Kitete cha Simba ugenini, nini shida?

Kitete cha Simba ugenini, nini shida?

Muhimu mashabiki wenzangu waliopo dar na mikoa ya jirani, tujitokeze kwa wingi uwanjani. Umoja wetu ndio nguvu yetu, kama kauli mbiu yetu ya #nguvuMoja inavyosema. Mechi ya jumamosi ni mechi kubwa na muhimu kuliko zote tulizocheza msimu huu. Nguvu ya kucheza nyumbani ni mashabiki. Na mashabiki ndio sisi. Tusitegeane kwenda uwanjani, usipange kukosa. Uwepo wetu tu uwanjani ni silaha tosha ya kuwachanganya kisaikolojia Vita. Tutimize wajibu wetu kama mashabiki kwa kujitokeza kwa wingi Jumamosi, na kisha tumuachie kocha uchebe, benchi la ufundi na wachezaji kutimiza wajibu wao uwanjani kwa kuchukua points 3.
Vita tunawaheshimu, na tunaheshimu historia yao pia katika soka la Afrika, ila Jumamosi watatusamehe, tunahitaji points 3. Hamna namna nyingine

the Legend☆
Uko Sawa mkuu! Mechi ya jumamosi si muhimu kwa Simba pekee ila pia soka la Tz na Africa Mashariki kwa ujumla.
 
Uko Sawa mkuu! Mechi ya jumamosi si muhimu kwa Simba pekee ila pia soka la Tz na Africa Mashariki kwa ujumla.
Ni kweli kabisa mkuu. Kwa hili nlitegemea hata wapinzani wetu wa jadi waungane na sisi, ila wao ndo wamekua mstari wa mbele kujaribu kutuvunja moyo. Hawajui ya kua kwa Simba kufika mbali zaidi katika michuano hii sio tuu ni faida kwetu kama klabu, ila ni kwa soka la Tanzania kwa ujumla, kwa maana itaongeza 'coefficient' ya nchi, na kuleta uwezekano wa klabu zaidi ya moja kupata nafasi ya kushiriki klabu bingwa miaka ijayo. Watu wanashangaa inakuaje Congo wawe na Vita na Mazembe, au South Africa wawe na Orlando Pirates na Mamelodi (Brazilians) kwenye klabu bingwa, ilihali Tanzania ipo Simba tu. Hawajui performance ya timu za nchi husika kwenye michuano ya CAF inaongeza coefficient ya nchi, na ndiyo hiyo inaamua nchi husika ipeleke timu ngapi

the Legend☆
 
Kinachoboa uwanjani ni utaratibu wa kuingia, mnaminyana kwenye foleni kama mabasi ya Mwendokasi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu uwe unaingilia kule shamba la bibi, kule wanapoingiliaga Yanga. Hamnaga nyomi kama la kule mbele. Mimi huwa ndo nnapoingilia, nkishapita getini natembea kurudi upande pendwa wa mnyama

the Legend☆
 
Wachezaji wetu hawajiamini .wanajiona kama wamepotea njia wanabaki kubutua tu mpira bora liende.
Angalia hata timu yetu ya taifa ikiwa ugenini ni the same..
Klabu zetu zinapaswa kupata wachezaji wanaojiamini kwa uwezo wao hata wakiwa nje ya Tanzania.. Kwa timu ya taifa ni kupata players wengi wanaocheza soka la kulipwa ligi kubwa tofauti na yetu.
 
Zamarek, al ahly, esperance. Nszo zinakitete ugenini? Lazima tukubaliane kuwa kwa mfumo wetu wa africa ni ngumu kushinda ugenini. Tumetofautiana mengi sana haswa mazingira na hali ya hewa, Hii inatokea hata timu za kiarabu zikija kwenye ukanda wetu. Pili, timun zinakosa suport ya washabiki wachezaji wanakosa morali
 
Swali zuri sana mkuu. Nawashangaa sana wanaosema eti game itakua ngumu sababu vita anajua umuhimu wake. Suala sio kujua umuhimu, kama ni umuhimu hata game waliyodroo na Saoura tena congo walijua umuhimu wake. Suala ni je wanaweza kutufunga nyumbani, katika mechi muhimu kwetu kuliko zote tulizocheza msimu huu, mechi ambayo tunajua fika tukishinda inaenda kuiweka Simba katika ramani ya soka la Afrika, mechi ambayo inaenda kuandika historia mpya ya klabu yetu, ndani na nje ya nchi, tena katika uwanja wa nyumbani, mbele ya mashabiki 60k+. To be honest sioni namna yoyote ambayo Vita anaweza kutoka salama taifa

the Legend☆
Simba alifungwa mbili bila shamba la bibi tena ilikua fainali dhidi ya stella ya Abdjan mbele ya rais wa wakati uo Mzee Mwinyi. Tena Simba iliyokua imekamilika achana na Simba hii Chai ya rangi. Mfadhili mkuu wa Simba Azim Dewji alitoa ahadi ya gari aina ya (KIA) kia kila mchezaji lakini walipigwa. Juz kati wakaja Mazembe wakampiga simba 3 , Nyuma kidogo walikuja Enyimba kampiga simba 3 sasa vita wakija sijui ubao utasomekaje.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simba alifungwa mbili bila shamba la bibi tena ilikua fainali dhidi ya stella ya Abdjan mbele ya rais wa wakati uo Mzee Mwinyi. Tena Simba iliyokua imekamilika achana na Simba hii Chai ya rangi. Mfadhili mkuu wa Simba Azim Dewji alitoa ahadi ya gari aina ya (KIA) kia kila mchezaji lakini walipigwa. Juz kati wakaja Mazembe wakampiga simba 3 , Nyuma kidogo walikuja Enyimba kampiga simba 3 sasa vita wakija sijui ubao utasomekaje.

Sent using Jamii Forums mobile app
Vita walishakuja na washaondoka pia. Vipi ubao ulisomekaje mkuu?

the Legend☆
 
Simba alifungwa mbili bila shamba la bibi tena ilikua fainali dhidi ya stella ya Abdjan mbele ya rais wa wakati uo Mzee Mwinyi. Tena Simba iliyokua imekamilika achana na Simba hii Chai ya rangi. Mfadhili mkuu wa Simba Azim Dewji alitoa ahadi ya gari aina ya (KIA) kia kila mchezaji lakini walipigwa. Juz kati wakaja Mazembe wakampiga simba 3 , Nyuma kidogo walikuja Enyimba kampiga simba 3 sasa vita wakija sijui ubao utasomekaje.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mohamed Mwameja muulize kuhusu hizo kia,pia mpira usikalili sana mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo ukiisoma hii post yako period inakushika hata mama ilishapita...😄😄😄 Mwezi huu wote utakuwa mwezini mpaka ukome kudandia dandia wanaume... Umeyaona sasa jana? Na bado.... Mwezi mzima unaenda hedhi....

Simba inawachezaji wenye umri mkubwa, wakikutana na watu wanao kimbiza, simba wanapoteana vibaya sana. Soura walikua wana kaba kuanzia mbele kwa kasi, Soura wakipata mpira ni mbio nyingi, wame cheza kwa kasi karibu dakika 75 kweli wachezaji wetu wangeweza kucheza dk 75 kwa kasi ile? Wachezaji wa Soura karibu wote mpira unakaa mguuni, Tutawalaumu bure Wahenga wetu. Apa Nyumbani Simba uwa wanatumia Gharama kubwa sana kushinda mechi yaani mambo ya nje ya uwanja ni mengi mno.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom