Red Giant
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 15,657
- 20,967
- Thread starter
- #21
SURA YA KUMI NA NNE: MTU WA KISIWANI.
Kwenye mteremko wa kilima nilisikia kokoto zikiteremka; nikaona kiumbe kinakuja kwa kasi, sikujua kama alikuwa ni mnyama au binadamu, . Nikazidi kutazama, nikaona ni kama nyani kwa kuwa uso wake ulikuwa na nywele nyingi, na moyo ukanipiga kwa hofu nisiweze hata kumeza mate. Sasa nikajiona kweli nimo hatarini, nyuma yangu kuna mabaharia wauaji, na mbele yangu kuna kiumbe anayetisha; nikaanza kurudi nyuma kwenye hatari nilizozijua kuliko kwenda mbele kwenye hatari nisizozijua. Nikaanza kurudi lakini kile kiumbe kilinizungulca kipate kunikata njia mbele yangu. Basi nikachoka sana, lakini hata ingekuwa sikuchoka, nisingeweza kushindana nacho kwa jinsi kilivyoweza kuruka na kwenda mbio.Nilipotazama
sana nikaona kuwa ni binadamu; nikaanza kukumbuka habari nilizozisikia za watu wanaokula watu, nikakaribia kupiga yowe kwa hofu.
Hata nilipofikiri nikaona kuwa huyu ni mtu tu, basi nikajipa moyo nikaanza kumkaribia. Yeye alijificha nyuma ya mti mnene. Mimi nikienda mbele yeye hurudi nyuma na kujificha nyuma ya miti. Mradi tukaendelea vivi hivi. Mwishowe alinyosha mikono na kupiga magoti, kama mtu anayesihi, nami nikasimama na kumwuliza, “Nani wewe?”Akajibu lakini sauti iikuwa imefifia kama sauti ya mtu asiyezoea kusema kwa siku nyingi, “Mimi ni Ben Gun. Sasa yapata miaka mitatu sikusema na binadamu.”
Basi katika kumtazama zaidi nikaona kuwa sura yake ilikuwa nzuri, tena ni mweupe kama mimi, lakini kwa sababu ya jua kali amegeuka rangi. Nguo zilitatukatatuka na ndevu zake zilikuwa ndefu sana. Nikasema, “Miaka mitatu! Loo! Kwani ulisukumiwa hapa na mawimbi?”
Akajibu, “Rafiki yangu, nilitupwa hapa na wanadamu miaka mitatu iliyopita, na tangu wakati huo ninaponea wadudu ya porini na chaza wa baharini. Sasa natamani sana kula chakula cha kwetu cha kizungu. Mara nyingi nikilala huota ndoto za chakula.”
Basi nikamwambia, “Vema, kama nikijaaliwa kurudi tena melini,
nakuahidi kuwa utashiba kwa chakula kizuri.”
Akajibu, “Wasema ukijaaliwa kurudi tena melini. Je, kwani kitu gani kitakachokuzuia usirudi?” Basi tukaongea kidogo, kisha akainamisha kichwa chake karibu na sikio langu kuninong’oneza; akasema, “Mimi ni tajiri sana, nina mali nyingi nami nitakutajirisha kwa sababu wewe ni mtu wa kwanza uliyeniona.” Kisha akakunja uso na kusema, “Sasa niambie kweli, meli ile si meli ya Flinti?”
Nikamwambia, “Meli ile si meli ya Flinti, na yeye Flinti mwenyewe amekwisha kufa lakini mabaharia wake wamo ndani ya ile meli.” Akauliza “Je, yumo mmoja mwenye mguu mmoja?”
