SoC02 Kiswahili ni Afrika Mashariki, Kiswahili ni Tanzania, Kiswahili ni Amani na Upendo

SoC02 Kiswahili ni Afrika Mashariki, Kiswahili ni Tanzania, Kiswahili ni Amani na Upendo

Stories of Change - 2022 Competition

BabaMorgan

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2017
Posts
4,869
Reaction score
13,137
HISTORIA YA KISWAHILI.
Kuna nadharia mbalimbali kuhusiana na historia ya lugha ya Kiswahili. Wapo wanaodai chimbuko la Kiswahili kuwa ni pwani ya Afrika mashariki, wataalamu kama Nae Freeman Granville (1959) kupitia kitabu chake kiitwacho (the medieval of Kiswahili language) anakuja na hoja kuwa Kilwa hata kabla ya karne ya 10 ilikuwa na umuhimu mkubwa kibiashara hivyo basi kulinganana na umuhimu huo wa biashara miongoni mwa wa wabantu wa kilwa na wageni(waarabu) ilipelekea kuibuka kwa lugha moja ambayo ndiyo inasadikika ni Kiswahili leo hii.

download (1).png


Nadharia nyingine ni kama asili ya Kiswahili ni huko Afrika ya magharibi(Kamerun) sababu kuu ni kuwa huko ndiko chimbuko la wabantu kabla ya kutawanyika kutokana na sababu mbalimbali na wapo wataalamu wanaosema kuwa chimbuko la Kiswahili ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Nadharia zote zaweza kuwa na mashiko kwa kuwa lugha ya Kiswahili ina maneno ya kibantu, kiarabu na baadhi ya maneno kutoka lugha tofauti kama kireno, kiingereza na kihindi kitu kilichochewa na muingiliano wa watu wa jamii tofauti kutokana na biashara pamoja na ujio wa wakoloni.

UMRI WA LUGHA YA KISWAHILI.
Lugha hii inakadirirwa kuwa na takribani na miaka 800 hadi 1000 toka kuanza kwake katika vituo vya biashara vya pwani ambako wafanyabiashara kutoka uarubuni, uajemi, na uhindi walipokutana na wenyeji wakazi wa Afrika.

Lugha ya Kiswahili iliweza kuzaliwa kutokana na wenyeji wabantu kupokea maneno mengi kutoka lugha tofauti hasa maneno ya kiarabu katika kuwasiliana.

DGd3TobXYAAqQX7.jpg

Kuenea kwa lugha ya kiswahili.
Kupitia biashara na muingiliano wa watu lugha ilianza kuenea sehemu mbalimbali za ulimwengu. wakati wa ukoloni lugha ya Kiswahili iliweza kusanifiwa na kamati ya kimaeneo ya lugha ya Kiswahili kwenye misingi wa lahaja ya unguja.

Kiswahili ni nini?
Kiswahili
ni lugha miongoni mwa lugha takribani elfu saba(7000) zinazozungumzwa ulimwenguni ikiwa inazungumzwa haswa katika eneo la Africa mashariki(Tanzania, Kenya, Uganda, Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo na kaskazini mwa Msumbiji).

Nchi zinazozungumza kiswahili.
Kiswahili ni lugha rasmi ya taifa katika nchi ya Tanzania na kenya. Uganda pia iliwahi kuwa lugha ya taifa wakati wa utawala wa Iddi amin matumizi ya Kiswahili yalipingwa na waganda kutokana na historia ya utawala wa kijeshi.

Mashariki mwa Kongo Kiswahili kimeenea sana na ni moja kati ya lugha nne za kitaifa katika jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Nchini Rwanda mnamo tarehe 8 februari 2017 bunge lilifanya Kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne baada ya Kinyarwanda, kifaransa na kiingereza.

