Kitendawili cha wasiojulikana hatimaye kimeteguliwa na Spika Tulia?

Kitendawili cha wasiojulikana hatimaye kimeteguliwa na Spika Tulia?

Mkuu Nguruvi3 mimi naogopa. Na mimi nakumbuka kipindi ambacho kiongozi moja wa UVCCM alitamka wazi kabisa kuwa wanaompinga Rais Magufuli wauawe. CCM kama chama kilikaa kimya, hakimuonya wala hakimkemea.

Matokeo yake Spika wa Bunge anawataka vijana hao hao wa CCM wamshughulikie yeyote yule watakayemkuta akiwasema vibaya viongozi wa CCM na serikali. Na mimi nasubiri tamko la CCM, chama tawala, je watakaa kimya?

Wengi walitekwa, wengi waliteswa na wengi walipotezwa, kisa? Kupinga au kukosoa kauli tata zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa CCM na serikali. Yupo na mwingine humu humu Jamii Forum kashauri wanaoikosoa hii serikali wachukuliwe hatua.

Pamoja na hayo leo kama wasemavyo wahenga a light appeared at the end of a long dark channel. Spika tulia kwa kujisahau au kulewa madaraka kawataka vijana hao kuwanyoosha eti wanaowasema vibaya viongozi ikiwa ni pamoja na yeye kama awali.

Kumbe walioitwa wasiojulikana yawezekana walikuwa wakitekeleza miongozo waliyokuwa wakipewa na chama chao...kuwanyoosha wapinzani wao. Wapo walionyoshwa wakapona na wapo walionyoshwa wasiamke tena , Munge walaze pahala pema peponi!
 
Tulia ni mkuu wa mhimili unaotunga sheria. Akiwa Spika anafahamu nchi inaendeshwa kwa sheria
Kitendo cha kutoka na kumasisha vurugu katika jamii ni cha kulaani na kulaaniwa na yoyote

Leo hatujui vijana aliowaelekeza 'wanyooke' na wenzao watachukua hatua gani.

Tunakumbu kumbu ya UVCCM wakisema wanaopinga JPM wauawe.
Spika ni mjumbe wa kamati kuu ya CCM katoa maagizo wasiokubaliana na wenzao wa CCM '' Nyooka naye'.

Hatujui kunyooka ni kwa namna gani, iwe kwa risasi kama Tundu Lissu au kwa mapanga kama Alphonce Mawazo au kupopotezwa kama Kanguye na Ben Saanane

Hatujui vijana wasio wa CCM wata react vipi pindi watakapokabiliwa na wenzao wa CCM wakati wa 'kunyooshwa'

Kwa kiongozi wa Bunge (Spika), Mbunge na Mjumbe wa kamati kuu ya CCM kuhamasisha vijana ' wanyooshane' ni kulitakia mabaya Taifa hili. Mauaji ya kimbari huanza na hamasa kama hizi zikiwahusisha vijana

Tulia Ackson amepoteza sifa ya kuwa kiongozi kwa kuhamasisha vurugu zinazoweza kupekelea mauaji na uvunjifu wa amani nchini.

Vurugu zozote zitakazotokea nchini kati ya vijana wa CCM na wasio , Spika Tulia atakuwa ima 'mtuhumiwa au Shahidi' hili hatalikwepa

CCM watoke watueleze ikiwa Tulia alikuwa anatumia ILANI ya chama chao ili kumsafisha
Ikiwa CCM watakaa kimya basi hili nalo ni lao

Katika mazingira ya kawaida, Tulia alitakiwa ajiuzulu Uspika au alazimishwe kujiuzulu kutokana na kauli inayohatarisha amani na usalama wa Taifa.

Mag3 Pascal Mayalla JokaKuu Kalamu Tindo

Na Tulia anahamasisha hayo maana anajua hawako madarakani kihalali, hivyo kusemwa vibaya ni lazima. Sasa anatengeneza kinga ya wao kutokusemwa vibaya kwani anajua vijana wa CCM wanaosaka vyeo watafanya lolote ili waonekane na kupatiwa vyeo. Hii jeuri ya madaraka huwa inaondoka kunapotokea machafuko, lakini kwa lugha za kubembelezana ndio uhuni kama huu utaendelea kushamiri.
 
