Kisa kipi kilikufanya ujute sana?


Na hujaacha kusnitch
 

Judy wako yupo Moro nowadays analewa daily
 
Hii sio jiteute kweli kwa akina afande mrocky na nziku?
 
HAKUNA lisilowezekana chini ya jua...

Akikushinda kwa nguvu ..wewe mtege kwa nyavu..hata Kama ita kuchukua miaka...

Unaishi maisha gani mkuu hayo?!
 
Miakankadhaa nyuma... mida ya jioni niko na wanangu tunazurul tu mtaani ghafla mwana anasema tupite home kwao kidogo kuna nshu kasahau then tuendelee misele kukagua mitaa...

Kwao geti kali wana walinzi wamasai na nini... tumekaa zetu ubarazani tunamsubiri mwana atoke ndani tusepe huku tunapiga story na masai mlinzi..

Story zikiendelea ghafla masai anatoa kichupa kina unga mweusi amaweka mdomoni tunamuukiza oya nini hiyo unaweka mdomoni Masai anasema chkua weka na ww rafiki utafurahi...

daaah sitakuja kisahau hii siku asee since that day i hv been addicted to snuff na inanikwamisha mambo kibao yani...

Hii mambo ya kujaribu jaribu kila kitu sio poa... unaweza haribu future yako yako yote kifala sana
 
Ukila single mother kesho yake akikupigia anakwambia msalimie mwanao.
True na huyu bibie alikuwa kila akinipigia simu anataka nisalimie wajukuu zake...alikuwa ananichosha sana kwa kulazimisha mapenzi yasiyokuwepo
 
Ngada,Ugolo na sigara wanasema ukijaribu huachi,kaa mbali navyo
 
Mkuu unaonekana una vielement vya kutaka upate kiurahisi au utapeli kabisa maana ukianzia na payslip za kufoji ukiwa chuo na ukajuta hutakuja kufanya mishe nyeusi na ukarudia tena, wewe sio wa mazoea Kwa pesa unabadirika muda wowote
 
Sasa broo si ungeendeleza tu hicho kipaji maana sio kazi rahisi kumtembezea bapa za panga binadamu hata kama unalipa kisasi inatakiwa ujasiri wa hali ya juu[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Inavyoonekana una hako kakipaji ulipaswa uanzishe kijiwe cha kukaba ungetoboa fasta tu
 
Mkuu unaonekana una vielement vya kutaka upate kiurahisi au utapeli kabisa maana ukianzia na payslip za kufoji ukiwa chuo na ukajuta hutakuja kufanya mishe nyeusi na ukarudia tena, wewe sio wa mazoea Kwa pesa unabadirika muda wowote
Na ndio mwanaume unapaswa kuwa hvo mkuu.
 
Mkuu unaonekana una vielement vya kutaka upate kiurahisi au utapeli kabisa maana ukianzia na payslip za kufoji ukiwa chuo na ukajuta hutakuja kufanya mishe nyeusi na ukarudia tena, wewe sio wa mazoea Kwa pesa unabadirika muda wowote
Kila anayeishi anapenda urahisi. Unadhani ungepewa uwezo wa kubadilisha maisha yako kwa ku.click vidole vyako viwili usingefanya hivyo?

Unajua kwanini vijana wengi wanaingia ki rahisi kwenye Betting? Forex? Au kwanini watu wengi walizama kirahisi kwenye Forever Living? Four Corners? Global Alliance? DU? ... Ni for obvious reason, kupata mafanikio kirahisi!

Je ni wapumbavu kwa kufanya hivyo hadi wengine wakaishia kutapeliwa na kupoteza pesa zao huko? Hapana, sio wapumbavu, bali ni Binadamu, na akili zetu zimesukwa ili kutulinda sisi tusiteseke. Kwaiyo inapotokea njia mbili mbele na moja ikaonekana ni ngumu, automatically lazima tupite ile rahisi (shortcuts).

So yes, anyday kwenye haya maisha nitachagua an easy way out ikiji present mbele yangu. But saivi nitachagua kwa umakini zaidi kwa kuzingatia mambo mengi ya ki usalama (kisheria). Kama wewe unadhani you can make it in this life by playing too safe, good luck with that.
 
Ila ndio wanaume inapaswa tuwe hivo, unacheza na fursa tu.
 
BETTING

Waliotutangulia huku duniani waliandika kuwa betting au uwekezaji kwa lugha ya kibiashara dunia ya leo sio kitu cha kutegemea ki uchumi kwa sababu hakitabiriki na huwezi kuwa master katika career hii. Hivyo basi ni muhimu kutafuta kazi inayotumia skills ambayo unaweza kui master kwenye kutafuta pesa kuliko kutegemea mambo ya kubahatisha.

Looh, sikuwahi kuelewa walimaanisha nini kwa kipindi kile. Japo nilikuja kuelewa in a hard way!