Map-of-East-African-countries-Source-United-Nations-43.png


Mafanikio ya kiswahili.
Tarehe 23 mwezi novemba mwaka 2021 shirika la umoja wa mataifa la elimu,sayansi na utamaduni UNESCO lilitangaza rasmi tarehe 7 ya julai kila mwaka kuwa siku ya kiswahili duniani.

download.png


Ni moja katika hatua muhimu za mafanikio ya Kiswahili katika anga za kimataifa. Katika azimio hilo lenye kurasa tatu, inaelezwa kuwa uamuzi huo unatokana na uamuzi wa kikao cha 212 cha bodi utendaji ya UNESCO kwa kutumia misingi mikuu kumi ambayo ni:

1. Kiswahili ni mawasiliano.

2. Wazungumzaji wa Kiswahili duniani.

3. Kiswahili Afrika mashariki, kati na kusini.

4. Kiswahili na kufanikisha SDGs(Sustainable Development Goals) na AcFTA(Africa Continental Free Trade Area)

5. Kiswahili katika idhaa za umoja wa mataifa.

6. Umoja wa mataifa na matumizi ya lugha zaidi ya moja.

7. Kiswahili na utajiri katika utofauti wa kiisimu.

8. Kiswahili ni lugha rasmi ya SADC(Southern African Development Community)

9. Kwa nini 7/7 na si tarehe nyingine. Tarehe 7/7/1954 nisiku ambayo chama cha TANGANYIKA AFRICAN NATIONAL UNION(TANU) chini ya hayati mwalimu julias kambarage nyerere,rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kilipitisha Kiswahili kama lugha ya kuunganisha harakati za ukombozi.

10. Maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani

Mafanikio mengine ni kama
  • Kuwepo kwa vyombo vya habari kama televisheni,redio na hata magazeti kuanzia ngazi ya kitaifa mpaka kimataifa vinavyotumia lugha ya Kiswahili kuwasilisha maudhui kwa hadhira.
  • Kuwa lugha ya afrika ambayo ni lugha rasmi katika serikali ya Tanzania na jumuiya ya afrika mashariki.
  • Kuanzishwa kwa kozi mbalimbali za Kiswahili katika ngazi ya shahada katika vyuo vya elimu ya juu kitaifa na kimataifa.
  • Tanzania kuna lugha zaidi ya 100 lakini Kiswahili kinazungumzwa na asilimia 90 ya idadi ya watu na ni moja ya nguzo muhimu inayounganisha makabila 130.
  • Kutumika katika mikutano mikubwa ya kimataifa kama lugha ya majadiliano.
  • Lugha ya Kiswahili kutumika kwenye sanaa kama maigizo,miziki, ushairi na uandishi na kupelekea kazi hizo kufanya vizuri kitaifa na kimataifa.

Idadi ya wazungumzaji wa Kiswahili ulimwenguni.
Katika makala ya umoja wa mataifa(UN) mkurugenzi mkuu wa shirika la umoja wa mataifa la elimu,sayansi na utamaduni (UNESCO) Audrey azoulay amesema ikiwa na wazungumzaji kati ya milioni 120 hadi 150 lugha ya Kiswahili ni moja ya lugha zinazoshamiri kuvuka mipaka ya inamozungumzwa.

Inakadiriwa lugha ya Kiswahili ina idadi ya watu kati ya milioni 100 mpaka 200

Kuendeleza na kukuza lugha ya Kiswahili.
Ni jukumu la kila mtu kuendeleza na kukuza lugha ya Kiswahili. sisi kama watanzania tunapaswa kupenda na kujivunia lugha yetu kwa maana ni sehemu muhimu wa utambulisho wetu kimataifa

Je tunaweza kufanya nini ili kuendeleza na kukuza lugha ya Kiswahili?

  • Kuweka msisitizo juu ya matumizi ya lugha ya Kiswahili kwenye mitaala ya elimu na shughuli za kiserikali.
  • Uanzishwaji wa majukwaa ya kimtandao yatayowakutanisha wazungumzaji wa Kiswahili popote walipo duniani.
  • Kuzalisha wataalamu wa Kiswahili wenye uadilifu wa hali ya juu watakaoweza kufundisha Kiswahili kimataifa.
  • Kuyapa nguvu ya kifedha na rasilimali watu taasisi na mabaraza ya Kiswahili.
  • Kusisitiza matumizi ya Kiswahili fasaha kwenye vyombo vya habari kama magazeti, televisheni na radio.
  • Kutengeneza kazi za sanaa zenye ubora wa kimataifa lugha ya Kiswahili.
  • Kuongeza ushirikano na mataifa mengine katika nyaja ya biashara na ujirani mwema.