Nikajibu, “Ndiyo, huyo
ni John Fedha.”Kisha akasema, “Ikiwa wewe umetumwa na mtu huyo basi nimekwisha kufa.” Sasa nikaona afadhali nimwambie habari zote. Nikaanza kumweleza tokea mwanzo mpaka mwisho. Basi akasema, “Ama wewe
ni kijana mzuri nami sina haja ya kuogopa, wala wewe nawe usiniogope, niamini tu. Mimi napajua mahali palipofichwa hazina zote. Zilifichwa na Flinti na watu wake sita, na alipokwisha kuzificha aliwaua wote sita. Basi baada ya miaka mitatu nilikuwa katika meli nyingine tukipita njia hii hii; kuona kisiwa tu nikasema, ‘Rafiki, hazina za Flinti zilifichwa katika kisiwa hiki.Twendeni tukazifukue.’ Nahodha akakasirika sana na kutugombeza lakini mimi pamoja na mabaharia wengine tukashuka pwani kutafuta hazina. Muda
wa siku kumi na mbii tulitafuta tusiivumbue, tukarudi melini. Tulipofika melini, Nahodha akasema, ‘Wewe Ben Gun sikutaki tena, chukua bunduki na baruti urudi kisiwani ukazitafute hazina peke yako.’ Basi wakaniacha hapa kisiwani, na hapa nimekaa sasa muda wa miaka mitatu. Basi sasa tukiisha fika melini nataka ueleze yote niliyokwambia, maana naona haya kwa hali yangu ilivyo. Tena ninayo mashua nimeificha karibu na hori.”
Mara tukasikia mlio wa mzinga, akaniuliza, “Nini hicho?”
Nikasema, “Nadhani wameanza vita! Nifuate.”
Basi nikaanza kukimbilia kule kulikokuwa na meli, na yeye akanifuata. Baada ya kitambo kidogo tukasikia bunduki zinapigwa na baada ya kukimbia kidogo, nikaona mbele yangu bendera ya Uingereza inapepea juu.
(Wasomaji lazima wafahamu ya kuwa mpaka hapo aliyesimulia hadithi ni yule kijana anayeitwa Jim Hawkins. Sasa yeye anaacha kusimulia na Bwana Daktari ameshika zamu ya kuhadithia mambo yaliyotokea.)
SURA YA KUMI NA TANO:
(Bwana Daktari anaendelea
kusimulia hadithi)
TWAFANYA SHAURI KUTOKA MELINI.
Twafanya shauri kutoka melini Ilikuwa saa saba na nusu mabaharia walipokwenda kutembea pwani. Nahodha na Bwana Treloni na mimi tulikuwa tukiongea katika shetri. Kama upepo ungalikuwako nadhani tungaliwapiga mabaharia wale waliobaki melini tukang’oa nanga kwenda zetu. Lakini upepo haukuwako na zaidi ya hayo tulisikia kuwa mwenzetu mmoja, Jim Hawkins alishuka pwani pamoja na mabaharia.
Hatukufikiri kuwa Jim Hawkins ameasi ila tulikuwa na wasiwasi kuwa labda huko atadhurika, hasa kwa sababu mabaharia wamekasirika. Basi tukaenda sitahani kutazama pwani, tukaona mabaharia wamekwisha teremka pwani na wawili wamebaki mashuani kulinda zamu. Wale sita waliobakia melini walikaa gubetini wakizungumza huku wamejaa chuki. Kungojea huku kulikuwa kubaya sana, nikawa sina budi kushuka pwani na baharia mmoja jina lake Hunta. Tukaingia mashuani, tukavuta makasia mpaka tukafika pwani. Wale watu wawili waliokuwa wakilinda zamu walipotuona wakaingiwa na shaka, tukawaona kama wanaofanya mashauri ya kufanya jambo, lakini mwishowe wakakaa tu. Na sisi tulishuka pwani kwa mbali kidogo na mahali pale waliposhukia wale mabaharia. Sasa nikaanza kutembeatembea na hapo ndipo nilipoona boma lenyewe. Hilo boma lilikuwa limejengwa kwa magogo na lilitosha kuingia hata watu arobaini, na sehemu ya nje kuzunguka boma palikuwa peupe sana. Boma liijengwa madhubuti sana, na ndani kulikuwa na kisima.