"Nyooka nae"

Lakini hiyo tungo ni tata, hata akipelekwa mahakamani sidhani kama atafungwa, na inawezekana alijua ndio maana akaitumia.

Inaonekana wengi wanaitafsiri kwa namna wanavyoona/taka wao, hasa kutokana na mazingira ya kisiasa yaliyopo kati ya CCM na wapinzani.

Lakini hiyo pekee kwangu naona haitoshi kumtia hatiani Tulia pale atakapotakiwa kujitetea.

Anaweza kusema "nyooka nae" alimaanisha kuwaambia vijana wa CCM wajibu hoja kwa hoja, sasa nani ataweza ku prove vinginevyo?

Kwa taarifa yako hiyo nyooka naye ni kuwafanyia ukatili wanaowasema. Na hata angesema wawaue wanaowasema vibaya, kwa mahakama hizi asingefanywa lolote. Lakini ingetokea mpinzani kasema hivyo, mahakama ingemtia hatiani mara moja! Usitegemee haki yoyote kwenye mahakama hizi ambazo ni sehemu ya huu utawala wa double standard mbele ya sheria.
 
Na Tulia anahamasisha hayo maana anajua hawako madarakani kihalali, hivyo kusemwa vibaya ni lazima. Sasa anatengeneza kinga ya wao kutokusemwa vibaya kwani anajua vijana wa CCM wanaosaka vyeo watafanya lolote ili waonekane na kupatiwa vyeo. Hii jeuri ya madaraka huwa inaondoka kunapotokea machafuko, lakini kwa lugha za kubembelezana ndio uhuni kama huu utaendelea kushamiri.
Wasi wasi wangu ni kuwa Vijana wa CCM wanaochochewa 'wanyooshe wenzao' wasio wa CCM kuna uwezekano yakatokea mapigano ya vijana yatakayoenea nchi nzima.

Polisi wapo wakimya lakini tutawakumbusha wakati huo yakitokea
Msajili wa vyama yupo kimya ingalikuwa wamesema hayo wapinzani leo ungemuona akihemu kila kona
Viongozi wa dini wamekaa kimya, wanasubiri balaa litokee waende uwanja wa Taifa kuombea Taifa amani

Hii kauli ni hatari sana kwasababu vijana wa CCM wamepewa kibali cha kunyoosha wenzao tena kauli hiyo ikikaliwa kimya na Polisi. Vijana wasio wa CCM tayari wanajua kuna 'amri' ya wao kushambuliwa na hivyo tayari wapo sensitive.

Tulia Ackson hataweza kukwepa lawama kutokana na madhara ya kauli yake
CCM haitakwepwa lawama kutokana na kukalia kimya kauli ya kuhamasisha vurugu pengine na mauaji

Hatujui kunyoosha ni kupigwa au kuuawa au kupotezwa!
 
Wasi wasi wangu ni kuwa Vijana wa CCM wanaochochewa 'wanyooshe wenzao' wasio wa CCM kuna uwezekano yakatokea mapigano ya vijana yatakayoenea nchi nzima.

Polisi wapo wakimya lakini tutawakumbusha wakati huo yakitokea
Msajili wa vyama yupo kimya ingalikuwa wamesema hayo wapinzani leo ungemuona akihemu kila kona
Viongozi wa dini wamekaa kimya, wanasubiri balaa litokee waende uwanja wa Taifa kuombea Taifa amani

Hii kauli ni hatari sana kwasababu vijana wa CCM wamepewa kibali cha kunyoosha wenzao tena kauli hiyo ikikaliwa kimya na Polisi. Vijana wasio wa CCM tayari wanajua kuna 'amri' ya wao kushambuliwa na hivyo tayari wapo sensitive.

Tulia Ackson hataweza kukwepa lawama kutokana na madhara ya kauli yake
CCM haitakwepwa lawama kutokana na kukalia kimya kauli ya kuhamasisha vurugu pengine na mauaji

Hatujui kunyoosha ni kupigwa au kuuawa au kupotezwa!