Hitimisho
  • Kiswahili ni Afrika mashariki
  • Kiswahili ni Tanzania
  • Kiswahili ni ustaarabu
  • Kiswahili ni amani
  • Kiswahili ni ushirikiano
  • Kiswahili ni harakati

Marejeo


PICHA. Kwa msaada wa Google.
 
Upvote 219
Taasisi ya Hakielimu imetoa matangazo kadhaa yenye kuonyesha udhaifu wa kutumia lugha ya Kiingereza kufundishia.

Ni kweli Kuna changamoto kutumia lugha ya Kiingereza kufundishia Kwa kuzingatia Walimu na wanafunzi wengi hawana msingi mzuri wa kufahamu lugha ya Kiingereza toka mwanzo.

Matokea inakuwa ngumu Kwa Walimu kuwasilisha maarifa Kwa ufasaha Kwa kutumia lugha ya Kiingereza pia wakati huo huo inakuwa ngumu Kwa mwanafunzi kupokea maarifa hayo.

Sasa ni wakati muafaka Kwa mamlaka na wizara husika kuja na maamuzi ni lugha gani itafaa kufundishia Kwa ngazi zote za elimu.
 
HISTORIA YA KISWAHILI.
Kuna nadharia mbalimbali kuhusiana na historia ya lugha ya Kiswahili. Wapo wanaodai chimbuko la Kiswahili kuwa ni pwani ya afrika mashariki, wataalamu kama Nae Freeman Granville (1959) kupitia kitabu chake kiitwacho (the medieval of Kiswahili language) anakuja na hoja kuwa Kilwa hata kabla ya karne ya 10 ilikuwa na umuhimu mkubwa kibiashara hivyo basi kulinganana na umuhimu huo wa biashara miongoni mwa wa wabantu wa kilwa na wageni(waarabu) ilipelekea kuibuka kwa lugha moja ambayo ndiyo inasadikika ni Kiswahili leo hii.

View attachment 2311226

Nadharia nyingine ni kama asili ya Kiswahili ni huko afrika magharibi(kamerun) sababu kuu ni kuwa huko ndiko chimbuko la wabantu kabla ya kutawanyika kutokana na sababu mbalimbali na wapo wataalamu wanasema kuwa chimbuko la Kiswahili ni jamhuri ya kidemokrasia ya congo.

Nadharia zote zaweza kuwa na mashiko kwa kuwa lugha ya Kiswahili ina maneno ya kibantu, kiarabu na baadhi ya maneno kutoka lugha tofauti kama kireno, kiingereza na kihindi kitu kilichochewa na muingiliano wa watu wa jamii tofauti kutokana na biashara pamoja na ujio wa wakoloni.

UMRI WA LUGHA YA KISWAHILI.
Lugha hii inakadirirwa kuwa na takribani na miaka 800 hadi 1000 toka kuanza kwake katika vituo vya biashara vya pwani ambako wafanyabiashara kutoka uarubuni, uajemi, na uhindi walipokutana na wenyeji wakazi wa Afrika.

Lugha ya Kiswahili iliweza kuzaliwa kutokana na wenyeji wabantu kupokea maneno mengi kutoka lugha tofauti hasa maneno ya kiarabu katika kuwasiliana.

View attachment 2311228
Kuenea kwa lugha ya kiswahili.
Kupitia biashara na muingiliano wa watu lugha ilianza kuenea sehemu mbalimbali za ulimwengu. wakati wa ukoloni lugha ya Kiswahili iliweza kusanifiwa na kamati ya kimaeneo ya lugha ya Kiswahili kwenye misingi wa lahaja ya unguja.

