Kisukari, presha na kansa ni hatari, kwanini watu wanaogopa UKIMWI zaidi?

Kisukari, presha na kansa ni hatari, kwanini watu wanaogopa UKIMWI zaidi?

manSniper

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2015
Posts
814
Reaction score
680
Kuna magonjwa yamekuja kwa kasi kwa sasa kama kansa na sugar ukipata sukari ni hatari maana ukipata kidonda kupona ni kazi pia inakimbilia chini, huwezi kufanya kwa ufanisi tendo la ndoa kwa kansa kupona haiwezekani labda kwa maombi.

Pia serekali imewatupa watu hawa maana dawa zake ni gharama sana za kupunguza makali ila sasa kwenye ukimwi dawa huu ugonjwa ukitumia dawa vizuri za kupunguza makali unaweza ishi miaka 30 ila umekua ugonjwa wanaougopa sana tofauti na kansa presha na kisukari hii inatokana na nini wadau?
 
Kansa na kisukari ni hatari sana kuliko hata huo ukimwi,
Kwanza saratani/kansa kufa ndio kupona kwako, kisukari masharti ni mengi mara usile hiki ila kula hiki pekee,

UKIMWI unaruhusiwa kula vingi sana pia hauna mateso kama kisukari labda mhusika asizingatie maelekezo ya daktari,

All in all ugonjwa ni ugonjwa tu, jilinde pia kula vizuri na mazoezi ili kuepuka kisukari na saratani,
 
Hatuna elimu ya kutosha juu ya haya magonjwa ndio maana mtu akisiki kansa anaona bora kumbe unateseka mpaka siku ya kufa lakini ukiwa na UKIMWI fuata mashrti tu hata wazima wataondoka wewe ukiwaangalia tu
 
"Walioamini kuwa UKIMWI upo, ndiyo hao wanaishi kwa hisia za Babu" - Young Killer
 
Maradhi ya Kisukari yanasumbua sana, ni ugonjwa unaokuuwa bila kujua. Utasikia unaumwa kichwa mara miguu mara mgongo kutahamaki figo zimekufa. Mungu atuokoe.

Mimi ni mhanga namshukuru Mungu naendelea vizuri kwa sasa.
 
Kuna magonjwa yamekuja kwa kasi kwa sasa kama kansa na sugar ukipata sukari ni hatari maana ukipata kidonda kupona ni kazi pia inakimbilia chini, huwezi kufanya kwa ufanisi tendo la ndoa kwa kansa kupona haiwezekani labda kwa maombi.

Pia serekali imewatupa watu hawa maana dawa zake ni gharama sana za kupunguza makali ila sasa kwenye ukimwi dawa huu ugonjwa ukitumia dawa vizuri za kupunguza makali unaweza ishi miaka 30 ila umekua ugonjwa wanaougopa sana tofauti na kansa presha na kisukari hii inatokana na nini wadau?

kwa mawazo yangu naona elimu imetolewa zaidi kwenye ukimwi kuliko hayo magonjwa mengine
 
Kama UKIMWI ungekuwa ugonjwa ningeuogopa kuliko hata kifo...lkn kwa sababu umechanganya UKIMWI na magonjwa hapo juu mm naogopa magonjwa kuliko UKIMWI.
 
Kama UKIMWI ungekuwa ugonjwa ningeuogopa kuliko hata kifo...lkn kwa sababu umechanganya UKIMWI na magonjwa hapo juu mm naogopa magonjwa kuliko UKIMWI.
kwa nini mtu akiwa na kisukari ni rahisi kusema kwa jamii ila ukimwi hasemi
 
sababu wanaamini ni ugonjwa unatokana na ngono zembe wanaona aibu
 
Kama UKIMWI ungekuwa ugonjwa ningeuogopa kuliko hata kifo...lkn kwa sababu umechanganya UKIMWI na magonjwa hapo juu mm naogopa magonjwa kuliko UKIMWI.


Ahsante mkuu kwa kusawazisha, maana naona watu wanachanganya mambo hapa. UKIMWI sio 'ugonjwa', bali ni avenue/channel ya kuelekea kupata 'magonjwa'.

Watu huchanganya sana hivi vitu. Kuna wengine wanasema eti UKIMWI 'unaambukizwa'. lol
 
Back
Top Bottom