Kitabu Cha Historia ya Yanga na Harakati za Kudai Uhuru

Kitabu Cha Historia ya Yanga na Harakati za Kudai Uhuru

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Watu kadhaa wameniuliza ukweli kuwa kuundwa kwa Yanga mwaka wa 1936 ilikuwa mbinu ya kudai uhuru wa Tanganyika.

Haya nimeambiwa yameandikwa katika kitabu cha historia ya Yanga ambacho kimetolewa hivi majuzi.

Jibu langu kwao ni kuwa ushahidi wa historia ya kudai uhuru wa Tanganyika hauonyeshi hivyo.

Historia ya TANU inaanza na historia ya African Association mwaka wa 1924 katika mazungumzo ya Kleist Sykes na Dr. Kwegyir Aggrey kutoka Achimota College, Ghana.

Dr. Aggrey alimshauri Kleist Sykes Waafrika wa Tanganyika waunde chama chao kama walivyofanya Wazungu (European Association) na Waasia (Indian Association).

Mwaka wa 1929 African Association ikaundwa waasisi wakiwa Cecil Matola (President), Kleist Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Ali Said Mpima, Suleiman Majisu, Humbi Ziota, Raikes Kusi na Watson Watts.

Mwaka wa 1948 African Association ikabadili jina lake ikawa Tanganyika African Association (TAA) Thomas Saudtz Plantan akiwa President na Clement Mohamed Mtamila Secretary.

Mwaka wa 1950 yakafanyika mapinduzi yaliyowatoa viongozi hawa madarakani kwa nguvu.

Serikali ikaamrisha TAA ifanye uchaguzi wa viongozi.

Uchaguzi ukawaingiza madarakani Dr. Vedasto Kyaruzi (President), Abdul Sykes (Secretary).

Uongozi huu ukaunda TAA Political Subcommittee wajumbe wakiwa: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.

Kamati hii kwa msaada wa Mwanasheria Earle Seaton ndiyo iliyofungua mawasiliano na UNO kuhusu Tanganyika kama nchi inayotawaliwa chini ya udhamini wa Uingereza.

Kamati hii kupitia juhudi za Hamza Mwapachu na Abdul Sykes ndiyo iliyomuingiza Julius Nyerere katika uongozi wa TAA mwaka wa 1953 na mwaka wa 1954 TANU ikaundwa Nyerere akiwa President.

Kwa kifupi hivi ndivyo TANU ilivyoundwa na hii ndiyo historia yake.

Kuwa Yanga iliasisiwa mwaka wa 1936 kudai uhuru hili halina ushahidi wowote.

Atakae kujua zaidi kuhusu historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika atazame video hiyo hapo chini:


View: https://youtu.be/b0wV_rF1W20?si=c_f8lKCVXRqd_GGE
 
Mzee leo umetupiga changa la macho, klabu ya Yanga ilitumika kama Saigon Club ilivyo kuwa eneo la kupangia mikakati ya kudai uhuru kwa cover ya michezo.

Huo ndio ukweli waulize wazee wako wakusimulie.
 
Watu kadhaa wameniuliza ukweli kuwa kuundwa kwa Yanga mwaka wa 1936 ilikuwa mbinu ya kudai uhuru wa Tanganyika.

Haya nimeambiwa yameandikwa katika kitabu cha historia ya Yanga ambacho kimetolewa hivi majuzi.

Jibu langu kwao ni kuwa ushahidi wa historia ya kudai uhuru wa Tanganyika hauonyeshi hivyo.

Historia ya TANU inaanza na historia ya African Association mwaka wa 1924 katika mazungumzo ya Kleist Sykes na Dr. Kwegyir Aggrey kutoka Achimota College, Ghana.

Dr. Aggrey alimshauri Kleist Sykes Waafrika wa Tanganyika waunde chama chao kama walivyofanya Wazungu (European Association) na Waasia (Indian Association).

Mwaka wa 1929 African Association ikaundwa waasisi wakiwa Cecil Matola (President), Kleist Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Ali Said Mpima, Suleiman Majisu, Humbi Ziota, Raikes Kusi na Watson Watts.

Mwaka wa 1948 African Association ikabadili jina lake ikawa Tanganyika African Association (TAA) Thomas Saudtz Plantan akiwa President na Clement Mohamed Mtamila Secretary.