Kwenye hili tayari vijana wa CCM wana Backup ya vyombo vya dola hasa hasa polisi. Tumekuwa tukiona vijana wa CCM wakawawafanyia ukatili wa wazi wapinzani, huku polisi wakiwapa cover vijana wa CCM. Na baada ya unyama huo, vijana wa upinzani wamekuwa wakigeuziwa kibao kuwa wao ndio wakosaji. Hali hii imekuwa ya kawaida ndio maana unaona vijana wengi wa upinzani wakiwa magereza kwa kesi za kubambikiwa. Iwapo hakutatokea machafuko ya kutosha, wapinzani wataendelea kuwa wahanga wa hizi lugha za kina Tulia.
 
..kwenye demokrasia zilizokomaa Spika Tulia Ackson angelazimishwa kujiuzulu kutokana na kauli yake inayohamasisha kuvunja sheria / ukatili.
Thubutu! Kama Madelu, pamoja na kusimamia wizi na kauli chafu, hakujiuzulu wala kuwajibishwa, itakuwa huyu Tulia! Naona huwajui CCM, pamoja na jeuri na dharau yao kwa wananchi, hajiuzulu mtu. Kama nafasi ya juu zaidi ingekuwepo, si ajabu angepandishwa cheo!
 
"Nyooka nae"

Lakini hiyo tungo ni tata, hata akipelekwa mahakamani sidhani kama atafungwa, na inawezekana alijua ndio maana akaitumia.

Inaonekana wengi wanaitafsiri kwa namna wanavyoona/taka wao, hasa kutokana na mazingira ya kisiasa yaliyopo kati ya CCM na wapinzani.

Lakini hiyo pekee kwangu naona haitoshi kumtia hatiani Tulia pale atakapotakiwa kujitetea.

Anaweza kusema "nyooka nae" alimaanisha kuwaambia vijana wa CCM wajibu hoja kwa hoja, sasa nani ataweza ku prove vinginevyo?
Na hao vijana watakuwa wameelewa hivyo kama ulivyoeleza? "Nyooka naye", vijana wenye vuguvugu la damu watafsiri ni "kujibu hoja", watu wasiojuwa kujenga hoja?
 
Thubutu! Kama Madelu, pamoja na kusimamia wizi na kauli chafu, hakujiuzulu wala kuwajibishwa, itakuwa huyu Tulia! Naona huwajui CCM, pamoja na jeuri na dharau yao kwa wananchi, hajiuzulu mtu. Kama nafasi ya juu zaidi ingekuwepo, si ajabu angepandishwa cheo!
Huyu Madelu mwenyewe anayo historia ndefu ya mambo ya aina hiyo..

Ile mikutano ya CHADEMA kule Arusha wakati bomu linarushwa na kuwakosakosa akina Mbowe, lakini mdada mmoja hakupata bahati, hadi leo ni kitendawili ambacho serikali ya CCM haikutaka kifumbuliwe.

Hiki chama kimekuwa ni tatizo kubwa kwa Tanzania.
 
The list is endless, aliwahi kusemaje Heri james, Kihongosi je? Mama Samia je?
 
Vurugu zozote zitakazotokea nchini kati ya vijana wa CCM na wasio , Spika Tulia atakuwa ima 'mtuhumiwa au Shahidi' hili hatalikwepa
Ni bahati nzuri au mbaya, ikitegemea na mtu anakolalia, kwamba CHADEMA moto wao na wa vijana wao umepigwa ganzi nyakati hizi, hasa baada ya onyo la Mwenyekiti kwa vijana wao.
Matamshi ya aina hii hayastahiri kunyamaziwa hata kidogo. Yalihitaji majibu ya haraka kutoka kwa chama hicho na maelekezo kwa vijana wao iwapo watafanywa kuwa sehemu ya "kunyooshwa."

Sasa hakuna jibu lolote, kwa hiyo kauli ya Spika ndiyo inayotawala.
 