Kiswahili ni nini?
Kiswahili
ni lugha miongoni mwa lugha takribani elfu saba(7000) zinazozungumzwa ulimwenguni ikiwa inazungumzwa haswa katika eneo la Africa mashariki(Tanzania, kenya, Uganda, jamhuri ya kidemokrasia ya kongo na kaskazini mwa msumbiji).

Nchi zinazozungumza kiswahili.
Kiswaahili ni lugha rasmi ya taifa katika nchi ya Tanzania na kenya. Uganda pia iliwahi kuwa lugha ya taifa wakati wa utawala wa Iddi amin matumizi ya Kiswahili yalipingwa na waganda kutokana na historia ya utawala wa kijeshi.

Mashariki mwa kongo Kiswahili kimeenea sana na ni moja kati ya lugha nne za kitaifa katika jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Nchini Rwanda mnamo tarehe 8 februari 2017 bunge lilifanya Kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne baada ya Kinyarwanda, kifaransa na kiingereza.

View attachment 2311232

Mafanikio ya kiswahili.
Tarehe 23 mwezi novemba mwaka 2021 shirika la umoja wa mataifa la elimu,sayansi na utamaduni UNESCO lilitangaza rasmi tarehe 7 ya julai kila mwaka kuwa siku ya kiswahili duniani.

View attachment 2311233

Ni moja katika hatua muhimu za mafanikio ya Kiswahili katika anga za kimataifa. Katika azimio hilo lenye kurasa tatu, inaelezwa kuwa uamuzi huo unatokana na uamuzi wa kikao cha 212 cha bodi utendaji ya UNESCO kwa kutumia misingi mikuu kumi ambayo ni:

1. Kiswahili ni mawasiliano.

2. Wazungumzaji wa Kiswahili duniani.

3. Kiswahili afrika mashariki, kati na kusini.

4. Kiswahili na kufanikisha SDGs na AcFTA.

5. Kiswahili katika idhaa za umoja wa mataifa.

6. Umoja wa mataifa na matumizi ya lugha zaidi ya moja.

7. Kiswahili na utajiri katika utofauti wa kiisimu.

8. Kiswahili ni lugha rasmi ya SADC.

9. Kwa nini 7/7 na si tarehe nyingine. Tarehe 7/7/1954 nisiku ambayo chama cha TANGANYIKA AFRICAN NATIONAL UNION(TANU) chini ya hayati mwalimu julias kambarage nyerere,rais wa kwanza wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kilipitisha Kiswahili kama lugha ya kuunganisha harakati za ukombozi.

10. Maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani

Mafanikio mengine ni kama
  • Kuwepo kwa vyombo vya habari kama televisheni,redio na hata magazeti kuanzia ngazi ya kitaifa mpaka kimataifa vinavyotumia lugha ya Kiswahili kuwasilisha maudhui kwa hadhira.
  • Kuwa lugha ya afrika ambayo ni lugha rasmi katika serikali ya Tanzania na jumuiya ya afrika mashariki.
  • Kuanzishwa kwa kozi mbalimbali za Kiswahili katika ngazi ya shahada katika vyuo vya elimu ya juu kitaifa na kimataifa.
  • Tanzania kuna lugha zaidi ya 100 lakini Kiswahili kinazungumzwa na asilimia 90 ya idadi ya watu na ni moja ya nguzo muhimu inayounganisha makabila 130
  • Kutumika katika mikutano mikubwa ya kimataifa kama lugha ya majadiliano.
  • Lugha ya Kiswahili kutumika kwenye sanaa kama maigizo,miziki, ushairi na uandishi na kupelekea kazi hizo kufanya vizuri kitaifa na kimataifa.

Idadi ya wazungmzaji wa Kiswahili ulimwenguni.
Katika makala ya umoja wa mataifa(un) mkurugenzi mkuu wa shirika la umoja wa mataifa la elimu,sayansi na utamaduni (UNESCO) Audrey azoulay amesema ikiwa na wazungumzaji kati ya milioni 120 hadi 150 lugha ya Kiswahili ni moja ya lugha zinazoshamiri kuvuka mipaka ya inamozungumzwa.

