GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
- Thread starter
- #21
Zingine sawa, lakini AZAM ya Mzee Saidi, sidhani!Unaweza kuta kwenye azam marine kuna fridge kabisa za kutunzia pork kwa mda iwapo safarini.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Zingine sawa, lakini AZAM ya Mzee Saidi, sidhani!Unaweza kuta kwenye azam marine kuna fridge kabisa za kutunzia pork kwa mda iwapo safarini.
Ila anapendwa na walaji wake wote!
Hata hivyo ni tamu!Eti umeshuhudia kwa kinywa 😅
Ila hao jamaa wanaonja bana, asikwambie mtu
Natamani kuifuatilia hiyo habari! Very interesting!!!Kihistoria Kitimoto ameingia Tanganyika kutokea Zanzibar.
Aisee!Walaji walishindwa kuvumilia baada ya kusikia muungano watakosa vyote
Kwa kilugha hata kwetu inatafsirika hivyo, yaani nyama ya kuku, samaki, mboga za majani, maharage nk nk.Kule "kwetu" wanaiita mboga
Uvumilivu gani wakati walaji wakubwa ni Wazanzibari wenyewe? Tena pale inapotengenezwa pana lodge ambapo wale viongozi na watu maarufu wasiopenda kuonekana wanapoagiza watengenezewa kitimoto huweka na booking ya chumba kabisa ili walie vyumbani wasionekane?Japo Zanziba ni sehemu ya Tanzania, inafahamika kuwa asilimia kubwa ya wakazi wake ni Waislamu. Na inafahamika kuwa nguruwe, au MBUZI KATOLIKI kama inavyoitwa na baadhi ya watu, ni wanyama haramu kwa Waislamu.
Lakini unajua hiyo mboga inapatikana hata Zanzibar? Kwa ambaye hajawahi kufika huko, anaweza asiamini. Hata mimi nilikuwa na mtazamo huo. Ulibadilika baada ya kushuhudia kwa macho yangu na kinywa changu.
Ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika Zanzibar. Nilipoulizia gesti iliyopo sehemu tulivu, baada ya kutoridhishwa na zilizopo maeneo ya Darajani, niliambiwa niemde kwa BI JANETH, mahali wanakouza kitimoto. Ipo Mbwe, Unguja.
Nilitilia mashaka hayo maelezo, lakini nikaamua kujiridhisha. Hata baada ya kufika kwa BI JANETH, na kuulizia vyakula vinavyopatikana hapo, bado sikuamini nilipotajiwa mpaka kitimoto. Lakini nilipojionea mwenyewe kwa macho yangu na kinywa changu, sikuwa na sababu tena ya kuwa na mashaka, badala yake, nilibaki na mshangao. Niligundua kuwa Mzanzibar si kama nilivyokuwa nikiifahamu, kwa kuambiwa.
Sijui ilifika fikaje hapo kwenye hiyo lodge! Sijui kama nguruwe wanafugwa huko Zanzibar au wametolewa bara.
Lakini naamini Serikali na Raia wanafahamu kuwa kuna biashara kama hiyo huko Zanzibar. Kitendo cha kuruhusu watumiaji wa hiyo mboga kujinafasi bila kubughudhiwa, hata kama ni katika baadhi ya maeneo tu, kinaonesha wazi kuwa Wazanzibar ni watu waelewa na wavumulivu pia.
Wameonesha kwa vitendo kuwa japo wao (wengi wao) hawaitumii kitimoto, wanaheshimu Imani za wengine. Ndiyo maana hawajaweka ukwazo kwa wanaohitaji hiyo mboga. Huo ni ustaarabu wa hali ya juu!!!
Hongereni sana Wazanzibar!
😀Waislam wanakula kitimoto safi kabisa, Kuna mashiekh kadhaa walikua wananiagiza,
Kivipi mkuu? Mimi nilikuwa natafiti tu, kujiridhisha kama ni yenyewe!Mtoa mada ulifaidi minofu [emoji23]
Nafikiri ni kwa sababu ilikuwa kati ya miradi pendwa ya Mashirika ya Kanisa Katoliki. Inasemekana Seminary nyingi za KATOLIKI zilikuwa na mradi wa ufugaji nguruwe.Hivi jina la mbuzi katoliki lilipatikanaje?
Aisee!!!Uvumilivu gani wakati walaji wakubwa ni Wazanzibari wenyewe? Tena pale inapotengenezwa pana lodge ambapo wale viongozi na watu maarufu wasiopenda kuonekana wanapoagiza watengenezewa kitimoto huweka na booking ya chumba kabisa ili walie vyumbani wasionekane?
Vijana wa kipemba na wakiarabu waliojizira wale huwa ndiyo wanailia palepale nje ( bar )
Aisee!Mwezi wa Ramadhani hii kitu inakosaga wateja kabisa
Bado tunakusubiri.nakuja