Basi nikapeleleza, nikaona kuwa watu wakiingia katika boma hili hawana hofu kabisa kwa kuwa wataweza kuwazuia watu wanaowashambulia kabla hawajafika karibu na boma, maana walio ndani wataweza kuwapiga. Basi nikaona mahali hapa patatufaa sana, iliyobaki ni kuweka chakula cha kutosha tu.
Basi nilipokuwa nikifikiri, mara nikasikia sauti ya mtu kama amepigwa risasi; nikafikiri kuwa sasa Jim Hawkins amekufa. Basi nikafanya haraka kurudi kwenye mashua ili turudi melini. Hata nilipo fika pwani nikawakuta wenzangu wakitetemeka kwa hofu, na wale mabaharia nikawaona kuwa hata na wao wakiogopa sana. Basi tulipofika melini nikaeleza yote niliyoyaona na niliyokuwa nayo moyoni. Tukaanza kukusanya chakula na nyama kisha tukatia mashuani pamoja na bunduki na baruti.
Basi ikabaki kutengeneza shauri la mabaharia wale sita waliobakia melini. Nikamtuma mtu mmoja wa upande wetu, nikampa bunduki na nikamweka upande mmoja wa meli, huku nyuma Nahodha na Bwana Treloni wakazunguka upande wa pii, wakamwita mkubwa wa mabaharia wale wakamwambia: “Sisi watu wawili tupo hapa na mtu yeyote akifanya au akionyesha hata dalili ya uasi atakufa.”
Wakashangaa sana na baada ya kusemezana wenyewe kwa wenyewe wakazunguka kutaka kutokea kwa nyuma, lakini wapi! Walipokuwa wakizunguka wakamwona yule mtu tuliyemweka, wakashindwa. Basi Nahodha akawaamuru washuke chini, nao wakashuka.
Basi mimi na Hunta na mwingine jina lake Josi tukaingia katika mtubwi na tukavuta makasia na tukafika pwani tena. Wale mabaharia wawili walipotuona tumerudi safari ya pili pwani wakataharuki sana na mmoja akatoka mbio, nami nikajua kwamba alikwenda kupeleka habari kwa mkubwa wao, John Fedha.
Basi hivi tukafanya safari tatu,
na kila safari tukachukua chakula na nyama na dawa na bunduki na baruti mpaka tukaisha kuweka vitu vya kutosha katika lile boma. Nikawaacha watu wawili humo kulinda boma Hata yote yalipokuwa tayari, tukarudi tena melini, na kwa kuwa katika wale mabaharia sita waliobaki melini kulikuwa na mmoja niliyetaka afuatane nasi, maana nilimjua kuwa hayumo katika kushauriana na waasi, nikamwita na kumwambia, “Gray, kama ukitaka kuja njoo upesi. Sasa tunatoka melini, nami najua kuwa huafiki mipango ya waasi, basi njoo upesi.”
Kimya! Kimya!
Nikazidi kumwambia, “Haya ati!Kama wataka kuja njoo upesi; sasa twatoka.”Basi mara nikasikia ghasia, tena nikamwona akitoka mbio; nikatambua kuwa wengine walijaribu kumzuia.
SURA YA KUMI NA SITA:
(Hadithi ya Bwana Daktari)
SAFARI YA MWISHO YA MTUMBWI WETU.
Safari hii ilikuwa na hatari nyingi, maana mtumbwi ulikuwa mdogo nasi sote watu watano tulikuwa watu wazima na tena tumepakia chakula na vitu vingine. Basi kila mara mawimbi yalipokuja maji yalikuwa yakiingia ndani. Mradi tulikuwa katika hatari ya kuzama.