Inakadiriwa lugha ya Kiswahili ina idadi ya watu kati ya milioni 100 mpaka 200

Kuendeleza na kukuza lugha ya Kiswahili.
Ni jukumu la kila mtu kuendeleza na kukuza lugha ya Kiswahili. sisi kama watanzania tunapaswa kupenda na kujivunia lugha yetu kwa maana ni sehemu muhimu wa utambulisho wetu kimataifa

Je tunaweza kufanya nini ili kuendeleza na kukuza lugha ya Kiswahili?

  • Kuweka msisitizo juu ya matumizi ya lugha ya Kiswahili kwenye mitaala ya elimu na shughuli za kiserikali.
  • Uanzishwaji wa majukwaa ya kimtandao yatayowakutanisha wazungumzaji wa Kiswahili popote walipo duniani
  • Kuzalisha wataalamu wa Kiswahili wenye uadilifu wa hali ya juu watakaoweza kufundisha Kiswahili kimataifa.
  • Kuyapa nguvu ya kifedha na rasilimali watu taasisi na mabaraza ya Kiswahili
  • Kusisitiza matumizi ya Kiswahili fasaha kwenye vyombo vya habari kama magazeti, televisheni na radio
  • Kutengeneza kazi za sanaa zenye ubora wa kimataifa lugha ya Kiswahili
  • Kuongeza ushirikano na mataifa mengine katika nyaja ya biashara na ujirani mwema.


Hitimisho
  • Kiswahili ni Afrika mashariki
  • Kiswahili ni Tanzania
  • Kiswahili ni ustaarabu
  • Kiswahili ni amani
  • Kiswahili ni ushirikiano
  • Kiswahili ni harakati

Marejeo

PICHA. GOOGLE.
,[emoji123][emoji123]
 
Mkuu nashukuru sana
Najaribu kujiuliza walitumia hesabu gani na kuja na idadi ya ya watu wanaozungumza kiswahili kuwa ni kati ya 100m had 120

Tz tupo 60m+ Kenya 45m+ Uganda tu assume 15 wanaoongea kiswahili + Congo 30m Rwanda 13m na nchi nyingine nyingi

Kwa ujumla ni karibia watu zaid ya 250 m wanaongea Kiswahili duniani
 
Najaribu kujiuliza walitumia hesabu gani na kuja na idadi ya ya watu wanaozungumza kiswahili kuwa ni kati ya 100m had 120

Tz tupo 60m+ Kenya 45m+ Uganda tu assume 15 wanaoongea kiswahili + Congo 30m Rwanda 13m na nchi nyingine nyingi

Kwa ujumla ni karibia watu zaid ya 250 m wanaongea Kiswahili duniani
Swali lako Lina mantiki. Kuhusu idadi inakadiliwa na sio idadi kamili.

Na Mimi nakuunga mkono kuwa idadi yaweza kuwa ni zaidi ya hapo lakini ni vyema kukumbuka Nchi kama Uganda, Rwanda na Congo idadi ya wazungumzaji wa kiswahili sio kubwa sana.

Na pia ndani ya nchi yetu Tanzania Kuna sehemu wanatumia lugha zao za asili na sio jambo la kushangaza kukutana na WaTanzania wasio jua kiswahili. Ndio maana Kuna baadhi ya shule za msingi zilizopo vijijini zinawahimiza wanafunzi kutumia lugha ya kiswahili wawapo mazingira ya shule
 
Ongera sana mkuu kwa chapisho lako zuri , kuhusu lugha ya kiswahili na dhima mbalimbali za kiswahili,bila kusahau history kidogo ya kiswahili, matumizi nk
 
Mr natumia chrome lakini link kwa ajili ya kupiga kura sioni kwenye uzi wako boss nahitaji kukusupport kwa andiko la kisomi
 
Back
Top Bottom