Na Tulia anahamasisha hayo maana anajua hawako madarakani kihalali, hivyo kusemwa vibaya ni lazima. Sasa anatengeneza kinga ya wao kutokusemwa vibaya kwani anajua vijana wa CCM wanaosaka vyeo watafanya lolote ili waonekane na kupatiwa vyeo. Hii jeuri ya madaraka huwa inaondoka kunapotokea machafuko, lakini kwa lugha za kubembelezana ndio uhuni kama huu utaendelea kushamiri.
Unaonaje mama anavyoupiga mwingi huku akiwakomesha mataga na kuwapenda machadema
 
Hii jeuri ya madaraka huwa inaondoka kunapotokea machafuko, lakini kwa lugha za kubembelezana ndio uhuni kama huu utaendelea kushamiri.
Swadakta!!
Hapo umenena. Machafuko yanatakiwa kuanzia kwenye mambo kama haya wanayoyaasisi CCM wenyewe.

Hapa sipishani nawe kwa sababu yoyote ile. Ila ndiyo hivyo tena, hakuna uongozi wa kusimamia harakati hizi za kuwaonyesha CCM kwamba "kunyooka" siyo kwa upande mmoja pekee.

Watatamba sana hawa watu.
 
..kwenye demokrasia zilizokomaa Spika Tulia Ackson angelazimishwa kujiuzulu kutokana na kauli yake inayohamasisha kuvunja sheria / ukatili.
Katika mazingira ya kawaida tu Tulia alitakiwa ajiuzulu kwasababu hizi
1. Kama kiongozi wa mhimili wa kutunga sheria ameonyesha kutojua maana ya sheria na matumizi yake
2. Alikuwa na nafasi ya kupokea Mswada wa CCM wa kufuta kifungu cha uhuru wa maoni kutoka katiba ya 1977
3. Ameligawa Taifa kwa kuhamaisha vurugu zinazoweza kuvuruga amani ya nchi
4. Ajiuzulu kwasababu kama huu si msiamamo wa CCM , Tulia ameipaka matope

Tulia must go!
 
Ni bahati nzuri au mbaya, ikitegemea na mtu anakolalia, kwamba CHADEMA moto wao na wa vijana wao umepigwa ganzi nyakati hizi, hasa baada ya onyo la Mwenyekiti kwa vijana wao.
Matamshi ya aina hii hayastahiri kunyamaziwa hata kidogo. Yalihitaji majibu ya haraka kutoka kwa chama hicho na maelekezo kwa vijana wao iwapo watafanywa kuwa sehemu ya "kunyooshwa."

Sasa hakuna jibu lolote, kwa hiyo kauli ya Spika ndiyo inayotawala.
Nakubaliana nawe kabisa, hata hivyo kauli ya Spika Tulia imejenga 'sensitivity' kwahiyo ile threshold ya uvumilivu kwa vijana wasio wa CCM imepungua sana. Hapa ninaogopa sana maana wakianza 'kunyooshana' kama anavyochochea Spika Tulia hali ya nchi sijui itakuwaje! Mungu atujalie

Msajili wa vyama kakaa kimya anasubiri wapinzani wajibu utamuona anavyohemuka
Viongozi wa dini ! mambo ''yakunyooshana'' yakianza tafadhali mfunge midomo yenu. Hatuhitaji sala zenu wakati mnajua kabias Spika Tulia anachochea hali mbaya sana ya vijana '' Kunyooka'

Hakuna anayejua kunyooka nini na hapo ndipo pana hatari. Sijui ni kuuana au kupotezana au kupopoana mawe! hakuna anayejua.

Hili la Tulia ni hatari sana Rais SSH 'wakianza kunyooshana' tatizo litatua mezani mwako! kama Tulia hana baraka za CCM tafadhali fanya la maana kwa masilahi ya Nchi. Tulia must go !

Kama kauli za Tulia zina baraka za CCM basi mwacheni aendelee na uongozi lakini siku kauli yake ikianza kufanya kazi (mungu tujalie yarabi yasitokee) basi sote tutawaambia ! hamkusikia Tulia akichochea kuni?
 
Back
Top Bottom