Nauliza, ni kisimbuzi gani cha ndani ambacho kitarusha kombe la Dunia la mwaka huu?
Miaka ya nyuma tulikuwa tunaona shamrashamra za matangazo kwenye visimbuzi vya ndani mfano Startimes kwamba watarusha, lakini mwaka huu kimya na zimebaki siku kadhaa!
CCM tulishawashauri, Watanzania tunapenda mpira ambapo husahau mambo mengine, hivyo CCM wajitahidi kadri wawezavyo wawasaidie visimbuzi vya ndani (local) au Channel Ten na Channel Ten Plus wanunue haki za kurusha matangazo ya Kombe la Dunia ili wananchi wasipate muda wa kufuatilia mambo ya nchi!
Sasa kama CCM wanaanza kupuuza hadi michezo hasa soka, naona wanajitengenezea bomu, maana kwa sasa kitu pekee kinachowazubaisha Watanzania ni mpira!
CCM toeni hela visimbuzi au chaneli yenu irushe kombe la Dunia hata bure! Msijisahau sana!
Miaka ya nyuma tulikuwa tunaona shamrashamra za matangazo kwenye visimbuzi vya ndani mfano Startimes kwamba watarusha, lakini mwaka huu kimya na zimebaki siku kadhaa!
CCM tulishawashauri, Watanzania tunapenda mpira ambapo husahau mambo mengine, hivyo CCM wajitahidi kadri wawezavyo wawasaidie visimbuzi vya ndani (local) au Channel Ten na Channel Ten Plus wanunue haki za kurusha matangazo ya Kombe la Dunia ili wananchi wasipate muda wa kufuatilia mambo ya nchi!
Sasa kama CCM wanaanza kupuuza hadi michezo hasa soka, naona wanajitengenezea bomu, maana kwa sasa kitu pekee kinachowazubaisha Watanzania ni mpira!
CCM toeni hela visimbuzi au chaneli yenu irushe kombe la Dunia hata bure! Msijisahau sana!