Ukiwa mzima ni rahisi kusema ugonjwa huu ni bora kuliko huu
Kuna magonjwa yamekuja kwa kasi kwa sasa kama kansa na sugar ukipata sukari ni hatari maana ukipata kidonda kupona ni kazi pia inakimbilia chini, huwezi kufanya kwa ufanisi tendo la ndoa kwa kansa kupona haiwezekani labda kwa maombi.
Pia serekali imewatupa watu hawa maana dawa zake ni gharama sana za kupunguza makali ila sasa kwenye ukimwi dawa huu ugonjwa ukitumia dawa vizuri za kupunguza makali unaweza ishi miaka 30 ila umekua ugonjwa wanaougopa sana tofauti na kansa presha na kisukari hii inatokana na nini wadau?
sababu wanaamini ni ugonjwa unatokana na ngono zembe wanaona aibu
Ukimwi unaambukiza. Hayo magonjwa mengine hayaambukizwi.
Kama UKIMWI ungekuwa ugonjwa ningeuogopa kuliko hata kifo...lkn kwa sababu umechanganya UKIMWI na magonjwa hapo juu mm naogopa magonjwa kuliko UKIMWI.