Kisa Chid Benz, bifu la Lady Jaydee na Ray C laibuka upyaaaaaa

Kisa Chid Benz, bifu la Lady Jaydee na Ray C laibuka upyaaaaaa

Nimeipenda hii comment kutoka IG.

Screenshot_20231215-183050_1.jpg
 
Nachokumbuka ni kwamba kila ijumaa nilikuwa naondoka shuleni mapema kwa ruhusa ya kwenda kusali ila kiukweli nilikuwa naishia salon moja mtaani jamaa alikuwa na deck ya cd(ya kwanza pale wilayani) na alikuwa na cd ililuwa na ngoma kadhaa za Ray C. Ki ukweli Ray C nilizipenda nyimba zake sana ila pia nilimpenda yeye kama yeye, lile jicho halikuwa la kawaida kwa kipindi kile kwa umri nilio kuwa nao. Mpaka leo jicho kubwa la mviringo ni kigezo kikubwa sana kwangu ukitaka nikuhonge hadi hela ya mwisho mfukoni. Ray C aliniteka sana japo Jide nae alikuwa na ngoma zake nzuri hasa alizoshirikishwa
 
Kweli kipenda roho ula nyama mbichi.
Jide sijawahi mkubali naona anaimba kwaya siyo muziki wa kawaida wa mtaani Kama Afro Pop, dance, n.k.
Dah mie jd hunipangi aisee,ile nyumbani lounge ,thai village, Machozi band ilikua bandika bandua hadi sasa nikiwa the marz naenda pale kumsalimia ,she is my sister kwa kweli
 
Bifu lilianzia baada ya hii interview aliyofanyiwa Chid Benz ,Chid alishauri Lady Jaydee akaimbe Gospel miaka miwili akae sawa ndipo arudi tena kwenye bongo fleva .
View attachment 2843396
Sasa lady Jaydee aliona kama hii dharau fulani hivi akajibu mashambulizi 👇👇👇👇👇

View attachment 2843397
Ikumbukwe Lady Jaydee na Chid Benz walishawahi kuwa na bifu miaka hiyo ya nyuma mpaka ikapelekea Lady Jaydee kumfuta na kufuta verse alizofanya Chid Benz kwenye video ya wimbo wa UPO JUU japo si Chid wala Lady Jaydee aliyejitokeza kujibu sababu haswa ilikuwa ni Nini japo habari za chini chini inasemekana Chid akimtongoza Lady Jaydee,Lady Jaydee akaona kama kavunjiwa heshima na Chid ukizingatia amemuacha kiumri mbali sana.Lakini wengine wanadai Chid alimvimbia Lady Jaydee kuna baadhi ya gharama za ziada alikuwa anahitaji ikiwemo nguo za kushutia video,nauli nk maana kipindi hicho alienda Kenya kwenye show ,,Jide akaona isiwe shida akamfuta.

Twende kazi,

Ikumbukwe pia Chidi siku za hivi karibuni amekuwa mtu wa malalamiko kila kukicha akilaumu wasanii wenzake kutomsaidia, mara amlaumu Diamond anarudisha wasanii wenzake nyuma maana anapenda kusujudiwa ,mara amlaumu Manara nk

Tazama moja ya video yake hapa chini 👇👇👇👇
View attachment 2843405View attachment 2843406

Sasa ghafla bin vuuuu 😂😂😂naona Ray C katoka huku mafichoni kaja kununua ugomvi kana kwamba ujumbe wa Lady Jaydee ulikuwa unamuhusu yeye.

Ray C akarusha kijembe kwa Jide kwamba heri ya yeye mla unga lakini amezaa kuliko Jide ambaye ni tasa.

Tazama hapa 👇👇👇👇

View attachment 2843408

Baada ya hicho kijembe Cha Ray C ,Jide akaja tena kujibu mashambulizi .

Tazama tena 👇👇👇👇

View attachment 2843410

Mashabiki nao hawakuwa nyuma ,wametoa nao michango yao.

Tazama 👇👇👇
View attachment 2843411

View attachment 2843413

Ikumbukwe bifu la Jaydee na Ray C lilidumu kwa muda mrefu kipindi hicho sababu kuu inayoaminika na wengi ilikuwa kugombania kuwa juu kila mmoja kuona yupo juu kuliko mwenzake.

Baadaye hilo bifu liliisha na wakafanya wimbo wa pamoja unaoitwa Namlaumu kama sikosei.

Wakawa marafiki kimtindo na kushirikiana mambo mbalimbali kutembeleana nk.

Tazama hapa picha Yao ya pamoja.


View attachment 2843414

Tunangojea majibu kutoka kwa Ray C tuone atajibu nini, tupo standby😂😂😂😂😂
Mwambie Ray C kama ameamua kupambana na 'teja' mwenzake basi wapambane wenyewe asianze habari za kumhusisha mtoto kwamba eti yeye sasa ana mtoto.
Amuweke mtoto nje ya ligi yao asijemchulia bure.
 
Kwenye kipaji, Jide kamuacha mbali sana Ray C

Tokea ametoka miaka ya 2000 Jide kaachia hit songs back to back mpaka leo hii, lakini Ray C nina hakika turudi hata 10 years nyuma niambie katoa hit song gani ndani ya huo muda hakika hutaiona. . .

Hivyo Jide ndio Malkia

Tukija kwenye hii tweet, Ray C ana kiherehere tu ina maana hafatilii kinachoendelea kiasi kutojua kuwa ile tweet Jide alimjibu chuma??

Al in all, Jide 95% Ray C 5%
 
Back
Top Bottom