Mwaka wa 1950 yakafanyika mapinduzi yaliyowatoa viongozi hawa madarakani kwa nguvu.

Serikali ikaamrisha TAA ifanye uchaguzi wa viongozi.

Uchaguzi ukawaingiza madarakani Dr. Vedasto Kyaruzi (President), Abdul Sykes (Secretary).

Uongozi huu ukaunda TAA Political Subcommittee wajumbe wakiwa: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.

Kamati hii kwa msaada wa Mwanasheria Earle Seaton ndiyo iliyofungua mawasiliano na UNO kuhusu Tanganyika kama nchi inayotawaliwa chini ya udhamini wa Uingereza.

Kamati hii kupitia juhudi za Hamza Mwapachu na Abdul Sykes ndiyo iliyomuingiza Julius Nyerere katika uongozi wa TAA mwaka wa 1953 na mwaka wa 1954 TANU ikaundwa Nyerere akiwa President.

Kwa kifupi hivi ndivyo TANU ilivyoundwa na hii ndiyo historia yake.

Kuwa Yanga iliasisiwa mwaka wa 1936 kudai uhuru hili halina ushahidi wowote.

Atakae kujua zaidi kuhusu historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika atazame video hiyo hapo chini:


View: https://youtu.be/b0wV_rF1W20?si=c_f8lKCVXRqd_GGE

Kwamba Yanga ina umri sawa na Simba 1936?
Pili, kila kitu kinapoundwa kina mwanzo wake. Kuunda kitu ni mchakato. Mzee nakufahamu kuwa wewe ni Kolo. Usipotoshe historia ya Yanga.
 
Mzee leo umetupiga changa la macho, klabu ya Yanga ilitumika kama Saigon Club ilivyo kuwa eneo la kupangia mikakati ya kudai uhuru kwa cover ya michezo.

Huo ndio ukweli waulize wazee wako wakusimulie.
Dr...
Mimi nimeulizwa na watu kuhusu historia ya Yanga na harakati za kudai uhuru.

Wameniuliza kwa kuwa wainajua nafasi yangu katika ujuzi wa historia ya TANU.

Hilo ndilo jibu langu.

Ikiwa unaona kuwa hayo niliyoandika si kweli hapana shida.
 
Dr...
Mimi nimeulizwa na watu kuhusu historia ya Yanga na harakati za kudai uhuru.

Wameniuliza kwa kuwa wainajua nafasi yangu katika ujuzi wa historia ya TANU.

Hilo ndilo jibu langu.

Ikiwa unaona kuwa hayo niliyoandika si kweli hapana shida.
Jibu murua kabisa aisee
 
Uhuru sio historia ya kukaririshwa

Uhuru sio jambo la Siku moja, bali uhuru ulikuwa ni mchakato wa mda mrefu.
Ulianzia mbali sana mchakato huu tokea kwa akina mkwawa, vita vya majimaji, machifu waliweka jifihada zao, mpaka kufikia kwenye vyama vya TAA nk.

Haikuwa jambo la siku moja, na wala halikuwa jambo la mtu mmoja au kikundi fulani pekee.

Hivyo kutambua mchango wa Club ya Yanga katika uhuru wa Tanganyika ni jambo la kheri

Yanga waliupiga mwingi
 
Uhuru sio historia ya kukaririshwa

Uhuru sio jambo la Siku moja, bali uhuru ulikuwa ni mchakato wa mda mrefu.
Ulianzia mbali sana mchakato huu tokea kwa akina mkwawa, vita vya majimaji, machifu waliweka jifihada zao, mpaka kufikia kwenye vyama vya TAA nk.

Haikuwa jambo la siku moja, na wala halikuwa jambo la mtu mmoja au kikundi fulani pekee.

Hivyo kutambua mchango wa Club ya Yanga katika uhuru wa Tanganyika ni jambo la kheri

Yanga waliupiga mwingi
Gill...
Yanga wala Sunderland hawakuhusika katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Katika historia ya uhuru wa Tanganyika ni club moja tu Young New Strong Team ya Tabora ndiyo iliyoshirikisha club yao na viongozi wao kuunda tawi la TANU.

Historia hii nimeieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
 
Back
Top Bottom