Kisa cha wanawake wa JF kuitwa vikongwe/vibibi

Kisa cha wanawake wa JF kuitwa vikongwe/vibibi

Kuwa na utambuzi bandia , kuna faida nyingi lakini vile vile kuna ficha mengi na kutatiza mengi pia.. Utambuzi bandia huleta hali ya kujiona wote tuko sawa kiumri, kiufahamu, kielimu, maono hata uzoefu
Ni mpaka pale kupitia maandishi yetu kwenye majukwaa mbalimbali ndio mtu anaanza kuona utofauti wa hayo yote...iwe kwenye mada kuu michango ya wasomaji ama aina ya jukwaa

Kiasili kati ya jinsia mbili hizi mwanamke na mwanaume, maumbile na sometimes akili ya mwanamke hukua na kukomaa haraka kuliko mwanaume..hili halina ubishi wa kubishaniwa ndio maana ni rahisi kwa mwanaume wa miaka 50 kulala na binti wa nusu ya umri wake ...lakini hali hiyo ni tofauti kabisa kwa wanawake

JamiiForums Ni mtandao uliojipambanua kwenye maono ya kuwa na usiri kwenye utambuzi ili kulinda privacy na maudhui ya wahusika...lakini ndio hapa wasiojitambua wamekitumia kipengele hiki vibaya
Tunaishi dunia ya mitandao na hili halikwepeki...lakini huko kwingine watu wanajiachia kwa picha na majina yao halisi hivyo ni rahisi kutambulika... Na huko mitandao maarufu mingi wateja wake kwa asilimia 85 hivi ni vijana chini ya miaka 30...

Unapokuja JF mambo ni tofauti kidogo wateja wake wa tangu mwanzo tayari wameshavuka miaka 30, na hata waliojiunga hapo katikati na baadae kidogo.....! JF inazidi kukua na kupata umaarufu huku ikivutia vijana wengi chini ya miaka 30, wake kwa waume..kundi ambalo damu inachemka hasa huku nafasi ya tafakuri na umakini vikiwa finyu sana

Ni kundi hili hasa la vijana wa kiume lililozoea kuchat na vibinti huko kwenye mitandao mingine , likiingia huku na kukutana na ID zenye majina ya kuvutia na picha pia, basi wao tayari hujenga picha fulani mawazoni mwao na kuchukulia huo ndio uhalisia
Na mama na dada zetu bila kuwaza sana ama kwa sababu zozote zile hujikuta wanaanza mazoea na hawa vijana hapa upenuni lakini baadae mambo hunoga na kuhamia PM...huko hubadilishana namba na kujenga ukaribu hadi kuonana

Kasheshe huja siku ya live event....dogo anataraji kukutana na pisi kinda kali kinyama,..... Mdada naye anataraji kukutana na mkaka fulani hivi decent mambo safi
Wengi hushangaana kimyakimya na kumalizana kimya kimya pia na hiyo ikiwa ndio date ya kwanza na ya mwisho...! Wadada kwa sehemu kubwa hukaa kimya na kusimuliana wenyewe kwa wenyewe...wadogo zangu wa kiume hawaweki kitu rohoni, kama hutalikuta kwenye post utalikuta kwenye reply.,..yote yakikandia uzee na utu uzima wa wanawake wa JF...

Ni vigumu kumchagulia mtu ID au avatar lakini kuepusha usumbufu ni vema watu wakawa na ID na avatar vinavyoendana na umri wao...Na kwa wadogo zangu wote JF ina watu wote humu ndani
Tuna mabibi na mababu zetu humu ndani
Tuna wajomba na mashangazi humu ndani
Tuna wadada na wakaka zetu, mawifi na mashemeji na wakwe
Tuna watoto wa mama, tuna vibaka matapeli.. Na wauza nyama pia
Tuna viongozi mbalimbali wakubwa na wadogo
Tuna matajiri na watu wenye biashara na connection mbalimbali
Wote hawa kwa ujumla wake TUNAKUTANISHWA NA UTAMBULISHO BANDIA....

Jifunze kuheshimu kila mtu....!!!!
🤣🤣🤣
Nilijua ni pisi kali baada ya kuona avatar yake nikaingia pm mambo yakaenda poa tuka date tukutane 77 hotel pale Arusha.

Niliwahi kufika mapema hapo hotel ili nimuone mpenzi wangu atakapokuwa anaingia jinsi alinyo kimwondoko mapozi nk.

Sitasahau siku hiyo baada ya kujikuta nipo na shangazi yangu na sio pisi kali niliyemtarajia yaani kumbe nilikuwa nachat pm na dada yake baba yangu mzazi,dadeki nilifuta kila kitu nikafungua acc mpya hata shangazi alifuta acc yake na sijui anatumia jina gani ila najua tunaye hapa JF

Yaani tangu siku hiyo nikawa naiheshimu JF na namheshimu kila member
Mkuu ukajua unakutana kitu kama mobeto flan hivi,ila jf watu wanajua kufake maisha 🤣
 
[emoji23][emoji23] mshana bwana

Bibi kizee Mimi [emoji4]
Kumzidi huyu? Acha utani kwenye masiala bac
Screenshot_20210307-111932.jpg
 
Mngekuwa tu wawazi. Ndio wengine tumeshakuwa bibi bomba ila tunapendana na wazee wenzetu na tunaelewana lugha moja. Leo nimeona fb mtu namjua na kumuheshimu sana, he is probably 65 yrs old. Kaandika amezaliwa 1980. Nikajiuliza sana why would he do that??

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
Hakuna anayependa uzee, basi tu inabidi tukubaliane nao coz asili inatuamuru, la hakuna anayetaka kuvuka 45. Huyo aliyeandika kazaliwa 80 namuelewa sana tu, japo inabidi akubaliane na asili.
 
Hatari sana mkuu,nikifanikiwa kuuza nyumba yetu ya urithi ya k'koo kwa pesa tunayoitaka,itabidi unipm namba ya huyo mtoto kitu konzi na yeye ajidai hata na iphone 12 max pro ya gb 516 mkuu
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]sawa mkuu
 
 
Mngekuwa tu wawazi. Ndio wengine tumeshakuwa bibi bomba ila tunapendana na wazee wenzetu na tunaelewana lugha moja. Leo nimeona fb mtu namjua na kumuheshimu sana, he is probably 65 yrs old. Kaandika amezaliwa 1980. Nikajiuliza sana why would he do that??

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaah lol
 
Mimi kuna Mkuu mmoja humu anaitwa Beef lasagna huwa namkubali tu ule upendo wa agape, nampendea tu hili jina yaani kila nikitamka hili jina kuna ka'smile flan hivi nakapata. Haijalishi umri wake utakavyokua ila imetokea tu kumkubali.
 
Na Kweli ni wabibi,.

Tena mtupe shikamoo nyingi.

Ila unaanzaje kujicomfedisha kwa tujitu tunaandika xawa my wangu,?

Nawaza huenda hao ndo masuger sukari (mammy).
Xaxa xi ndio my wang [emoji3][emoji3]
 
Back
Top Bottom