Lakini zaidi ya hayo tuliingia katika mkondo wa maji tukachukuliwa mbali kidogo, lakini tulipokaribia pwani nguvu za mkondo wa maji zikapungua, ikawa kazi nyepesi. Lakini hatari haikutuacha bado, maana tulisahau kuwa kuna mzinga melini. Tukawa mara kwa mara tukitazama nyuma; tukawaona wale mabaharia watano waliobaki melini wanaondoa turubali la mzinga. Basi sasa ikawa vimoto kabisa, na bwana Nahodha akauliza, “Je, nani aliye na shabaha barabara?”
Tukajibu, “Huyu Bwana Livesi, ndiye hodari kwa shabaha.”
“Vema, haya Bwana Livesi, twaa bunduki yako, mpige yule mtu mmoja na labda wale wengine wataogopa.” Basi akatwaa bunduki, akaelekeza
na kuipiga. Hakumpiga yule aliyekuwa tayari kupiga mzinga, maana ile risasi llimkosa, ikampiga mtu mmoja aliyekuwa amesimama karibu yake, akaanguka na kulia kwa sauti kubwa. Basi mara tukasikia wengine wakipiga kelele tukatazama pwani tukawaona mabaharia wale walioshuka zamani wote wanakuja mbio pwani. Basi sasa tukawa na haraka kufika pwani kabla hawajawahi kufika mahali tulipokusudia kushukia. Tukavuta makasia kwa nguvu zetu zote. Hata tulipokuwa karibu kufika pwani mara wale watu wa melini wakapiga mzinga na risasi yake ikapita juu, lakini kwa kishindo chake, mashua yetu ikazama. Kwa bahati tukawa tumekwisha fika karibu na pwani, maji ya magoti tu.
Basi tukatoka upesi tukaenda pwani, lakini hatukuwahi kuteremsha chakula
na vitu vinginevyo, ikawa tukapata hasara. Na katika zile bunduki zetu tano, mbili tu ndizo zilizokuwa hazikupata maji.
Tulipofika pwani hatari ikazidi, maana tulisikia sauti za watu wanaotoka upande wa boma letu; basi tukafanya haraka kwenda huko kunako boma tuone mambo gani yatakayotokea.
Kwenye mteremko wa kilima nilisikia kokoto zikiteremka; nikaona kiumbe kinakuja kwa kasi, sikujua kama alikuwa ni mnyama au binadamu, . Nikazidi kutazama, nikaona ni kama nyani kwa kuwa uso wake ulikuwa na nywele nyingi, na moyo ukanipiga kwa hofu nisiweze hata kumeza mate. Sasa nikajiona kweli nimo hatarini, nyuma yangu kuna mabaharia wauaji, na mbele yangu kuna kiumbe anayetisha; nikaanza kurudi nyuma kwenye hatari nilizozijua kuliko kwenda mbele kwenye hatari nisizozijua. Nikaanza kurudi lakini kile kiumbe kilinizungulca kipate kunikata njia mbele yangu. Basi nikachoka sana, lakini hata ingekuwa sikuchoka, nisingeweza kushindana nacho kwa jinsi kilivyoweza kuruka na kwenda mbio.Nilipotazama
sana nikaona kuwa ni binadamu; nikaanza kukumbuka habari nilizozisikia za watu wanaokula watu, nikakaribia kupiga yowe kwa hofu.
Hata nilipofikiri nikaona kuwa huyu ni mtu tu, basi nikajipa moyo nikaanza kumkaribia. Yeye alijificha nyuma ya mti mnene. Mimi nikienda mbele yeye hurudi nyuma na kujificha nyuma ya miti. Mradi tukaendelea vivi hivi. Mwishowe alinyosha mikono na kupiga magoti, kama mtu anayesihi, nami nikasimama na kumwuliza, “Nani wewe?”Akajibu lakini sauti iikuwa imefifia kama sauti ya mtu asiyezoea kusema kwa siku nyingi, “Mimi ni Ben Gun. Sasa yapata miaka mitatu sikusema na binadamu.”
