Kitabu kipya: Tanzania na propaganda za udini na prof. Ibrahim Noor


Kwanza kabisa mimi si Mwarabu. Bali nnakijuwa Kiarabu - Kumbuka hilo. Halafu kama umenisoma vizuri post zangu nimeelezea juu huko ni nini maana ya Arab au Waarabu. Rudi, unaonesha amma husomi tunachojadili amma una kumbukumbu finyu.

Halafu nnafurahi sana kuwa unajuwa maana ya Abantu kuwa ni watu, Wallahi nimefurahi sana kwani inaonesha labda unajuwa kweli maana ya Bantu ila inakuwa vigumu sana kwako kukiri na au kuielezea au hauijuwi na unakisia tu. Kwani umeilezea nusu maana tu tena umeitoa nilivyouliza mimi "Bantu" ukaiongozea "A"bantu". Hiyo inaitwa "manipulation".

Jee hukusoma juu nimekuwekea kipande kutoka Makerere University wanavyofundisha chuoni hapo maana ya Bantu? naomba urudi ukasome ujuwe maana sahihi ya Bantu, unaweza kuwa ni Mbantu lakini pengine maana ya Bantu huijuwi.
 
Nimekwambia siendi kusoma site kitu nachokijua, wewe unayesoma sites iseme, maana mimi Mbantu unaponipa maana nyingine inanibidi nitafute ni lugha gani imetumika. Faiza, ABANTU ni kibantu chenyewe hakuna manipulation katika lugha yangu nakufundisha lugha yangu badala ya hawa wavumbuzi kina Christopher Columbus alokwenda visiwa vya West Indies akukata kuna Wahindi kule akadhani amevumbua India kumbe yupo dunia nyingine kabisa.

Binadamu walihama hama miaka yote na majuzi tu wazungu wamekuja kubali kwamba hata hiyo North Amerika, Wachina na Wahindi walifika na kuishi huko kabla yao, lakini bado sio wenyeji na walikuja fuata nini ama walifanya biashara na watu gani wanayumba kutafuta mifupa na mafuvu.

Come on now Faiza, mimi najua wewe sio Mwarabu ila unanichosha sana kujisikia mwarabu sana kwa sababu unaongea lugha au jamaa amal? halafu unasema Waarabu ni watu wanaongea Kiarabu ilihali wapo waarabu wasiongea Kiarabu. Kisha basi Uarabu sio Asili ni kabila tu, Semitic ndio asili yao na hapa kuna makabila mengi sana na lugha nyingi kama unavyosema Wabantu.

Wewe umetumia Sandawe na Baruge kuwa ndio wenye asili haswa ya Tanganyika na ni makabila tu mawili sijui matatu kwa Tanganyika nzima, Nilipokuuliza asili yao ukarudi na Cushitic na Semitic kuonyesha hata wao sio wenyeji Tanganyika walitokea Kusini na Kaskazini, sasa ikiwa hata hawa sio, wenyeji haswa ni kina nani ikiwa hata hawa inaonyesha walihamia Tanganyika tena umetumia kabila mbili na sio Asili ya watu hawa.

Na hakuna mahala popote panasema Cushities na Semitics ndio wenye Asili ya kwanza Tanganyika ila unatumia mila na tamaduni za makabila kama Sandawe ambao ni wawindaji lazima watahamia sehemu za wanyama kuwinda na kuishi na hao Baruge ni wafugaji lazima watatafuta sehemu za malisho kwa mifugo yao, hivyo kufika kwao Tanganyika hakuwapi miliki ya ardhi hiyo na ni makabila mawili tu uloyataja ina maana sehemu nyingine hapakuwa na watu kabisaa!
 

Naona darsa limekuingia na sasa unaanza kukiri uliyoyapata kutoka kwangu ki aina yako.

Huwezi kwenda kusoma link lakini wewe unahaki ya kuniwekea link nikasome maana ya Zenjbar? what a double standard.

Bantu hujaelezea maana yake kabisa umeelezea "Abantu" tena nusu nusu, unaogopa nini lama unaelewa? Isitoshe, historia niliyokuwekea kuhusu Bantu inatoka Makerere University Uganda, sasa hao akina Columbus na Makerere wapi na wapi?

Kwa maana hiyo hiyo, kuna mahala panasema Sandawe na makabila mengine kadhaa yanayopatikana Tanganyika ni Cushites na wapo zamani hapa Tanganyika kuliko Wabantu. Sasa mgeni aliyewakuta wenyeji anakuwa na asili zaidi ya aliowakuta? Si vituko hivyo?

Au Historia yako aliyekufundisha hakukwambia Wabantu wamefika lini Afrika ya Mashariki? na hakukwambia Cushites wamefika lini Afrika ya Mashariki? Alidanganya kuwa Wabantu Tanganyika hawakuja?

