tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 24,225
- 22,632
Ndani ya muungano wa EAC nchi ya Kenya imekuwa mstari wa mbele katika kuleta chokochoko za hapa na pale, hasa ikiichokonoa Tanzania mara kwa mara. Ingawa hivyo, Rais wa Kenya Hon Uhuru Kenyatta amefika yeye mwenyewe mubashara kuja kumuaga hayati Dr Magufuli.
Nchi za Uganda na Rwanda hazijawahi kujiingiza kwenye utata wowote ndani ya EAC mbali na lile tukio ambalo Kenya iliishawishi Uganda kusaini makubaliano ya ujenzi wa reli kutoka Mombasa hadi Kampala pasipo kuishirikisha Tanzania.
Utawala wa hayati Rais Magufuli ulikuwa unafanana sana na ule wa Kagame, hadi watu kufikia hatua ya kudhani kuwa huenda staili yake ya utawala alikuwa ameinakili kutoka kwa Kagame. Pia Museveni amekuwa mara kwa mara akiitembelea Tanzania na amesikika mara nyingi akiufagilia utawala wa hayati Magufuli.
Sasa swali ni ni: Je, kwanini Kagame na Museveni wametuma wawakilishi kuja kuomboleza kifo cha Magufuli lakini Kenyatta amekuja yeye mwenyewe mubashara? Hawa majirani wawili wanaogopa nini kuja Tanzania? Is there any hidden agenda behind their absecnce in this crucial occasion?
Marais wametoka all the way from Southern Africa up to Tanzania lakini hawa jamaa wapo hapa karibu wame-mute tu! Kama nauli ya ndege ni tatizo wangeweza kusafiri hata kwa basi na kufika Dodoma mapema kabisa kumuaga kiongozi mwenzao aliyelala mauti. Hata wangeweza kukodi basi moja wakasafiri wote kwa pamoja ili kuokoa gharama. Lakini wameamua, kwa makusudi kabisa, kutuma wawakilishi. Je, hii ni sawa?
Nchi za Uganda na Rwanda hazijawahi kujiingiza kwenye utata wowote ndani ya EAC mbali na lile tukio ambalo Kenya iliishawishi Uganda kusaini makubaliano ya ujenzi wa reli kutoka Mombasa hadi Kampala pasipo kuishirikisha Tanzania.
Utawala wa hayati Rais Magufuli ulikuwa unafanana sana na ule wa Kagame, hadi watu kufikia hatua ya kudhani kuwa huenda staili yake ya utawala alikuwa ameinakili kutoka kwa Kagame. Pia Museveni amekuwa mara kwa mara akiitembelea Tanzania na amesikika mara nyingi akiufagilia utawala wa hayati Magufuli.
Sasa swali ni ni: Je, kwanini Kagame na Museveni wametuma wawakilishi kuja kuomboleza kifo cha Magufuli lakini Kenyatta amekuja yeye mwenyewe mubashara? Hawa majirani wawili wanaogopa nini kuja Tanzania? Is there any hidden agenda behind their absecnce in this crucial occasion?
Marais wametoka all the way from Southern Africa up to Tanzania lakini hawa jamaa wapo hapa karibu wame-mute tu! Kama nauli ya ndege ni tatizo wangeweza kusafiri hata kwa basi na kufika Dodoma mapema kabisa kumuaga kiongozi mwenzao aliyelala mauti. Hata wangeweza kukodi basi moja wakasafiri wote kwa pamoja ili kuokoa gharama. Lakini wameamua, kwa makusudi kabisa, kutuma wawakilishi. Je, hii ni sawa?