Basi katika kumtazama zaidi nikaona kuwa sura yake ilikuwa nzuri, tena ni mweupe kama mimi, lakini kwa sababu ya jua kali amegeuka rangi. Nguo zilitatukatatuka na ndevu zake zilikuwa ndefu sana. Nikasema, “Miaka mitatu! Loo! Kwani ulisukumiwa hapa na mawimbi?”
Akajibu, “Rafiki yangu, nilitupwa hapa na wanadamu miaka mitatu iliyopita, na tangu wakati huo ninaponea wadudu ya porini na chaza wa baharini. Sasa natamani sana kula chakula cha kwetu cha kizungu. Mara nyingi nikilala huota ndoto za chakula.”
Basi nikamwambia, “Vema, kama nikijaaliwa kurudi tena melini,
nakuahidi kuwa utashiba kwa chakula kizuri.”
Akajibu, “Wasema ukijaaliwa kurudi tena melini. Je, kwani kitu gani kitakachokuzuia usirudi?” Basi tukaongea kidogo, kisha akainamisha kichwa chake karibu na sikio langu kuninong’oneza; akasema, “Mimi ni tajiri sana, nina mali nyingi nami nitakutajirisha kwa sababu wewe ni mtu wa kwanza uliyeniona.” Kisha akakunja uso na kusema, “Sasa niambie kweli, meli ile si meli ya Flinti?”
Nikamwambia, “Meli ile si meli ya Flinti, na yeye Flinti mwenyewe amekwisha kufa lakini mabaharia wake wamo ndani ya ile meli.” Akauliza “Je, yumo mmoja mwenye mguu mmoja?”
Nikajibu, “Ndiyo, huyo
ni John Fedha.”Kisha akasema, “Ikiwa wewe umetumwa na mtu huyo basi nimekwisha kufa.” Sasa nikaona afadhali nimwambie habari zote. Nikaanza kumweleza tokea mwanzo mpaka mwisho. Basi akasema, “Ama wewe
ni kijana mzuri nami sina haja ya kuogopa, wala wewe nawe usiniogope, niamini tu. Mimi napajua mahali palipofichwa hazina zote. Zilifichwa na Flinti na watu wake sita, na alipokwisha kuzificha aliwaua wote sita. Basi baada ya miaka mitatu nilikuwa katika meli nyingine tukipita njia hii hii; kuona kisiwa tu nikasema, ‘Rafiki, hazina za Flinti zilifichwa katika kisiwa hiki.Twendeni tukazifukue.’ Nahodha akakasirika sana na kutugombeza lakini mimi pamoja na mabaharia wengine tukashuka pwani kutafuta hazina. Muda
wa siku kumi na mbii tulitafuta tusiivumbue, tukarudi melini. Tulipofika melini, Nahodha akasema, ‘Wewe Ben Gun sikutaki tena, chukua bunduki na baruti urudi kisiwani ukazitafute hazina peke yako.’ Basi wakaniacha hapa kisiwani, na hapa nimekaa sasa muda wa miaka mitatu. Basi sasa tukiisha fika melini nataka ueleze yote niliyokwambia, maana naona haya kwa hali yangu ilivyo. Tena ninayo mashua nimeificha karibu na hori.”
Mara tukasikia mlio wa mzinga, akaniuliza, “Nini hicho?”
Nikasema, “Nadhani wameanza vita! Nifuate.”
Basi nikaanza kukimbilia kule kulikokuwa na meli, na yeye akanifuata. Baada ya kitambo kidogo tukasikia bunduki zinapigwa na baada ya kukimbia kidogo, nikaona mbele yangu bendera ya Uingereza inapepea juu.
(Wasomaji lazima wafahamu ya kuwa mpaka hapo aliyesimulia hadithi ni yule kijana anayeitwa Jim Hawkins. Sasa yeye anaacha kusimulia na Bwana Daktari ameshika zamu ya kuhadithia mambo yaliyotokea.)