Unanisikitisha sana kwa ufinyu wa ufahamu na uelewa unaouonesha.
 
Unajipiga chenga mwenyewe nimeshakwambia BANTU maana yake na kukupa haswa inavyotamkwa sio kiuandishi. Wewe umakazania ulichosoma Makerere wakati mimi lugha yangu na Mbatu haswaa. Cushites wapo Manyara na Arusha, Tanganiyka sio Manyara tu. Historia uloitoa imeonyesha hata hawa ni wahamiaji iweje useme Wabantu walihamia baada wakati Wasandawe hawakuishi Dar, Tabora, Mwanza, wala Morogoro?

Lets cut the chase, nikuulize kuhusu Zanzibar. 1. Kati ya Pashtons, Waarabu na Persian kina nani walokuwepo mwanzo ama wenye asili ya Zanzibar kuliko wengine., 2. na walipokuwa wakifanya biashara ya viungo hawapakuwepo na wakulima wa makabila kama Wahadimu na Matumbatu? 3. na kwa nini Unafikiri jina Zanzibar ilitokana na kiarabu na sio Ki Persian?
 


Aaaha, nnafurahi kuwa umekiri kuwa Ubantu ni lugha.

Kuhusu hilo la Sandawe na au Manyara kuwa ni Tanganyika pekee, hizo ni porojo zako na hakuna mahala popote mimi nilipoandika hivyo, nnaku challenge onesha na usitake kutia maneno yako kinywani mwangu. Tafadhali.

Kuhusu hili la Waarabu na akina nani sijuwi ni nani kaja kwanza, ni very simple, kama umenisoma post zangu utaelewa kuwa nimesema mara chungu nzima Mwarabu hakuja Afrika na nimekuwekea ushahidi chungu nzima ku prove hilo na Zanzibar ni kisiwa kilichopo Afrika. Kwa hiyo swali lako hili ni irrelevant.

Zingine unaleta ni porojo tu na hauna jipya.

Tana nnarudia, ongea lakini si usitake kutia maneno yako vinywani mwa watu, juu huko umezuwa kuwa Alama Mohamed Said vitabu vyake vimefungiwa Tanzania, tukakushushuwa, ukazuwa tena kuwa vina udini na vinamshusha Nyerere, tukakwambia leta ushahidi umeshindwa, sasa unakuja na uongo wa kuzua mambo ambayo sikuyasema. Au Kingereza kinakupiga chenga? Licha ya kukupa darsa kuhusu Waarabu, kuhusu Wabantu, kuhusu Sandawe na wengineo, kuhusu Zenjbar na maana yake lakini bado unakuja na uongo? Unanshagaza!

Kuwa mkweli nafsi yako iwe katika amani. Huna sababu ya kuzuwa, huu ni mjadala tu na uansomwa na wengi na kuzuwa kwako kunakushushia hadi yako, huna sababu ya kujidanganya nafsi yako kwa kupindua na kupindisha maneno.

Mwarabu hakuja Afrika.
 
Faiza mbona challenge zako za kitoto hivi. K wapi nimeandika kukushutumu kuwa Wasandawe waliishi Manyara? au unazungumzia WaBaruge. Nilichokuuliza kipo wazi Kabisa Tanganyika kubwa ina maana haya makabila mawili tu ndio yalikaa Tanganyika yote? na wamegundua hivyo kwa kupata mifupa na mafuvu ya watu waloishi Tanganyika au?

Usikwepe maswali sii wewe ulosema unajua sana nimekuuliza na kwa ujuzi wako nambie majibu maana umesoma Makerere. Unakimbia nini sasa, hivyo unapoulizwa swali bila shaka utakuwa na jibu. Nipe majibu ya hayo maswali matatu tu tumalize Ubishi na nakuhakikishia ubishi utakwisha tutaijua kweli..Nawe nakuomba jibu maswali kama ulivyokuwa uking'ang'aniza ujibiwe kwanza.
 

Hujanisoma juu huko, si makabila mawili tu, wewe ndiyo uliuliza hayo mawili tu, umesahau? katika makabila uliyoyaona na kuyakuta ukachaguwa na kuuliza kuhusu hayo mawili tu, mbona una kumbukumbu finyu hivi? nikuwekee post ili nikukumbushe?

Na ungenisoma kwa utuvu juu huko, ungeona nimekuonesha kuwa utaalaam wa sasa wa DNA pia umetumikan na wamechukuliwa sampling ya DNA ya watu walio hai, halafu unauliza kuhusu mifupa! Rudi kasome.

