Muhimu mashabiki wenzangu waliopo dar na mikoa ya jirani, tujitokeze kwa wingi uwanjani. Umoja wetu ndio nguvu yetu, kama kauli mbiu yetu ya #nguvuMoja inavyosema. Mechi ya jumamosi ni mechi kubwa na muhimu kuliko zote tulizocheza msimu huu. Nguvu ya kucheza nyumbani ni mashabiki. Na mashabiki ndio sisi. Tusitegeane kwenda uwanjani, usipange kukosa. Uwepo wetu tu uwanjani ni silaha tosha ya kuwachanganya kisaikolojia Vita. Tutimize wajibu wetu kama mashabiki kwa kujitokeza kwa wingi Jumamosi, na kisha tumuachie kocha uchebe, benchi la ufundi na wachezaji kutimiza wajibu wao uwanjani kwa kuchukua points 3.
Vita tunawaheshimu, na tunaheshimu historia yao pia katika soka la Afrika, ila Jumamosi watatusamehe, tunahitaji points 3. Hamna namna nyingine
the Legend☆