SURA YA KUMI NA TANO:
(Bwana Daktari anaendelea
kusimulia hadithi)
TWAFANYA SHAURI KUTOKA MELINI.
Twafanya shauri kutoka melini Ilikuwa saa saba na nusu mabaharia walipokwenda kutembea pwani. Nahodha na Bwana Treloni na mimi tulikuwa tukiongea katika shetri. Kama upepo ungalikuwako nadhani tungaliwapiga mabaharia wale waliobaki melini tukang’oa nanga kwenda zetu. Lakini upepo haukuwako na zaidi ya hayo tulisikia kuwa mwenzetu mmoja, Jim Hawkins alishuka pwani pamoja na mabaharia.
Hatukufikiri kuwa Jim Hawkins ameasi ila tulikuwa na wasiwasi kuwa labda huko atadhurika, hasa kwa sababu mabaharia wamekasirika. Basi tukaenda sitahani kutazama pwani, tukaona mabaharia wamekwisha teremka pwani na wawili wamebaki mashuani kulinda zamu. Wale sita waliobakia melini walikaa gubetini wakizungumza huku wamejaa chuki. Kungojea huku kulikuwa kubaya sana, nikawa sina budi kushuka pwani na baharia mmoja jina lake Hunta. Tukaingia mashuani, tukavuta makasia mpaka tukafika pwani. Wale watu wawili waliokuwa wakilinda zamu walipotuona wakaingiwa na shaka, tukawaona kama wanaofanya mashauri ya kufanya jambo, lakini mwishowe wakakaa tu. Na sisi tulishuka pwani kwa mbali kidogo na mahali pale waliposhukia wale mabaharia. Sasa nikaanza kutembeatembea na hapo ndipo nilipoona boma lenyewe. Hilo boma lilikuwa limejengwa kwa magogo na lilitosha kuingia hata watu arobaini, na sehemu ya nje kuzunguka boma palikuwa peupe sana. Boma liijengwa madhubuti sana, na ndani kulikuwa na kisima.
Basi nikapeleleza, nikaona kuwa watu wakiingia katika boma hili hawana hofu kabisa kwa kuwa wataweza kuwazuia watu wanaowashambulia kabla hawajafika karibu na boma, maana walio ndani wataweza kuwapiga. Basi nikaona mahali hapa patatufaa sana, iliyobaki ni kuweka chakula cha kutosha tu.
Basi nilipokuwa nikifikiri, mara nikasikia sauti ya mtu kama amepigwa risasi; nikafikiri kuwa sasa Jim Hawkins amekufa. Basi nikafanya haraka kurudi kwenye mashua ili turudi melini. Hata nilipo fika pwani nikawakuta wenzangu wakitetemeka kwa hofu, na wale mabaharia nikawaona kuwa hata na wao wakiogopa sana. Basi tulipofika melini nikaeleza yote niliyoyaona na niliyokuwa nayo moyoni. Tukaanza kukusanya chakula na nyama kisha tukatia mashuani pamoja na bunduki na baruti.
Basi ikabaki kutengeneza shauri la mabaharia wale sita waliobakia melini. Nikamtuma mtu mmoja wa upande wetu, nikampa bunduki na nikamweka upande mmoja wa meli, huku nyuma Nahodha na Bwana Treloni wakazunguka upande wa pii, wakamwita mkubwa wa mabaharia wale wakamwambia: “Sisi watu wawili tupo hapa na mtu yeyote akifanya au akionyesha hata dalili ya uasi atakufa.”
Wakashangaa sana na baada ya kusemezana wenyewe kwa wenyewe wakazunguka kutaka kutokea kwa nyuma, lakini wapi! Walipokuwa wakizunguka wakamwona yule mtu tuliyemweka, wakashindwa. Basi Nahodha akawaamuru washuke chini, nao wakashuka.