Sasa ni nani anaebishana kitoto? mimi au wewe vitu unavisoma halafu unauliza tena hivyo hivyo, huo ndiyo utoto.

Hakuna swali lako nililolikimbia hata moja na nnaona unajichanganya tu, mfano unaniuliza Waarabu wamekuja lini, wakati mimi nimesema hawakuja na hilo swali ni irrelevant kwangu, kwani mimi nnasema hawakuja. Umesahau kuwa wewe ndiyo uliyesema wamekuja karne ya 14 na 15 ? Nikakwambia hapana na nikakuonesha kuwa hiyo ni miaka aliyokuja Vasco Da Gama na si Waarabu, ukarudi umerekebisha kuwa ni katne ya 4 au 5 na ukasema eti ulikosea ku type tu. Ukaja na ujio wa "wafuasi" wa mtume. Nikakuuliza, jee kabla ya hao wafuasi kulikuwa hakuna misafara ya Hejaz na Najid? ukawa hujuwi Hejaz na Najd ni nini, nikakupa darsa ukapaelewa, ukaja na kujidai kuwa "hapo ni Mesopotamia utakubali utakataa?", nikakwambia hapana si kweli, hapo si Mesopotamia, nikakupa darsa la wapi Mesipotamia ukaja nakujidai eti "google" na kujichekesha kijinga. Nikakupa darsa lingine.

Yote hayo umesahau? halafu unanambia mimi eti "challenge" zangu "za kitoto", wakati hapa kwako mimi siioni "challenge" yoyote zaidi ya kukupa darsa, na "challenge" kubwa iliopo ni ufahamu wako tu, you are too slow to learn, lakini usijali, kwangu utasoma tu.
 

some time unajichanganya maana ukisema uarabu ni Lugha naomba nijibu maswali haya machache Je Mtoto wa Mzaramo(mweusi) akizaliwa Oman na Lugha Mama yake ikiwa ni kiarabu Je huyo Mtoto automatic anakuwa Mwarabu? Je watu wa Irani ni waarabu? watu wa Uturuki ni waarabu?
 
Mwandishi wa kitabu hiki bwana Ibrahim Noor Sharrif na wengine wengi wenye mwonekano (kwa rangi ya ngozi) wapo kwenye IDENTITY CRISIS na ndiyo unayowafanya watunge stories za ajabu ajabu.
Hawa ni watu ambao walipokuwa wanakua, walijiona ni binadamu bora kwa kujiita WAARABU kuliko kujiita waafrika weusi.
Walipojaribu kwenda ulaya na Marekani, wakastukia wanaitwa BLACKS.
Walipojaribu kwenda nchi za kiarabu kama SAUDIA na YEMENI wakastukia wanaitwa BLACKS.
Sasa wameamua kujiita WAARABU wa AFRICA wanatunga stories eti walikuwepo Africa kabla ya wabantu...
Ni kutaka kujiridhisha tu psychologically kwamba status yao ya uarabu iko pale pale, na wana nyumbani kwao ambako ni Africa, ambako walikuwepo kabla ya waafrika weusi... Ni tatizo tu la identity crisis
Hakuna haja ya kuwabishia. Waache waendelee kujiridhisha...
By the way, mwarabu gani ana pua kama hiyo inayoonekana kwenye picha ya kitabu?? Mwarabu koko?
 
Nanren,
Umetoa hoja zako na In Sha Allah watu watasoma ila hilo tusi...
Neno la mwisho katika bandiko lako.
 

Hahahaha si ubora kuwa Mwaarabu hata waarabu wenyewe wanabaguana kama ilivyo kwa Waafrika, Uislam unatufundisha mbora kati yetu ni mwenye kumcha Mwenyeezi Mungu, na si rangi, kabila, lugha wala taifa.

Jee, unajuwa maana ya neno ustaarabu?
 

Hebu jisomee kidogo kuhusu Waarabu labda utawaelewa:

Arabs (Arabic: عرب‎, ʿarab) are a major panethnic group.[SUP][14][/SUP] They primarily inhabit Western Asia, North Africa, parts of the Horn of Africa, and other areas in the Arab world. Arabic-speaking populations in general are a highly heterogeneous collection of peoples, with different ancestral origins and identities. The ties that bind the Arab peoples are a veneer of shared heritage by virtue of common linguistic, cultural, and political traditions. As such, Arab identity is based on one or more of genealogical, linguistic or cultural grounds,[SUP][15][/SUP] although with competing identities often taking a more prominent role,[SUP][16][/SUP] based on considerations including regional, national, clan, kin, sect, and tribe affiliations and relationships. If the Arab panethnicity is regarded as a single population, then it constitutes one of the world's largest groups after Han Chinese.