Miaka kadhaa nyuma, wakati mambo ya kubet yameanza kutaradadi nakumbuka kulikua na vi ofisi flan town ukipita unakuta watu wamejazana huko hadi wameunga foleni ukichungulia kwa ndani unaona maandishi yanayo wakawaka yanapita kwa juu hata huelewi ni nini. Una amua kuuliza unaambiwa watu wanacheza kamari. Duh, kusikia kamari unachanja mbuga maana kwa wakati ule neno "kamari" lilikua linaogopesha sana sio kama saivi.

Basi bhana, nikawa naishia tu kuangalia kwa mbali. Miaka ikasonga, betting ikazidi kukuwa, makampuni yakaanza kuongezeka, mpaka ikafika mahali karibu kila siku nikiwa kwenye mgahawa nakunywa chai siachi kuona washkaji wana vikaratasi vyeupe virefu (nilikuja kujua baadae sana vinaitwa mikeka).

Punde si punde nikaanza kusikia story za fulani kavunja Milioni kadhaa, fulani kavunja laki kadhaa, Daah. Katamaa kakaanza ku beep kwa mbali. Nikasema kwani nini mbaya kujua hii michezo inachezwaje acha niulize kidogo.

Mwana akanielewesha kuhusu hiyo michezo sema binafsi nikawa interested zaidi na betting ya soccer. Kwa sababu niliona ina uwazi. Mpira hauna longolongo, timu ikishinda kila mtu anajua kwa hiyo si rahisi kutapeliwa.

Muda ukaenda, story za watu kuvunja hela zikawa zinazidi kuwa nyingi. Ikafika mahali nikawa kama naanza kujiskia vibaya. Naona kama ni mimi peke yangu tu ndio nimebaki sina hela. Walivyokuja Meridian na system yao ya online betting, dah nikajikuta na mimi nimo ndani.

Duuh, kumbe nilikua natamani kubet sema nilikua naona aibu kuonekana hadharani. Sasa hii ya online najua hakuna mtu anaweza kunisanukia kama nacheza hata nikishinda ni siri yangu. Heheee! Sijawahi kushinda kitu! Hata mia! Kwaiyo maumivu yakawa ni ndani kwa ndani.


Betting ina addiction mbaya sana. Unaanza kujua umesha athirika na Betting pale tu unapoanza ku chase loss. Yani unapoanza kuweka hela haraka haraka ili kurudisha pesa uliyopoteza. Nakumbuka kuna kipindi nilikua hadi nakopa pesa nabetia na inaliwa yote. Pesa ya kodi nabetia inaondoka yote. Kila mahali ni madeni. Halafu kibaya zaidi hata nikipokea hela kidogo kazini naona uzito kwenye kulipa yale madeni napata wazo la kuweka mkeka hata wenye odds 4 tu ili pesa ijae nimalize madeni yote kwa mara moja lakini wapi. Yote imeenda na maji. Nikawa depressed!

Walioniamini na kunikopesha wakaanza kuniona mtu wa ajabu sana, nafanya kazi napokea hela, silipi madeni ya watu kwa makusudi. Kumbe hela yenyewe ya kazi inaishia kwenye mikeka. Baadhi ya wadeni wangu wakachoshwa na sound zangu, wakaji organize wakaja ghetto wakabeba vitu hadi simu yangu wakapita nayo na bado wakanipa tarehe ya kumalizia madeni yaliyobaki la sivyo watanishtaki hadi kazini. Dah mambo ya aibu!


Nikaapa naacha kubet rasmi. Of course bado nilikua nataka kuendelea sema hata simu ya kubetia nilishanyang'anywa, na kwenda vibandani siwezi maana nafanya kwa siri. Nikapiga kazi mpaka nikamaliza madeni yote kwa kipindi kirefu sana. Na ki ukweli hakuna kitu kilikua kinaniumiza kama kulipia madeni ambayo sijafanyia kitu. Bora hata zile hela nilizokopa ningekua nimekula. Zote zilipotelea huko kwenye mikeka!

Muda ukaenda mpaka nikafanikiwa kununua simu nyingine ya smartphone. Siku moja napitapita huko Instagram, mara pap nakutana na mtu kashika bango la milioni 30 za Sportpesa, Daah vinyweleo vikasimama tena!

Nikasoma soma comments nikaona kama kila mtu anampa hongera nikaona hawa jamaa watakua legits, nikasahau yaliyonikuta huko nyuma nikaona nijiunge nao chap. Walikua na mchezo wao mmoja wanaita Jackpot, ukikosea mechi kidgo katika zote 13 wanakupa hela. Sa ngapi nisijaribu niotee 12. Duh Milion 10 na ushee hizi hapa. Nikaona kama ni utani.

Mara jamaa wakanipigia simu wakaniambia niende ofisini kwao wakahakiki taarifa zangu wanipe mpunga. Kweli nikafika nikamalizana nao, mpunga ukaingia kwenye account. Nikasema dah, elf mbili tu imenipa Mita 10. Maisha si ndio haya. Heheee.


Kilichonikuta na hizo Mil 10 ni story for another day!
 

Mkuu malizia[emoji23]visa vyako vinakuaga noma sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…