Basi mimi na Hunta na mwingine jina lake Josi tukaingia katika mtubwi na tukavuta makasia na tukafika pwani tena. Wale mabaharia wawili walipotuona tumerudi safari ya pili pwani wakataharuki sana na mmoja akatoka mbio, nami nikajua kwamba alikwenda kupeleka habari kwa mkubwa wao, John Fedha.
Basi hivi tukafanya safari tatu,
na kila safari tukachukua chakula na nyama na dawa na bunduki na baruti mpaka tukaisha kuweka vitu vya kutosha katika lile boma. Nikawaacha watu wawili humo kulinda boma Hata yote yalipokuwa tayari, tukarudi tena melini, na kwa kuwa katika wale mabaharia sita waliobaki melini kulikuwa na mmoja niliyetaka afuatane nasi, maana nilimjua kuwa hayumo katika kushauriana na waasi, nikamwita na kumwambia, “Gray, kama ukitaka kuja njoo upesi. Sasa tunatoka melini, nami najua kuwa huafiki mipango ya waasi, basi njoo upesi.”
Kimya! Kimya!
Nikazidi kumwambia, “Haya ati!Kama wataka kuja njoo upesi; sasa twatoka.”Basi mara nikasikia ghasia, tena nikamwona akitoka mbio; nikatambua kuwa wengine walijaribu kumzuia.
SURA YA KUMI NA SITA:
(Hadithi ya Bwana Daktari)
SAFARI YA MWISHO YA MTUMBWI WETU.
Safari hii ilikuwa na hatari nyingi, maana mtumbwi ulikuwa mdogo nasi sote watu watano tulikuwa watu wazima na tena tumepakia chakula na vitu vingine. Basi kila mara mawimbi yalipokuja maji yalikuwa yakiingia ndani. Mradi tulikuwa katika hatari ya kuzama.
Lakini zaidi ya hayo tuliingia katika mkondo wa maji tukachukuliwa mbali kidogo, lakini tulipokaribia pwani nguvu za mkondo wa maji zikapungua, ikawa kazi nyepesi. Lakini hatari haikutuacha bado, maana tulisahau kuwa kuna mzinga melini. Tukawa mara kwa mara tukitazama nyuma; tukawaona wale mabaharia watano waliobaki melini wanaondoa turubali la mzinga. Basi sasa ikawa vimoto kabisa, na bwana Nahodha akauliza, “Je, nani aliye na shabaha barabara?”
Tukajibu, “Huyu Bwana Livesi, ndiye hodari kwa shabaha.”
“Vema, haya Bwana Livesi, twaa bunduki yako, mpige yule mtu mmoja na labda wale wengine wataogopa.” Basi akatwaa bunduki, akaelekeza
na kuipiga. Hakumpiga yule aliyekuwa tayari kupiga mzinga, maana ile risasi llimkosa, ikampiga mtu mmoja aliyekuwa amesimama karibu yake, akaanguka na kulia kwa sauti kubwa. Basi mara tukasikia wengine wakipiga kelele tukatazama pwani tukawaona mabaharia wale walioshuka zamani wote wanakuja mbio pwani. Basi sasa tukawa na haraka kufika pwani kabla hawajawahi kufika mahali tulipokusudia kushukia. Tukavuta makasia kwa nguvu zetu zote. Hata tulipokuwa karibu kufika pwani mara wale watu wa melini wakapiga mzinga na risasi yake ikapita juu, lakini kwa kishindo chake, mashua yetu ikazama. Kwa bahati tukawa tumekwisha fika karibu na pwani, maji ya magoti tu.
Basi tukatoka upesi tukaenda pwani, lakini hatukuwahi kuteremsha chakula
na vitu vinginevyo, ikawa tukapata hasara. Na katika zile bunduki zetu tano, mbili tu ndizo zilizokuwa hazikupata maji.
Tulipofika pwani hatari ikazidi, maana tulisikia sauti za watu wanaotoka upande wa boma letu; basi tukafanya haraka kwenda huko kunako boma tuone mambo gani yatakayotokea.