The Arabian Peninsula itself was not entirely originally Arab. Arabization occurred in some parts of the Arabian Peninsula. For example, the language shift to Arabic displaced the indigenous South Semitic Old South Arabian languages of modern-day Yemen and southern Oman. These were the languages spoken in the civilisations of Sheba, Ubar, Magan, Dilmun, and Meluhha-which were spread via migrants from the Arabian peninsula, together with written script, in the 8th and 7th centuries BC to the Horn of Africa (Ethiopia, Eritrea, Djibouti, and Somalia).


Chanzo: Arabs - Wikipedia, the free encyclopedia
 
Nanren

Nimeuliza, umekimbia hujanijibu, nata jibu au majibu yako kwa hili:

Jee, unajuwa maana ya neno ustaarabu?
 
Last edited by a moderator:
Ukikiangalia saaaaana maudhui yake unatambukuwa kitabu chenyewe nacho ni propaganda za kidini zaidi sidhan kama kitaleta jipya..
Nikushukuru Profesa Ibrahim Noor Shariff kwa utafiti wa kina hadi kukiandika na kukitoa kitabu hiki. Wanaobeza, ni mazao ya Elimu ya historia ya kukaririshwa na si wanahistoria wa kufanya utafiti.

Nilipata kumsoma Ibn Batuta na safari zake ktk Karne ya 14 na kwamba aliongea kiarabu na watu alowakuta Pwani ya Afrika Mashariki. Na pia ameeleza Ibn Batuta kuwa, alipofika Sofala, Kilwa na Malindi alikuta watu wakiwa na nyumba zenye sura kama nyumba za Arabuni.

Tusome historia.. Tusikaririshwe
 


Weye kweli umeghafilika. Hata tukisema kwamba warabu wamekuja Zanzibar mwaka 1832, Sheria ya Zanzibar ambayo ilitungwa na hao unaowaita wabantu ambao ndio eti wanasemwa kuwa ndio waliopindua basi inatamka kuwa; Mtu yeyote aliekuwepo Zanzibar siku ya mapinduzi ya mwaka 1964 basi ni Raia wa Zanzibar. Kwa maana hiyo ni kwamba hata hao unaowaita warabu unaosema walikuja mwaka 1832 kwa mujibu wa sheria nao ni raia halali wa Zanzibar na Tanzania. Sasa sijuwi inakuwaje kwamba raia wa wanapochaguwa eti hawapewi. Huo ni Ukoloni na tumeshautambua na ipo siku kwa uwezo wa Allah mkoloni mweusi ataondoka. Chuki zako za kidini na ubaguzi wa kikabila na rangi umekufanya uwe kipofu. Kwamba wanaopigia kura wapinzani zanzibar wote ni warabu? sasa kwa nini mumekubali mfumo wa vyama vingi? Huo ndio unafiki mkubwa kabisa.
 

Kwenye red; hapo ndipo nilipojuwa kwamba weye huko fair, ni mtu mwenye chuki za kidini tu na wala si mpingaji wa ukoloni. Hebu tujiulize vita ya mao mao kenya ilipiganwa dhidi ya mkoloni wa kingereza kwa malengo gani?, Rais mugabe amewanyan'ganya wazungu ardhi zimbabwe, hivi hao wazungu wa zimbabwe waliipataje hiyo ardhi? Makaburu wa africa ya kusini waliipataje ardhi? Kitabu kimekuja mtu amefanya utafiti, wewe badala ya kufanya na weye utafiti wako ukaja kukipinga hiki kitabu, unabaki kutoa povu na kudhihirisha chuki zako za kidini na akina lukuvi.
 

Watumwa walipelekwa arabuni kufanya kazi gani? mimi najuwa watumwa walipelekwa latin amerika kufanya kazi ktk mashamba ya wakoloni. Na utumwa ulipigwa marufuku baada ya wakoloni kuvumbua viwanda ikawa watumwa hawahitajiki tena sasa huko amerika kutokana na ukweli kwamba kazi walizo wakifanya watumwa nyingi zao zilikuwa zinafanywa na mashine tena kwa ufanisi na kwa gharama nafuu. Arabuni huwezi kukuta watu wengi weusi kwa sababu watumwa walikuwa hawapelekwi arabuni mkuu. Historia ya shule ni urongo mtupu, soma historia nyingine kisha linganisha acha ushabiki.
 

So you are going to read the book not to get understanding but to reply? That is reactive behavior.

Halafu kama umeisoma Quran na kisha umeamua ku i dismiss, hakika upo ktk hasara.
 
Kaweka nukuu flani hapo kwa juu anasema watu "watu wema ni...."ili wewe ambaye hata kwa hata hiyo nukuu hujaelewa naweza sema kuna bias sehemu flani acha akili yako itambae itaujuwa ukweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…