasa MaRC na MaDC. Alinipa visa vichache, kigeni kwangu kilikuwa cha RC wa Kilimanjaro, aliyeitwa Namfua. Kuwa;

Serikali ya mkoa wa Kilimanjaro na Chama viliamua kuwa jengo lilokuwa la Watawa huko Kilimanjaro, lichukuliwe na kufanya shughuli za serikali. Walipouliza, wao wataenda wapi na wanachukua kwa utaratibu gani; jibu lilikuwa ni kuwa serikali na chama imeamua—enzi hizo, zilikuwa ni za chama kushika hatamu(Party Supremacy), RC pia alikuwa ni Katibu wa Chama wa Mkoa. Kisha kupewa siku 21 wawe wamehama.

Watawa wale, walimlilia Padre wao, aliyewapa majibu kuwa yeye hana cha kufanya, bali wafunge na kuomba. Kabla ya muda wa siku 21 kufika, RC Namfua, alipata safari ya kikazi nje ya nchi, maagizo yake ilikuwa akirudi, watawa wale wawe wameondoka (maana siku hizo 21 zitaisha akiwa nje ya nchi).

Aliporudi safari yake, baada ya kufika tu Airport, swali lake la kwanza likawa 'Watawa wameshahama?' Jibu alipewa kuwa bado wapo.

View attachment 2570345
Basi, Namfua akaagiza Defender mbili (101 enzi hizo) za askari, wenye silaha, ziongozane naye na kuanza safari kuwafuata watawa wale. Kabla hajaenda hata ofisini kwake, moja kwa moja kutoka Airport, bila hata Protocol ya kuongozana na DC, na kuwatanguliza Askari mbele, msafara ulielekea kwa watawa wale.

Wakiwa njiani, alikatiza mbuzi, dereva katika harakati za kumkwepa; alifunga breki za ghafla, RC ambaye hakuwa amefunga mkanda, alichomokea kwenye windscreen, na maisha yake yakaishia pale. Msafara ukageuza, na kuwa msafara wa msiba.

Kisa hiki, na cha Dr Kleruu, vyaelezwa kuwa ndio vilichangia walau kuwafanya viongozi wa Nyerere kuwa na ustaarabu kwa wananchi.

Cc: Mohamed Said JokaKuu Sky Eclat Pascal Mayalla Red Giant
Watu mmekubuhu kwa uongo
 
Back
Top Bottom