Kitendo cha Mwigulu kumtaja Rais kuhusika na ufisadi Ripoti ya CAG ni sahihi?

Kitendo cha Mwigulu kumtaja Rais kuhusika na ufisadi Ripoti ya CAG ni sahihi?

Hii Nchi ina matatizo sana,sio wabunge sio Wananchi wote hawajui jinsi mifimo ya uendeshaji wa Nchi.

Nilisema siku ile kuwa SAMIA anachukulia watu kama wajinga na ni kweli ni wajinga,labda anafanya kwa malengo yake ya kisiasa.

Malipo ya projects kubwa hizo zinapitishwa na Katibu Mkuu Kiongozi,ambaye ana pata idhini moja kwa moja kutoka kwake.Sasa iweje aseme watu wanaongeza bei.
 
Hakuna mantiki kuamuangushia Mwigula Nchemboo jumba bovu wezi ni wengine ye anaingiaje? Watu wanaweka mezani documents ziko sawa utajuaje kuwa ukilipa hawatekelezi?
 
Mwigulu yupo sahihi kabisa,huyo spika wenu anayeendasha Mhimili wa Serikali lakini hajuo uendeshaji wa serikali ni matatizo.
 
Mwigulu Nchemba kwenye utetezi wake bungeni amemtaja Rais kuwa ndiye anayeidhinisha fedha zote za Serikali jambo ambalo limezua utata na hisia kubwa kwa wananchi kuhusiana na ufisadi mkubwa uliotajwa na CAG kwenye maeneo mbalimbali .

Ufisadi mkubwa umetajwa kwenye Wizara ya Fedha, Wizara ya Nishati, Wizara ya Afya, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Habari na Wizara ya Maji, TAMISEMI na maendeleo mbalimbali.


ni sahihi kabisa.....inakuwaje rais unamteua chokoraa asiye na adabu kuwa mawaziri? tena waziri wa fedha na mipango?
 
Hii nchi ina sheria za kipumbavu na kilofa sana zilizotungwa na malofa.Rais akikosea anajifanya hajahusika lakini akifanya cha kusifiwa anadai kafanya yeye.Mwiguku uko sahihi kabisa rais kaidhinisha na kama kukosea na yeye asijitoe.
 
Mwigulu Nchemba kwenye utetezi wake bungeni amemtaja Rais kuwa ndiye anayeidhinisha fedha zote za Serikali jambo ambalo limezua utata na hisia kubwa kwa wananchi kuhusiana na ufisadi mkubwa uliotajwa na CAG kwenye maeneo mbalimbali .

Ufisadi mkubwa umetajwa kwenye Wizara ya Fedha, Wizara ya Nishati, Wizara ya Afya, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Habari na Wizara ya Maji, TAMISEMI na maendeleo mbalimbali.


"Stupid" natamani sana "Prof. Mussa Assad" ateuliwe waziri wa fedha yule bwana anahofu ya Mungu.
 
Mwigulu Nchemba kwenye utetezi wake bungeni amemtaja Rais kuwa ndiye anayeidhinisha fedha zote za Serikali jambo ambalo limezua utata na hisia kubwa kwa wananchi kuhusiana na ufisadi mkubwa uliotajwa na CAG kwenye maeneo mbalimbali .

Ufisadi mkubwa umetajwa kwenye Wizara ya Fedha, Wizara ya Nishati, Wizara ya Afya, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Habari na Wizara ya Maji, TAMISEMI na maendeleo mbalimbali.


Mwigulu sio mwadilifu ila alichokisema bungeni ni cha kweli tupu ila mnataka kumtoa kafara (scapegoat) kuepuka dhahama ya siku chache zijazo kwenu ninyi watawala wezi, walafi na wabadhirifu wa mali za umma na wenye dhuluma lukuki dhidi ya wananchi wa kawaida.
 
Rais ali bariki wizi. Wale kwa urefu wa kamba yao.
 
Mbona Rais anapopeleka maendeleo sehemu mbalimbali huwa wanamsifia? amejenga zahanati, barabara, madarasa, sifa zote kwake..

Tena Ole Sendeka ndie huwa kinara wa kutoa hizo sifa.

Kwanini basi hizo pesa Rais anazopeleka kwenye hayo maendeleo zikipigwa asihusishwe? badala yake lawama waangushiwe watendaji tena kwa kunukuu ibara ya Katiba?!

Basi kama ndio hivyo, kuanzia leo wanapojenga barabara, shule, zahanati.. pongezi wapelekewe hao watendaji.

Lakini tofauti na hapo, Rais anahusika kwa yote hayo, Mwigulu yupo sahihi, ndio maana Rais amekuwa mpole kwa wapigaji, anawabembeleza waondoke wenyewe ofisini.
Ww ni GT,unastahili nyota 3
 
Tatizo ni kwamba Rais huwa anapewa sifa kuwa amepeleka fedha mahali labda kujenga barabara au hospitali au shule. Kwa muktadha huo Rais ndio huidhinisha malipo hayo kwa hiyo kuhalalisha hiyo sifa anayopewa!! Sasa huo ni mtego mbaya sana!! Ukukubali sifa inabidi ukubali pia lawama kama pesa zimepigwa maana ulishakubali kuwa pesa huwa unapeleka wewe!! Taasisi ya urais iachane na sifa za binafsi ambazo siyo halisi badala yake sifa iende kwa serikali moja kwa ,moja kupitia watendaji na lawama ziende kwa serikali moja kwa moja pia kupitia watendaji!!! Ukikubali sifa ni ngumu kukataa lawama!! Maana zote zinatokana na pesa zinazodaiwa umepeleka wewe kwa maana ya kuidhinisha!!
 
Rais ali bariki wizi. Wale kwa urefu wa kamba yao.
Hapo kwa kweli alikosea!! Alilalamika tu kuwa wanakula kwa kuvuka urefu wa kamba zao hadi wanavimbiwa!! Ilitoa picha kuwa wakila kwa mujibu wa urefu wa kamba zao na wasivimbiwe hilo siyo tatizo!!
 
hakujua kama atakuwa mwizi
Mwigulu ni mwizi tangu enzi za Kikwete na kuna tuhuma ilikuwa inamhusu moja kwa moja ila kwa vile ccm imekaa kwa maslahi ya kulindana ndiyo maana unaona bado yupo kwenye Baraza la Mawaziri na kupewa Wizara nyeti ambayo ndiyo Roho ya nchi.
 
Sijui ni masikio yangu,nilimsikia Waziri wa Fedha na Mipango , wakati anajibu hoja ya Mbunge wa Simanjiro,akisema ninanukuu "Utaratibu wa malipo ya Serikali kuidhinishwa na Rais ,ulianza kipindi cha Serikali ya awamu ya nne wakati yeye akiwa naibu Waziri wa Fedha na umeendelea kwa awamu ya tano na awamu ya sita".

Maoni yangu

-Kumbe Matakwa ya Katiba yetu yameanza kuvunjwa inakaribia miongo 2,
-Viongozi wetu,wanatupiga changa la macho wanapoahidi kulinda na kutetea Katiba ya JMT., wakati wanafanya kinyume chake.

Ushauri
-Viongozi waheshimu na kulinda Katiba ya JMT kama wajivyoapa.
-Mchakato wa Katiba Mpya,uharakishwe/Ukamilishwe.
 
Back
Top Bottom