Kitimtim Kipawa - JK azuiliwa kupita

Kitimtim Kipawa - JK azuiliwa kupita

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2008
Posts
5,457
Reaction score
963
HEBU TUJULISHENI MLIOKO KIPAWA...mabomu ya machozi huko...ni aje wamemzuia mkuu wa nchi asipite?
 
Ni kweli VC,

Mabomu ya machozi yanaendelea kupigwa...

Hii imesababisha hata nikate simu kwa mwakilishi wetu kwenye Press Conference ya Zitto ili kuongea na huyu aliye eneo la tukio.

Hali si shwari
 
Kulikoni tena wakuu. Ni maswala ya upanuzi wa airport au ni nini?
Yeah,

Wananchi hawataki kulipwa fidia kwa sheria ya mwaka 1967. Wanataka sheria mpya ndo itumike. Leo ndio siku iliyokuwa imepangwa kuanza kulipwa kwa wananchi hawa lakini walitoa tamko kuwa hawakubaliani na serikali na hivyo leo wakaamua kutanda barabarani kumzuia JK kwenda Airport.
 
Bila shaka ni masuala ya fidia.Wengi wanapinga kulipwa fidia kwa kutumia sheria ya zamani wakati tayari ipo sheria mpya.

Walioko uko tafadhali tupeni habari kamili
 
HAli kidogo imetulia ila sie tulio jirani nao tumeyapata hayo machozi
 
Bila shaka ni masuala ya fidia.Wengi wanapinga kulipwa fidia kwa kutumia sheria ya zamani wakati tayari ipo sheria mpya.

Walioko uko tafadhali tupeni habari kamili
Ngongo,

Ndicho chanzo, kuna mtu yupo jirani na eneo hilo, nitakufahamisheni hatma ya wananchi hawa.
 
HAli kidogo imetulia ila sie tulio jirani nao tumeyapata hayo machozi
Great,

Afadhali umetufahamisha walau kama hali imetulia. Ilikuwaje? Nani alikuwa anapiga mabomu hayo? Ili iweje? Kwanini wananchi watawanyishwe? Kwanini rais asiwasikilize kabla ya kuendelea na safari yake? Kipi muhimu kwake?
 
kwa hesabu za haraka haraka yamepigwa zaidi ya kumi tulikuwa tunawachungulia kwa dirishani tu vijana wa ukonga walivyokuwa wanakimbizana na wakazi hao waliogoma kulipwa pesa zao leo sababu kubwa ni huo mfumo wanaotaka kuutukia.

Ila kuna bango moja limenifurahisha linasema "HATUDANGANYIKI NA VIJISENTI VYENU"
 
Great,

Afadhali umetufahamisha walau kama hali imetulia. Ilikuwaje? Nani alikuwa anapiga mabomu hayo? Ili iweje? Kwanini wananchi watawanyishwe? Kwanini rais asiwasikilize kabla ya kuendelea na safari yake? Kipi muhimu kwake?



Mkuu si unajua tena hii sirikali yetu ikiamua kitu imeamua?
Vijana wa hapa jirani na kipawa (FFU) ndio walikuwa na haka kajizoezi maana yamekaa muda mrefu kwenye ile stoo yao hayajatumika nao hawajafanya mazoezi ya kupiga na kukamata watu.

Ili muheshimiwa apite asibughuziwe.

Wameona hiyo ndio njia sahihi ya kuwatawanya wananchi but hali halisi walikuwa wafunge barabara wakatu mkuu anaporejea kutoka butihama ili wamweleze kilio chao kwanini serikali yake haiwatendei haki hao wakaazi wa huku Kipawa.

Kwasababu amechoka anahitaji kupunzika

Umuhimu wake ni kupita kwenda Ikulu .......

 
Great,

Afadhali umetufahamisha walau kama hali imetulia. Ilikuwaje? (Watu wamechoka)
Nani alikuwa anapiga mabomu hayo? (Wale jamaa wa "Ndio afande")
Kwanini wananchi watawanyishwe? (Mkuu anawahi matibabu)
Kwanini rais asiwasikilize kabla ya kuendelea na safari yake? Kipi muhimu kwake? (Afya yake kwanza)

>Kuna siku yaja lakini hatuijui, Inshallah<
 
lakini watalipwaje kwa sheria mpya wakati uamuzi umefanyika kwa sheria ya zamani? wenye kufahamu sheria nifafanulieni tafadhali...
 
kwa hesabu za haraka haraka yamepigwa zaidi ya kumi tulikuwa tunawachungulia kwa dirishani tu vijana wa ukonga walivyokuwa wanakimbizana na wakazi hao waliogoma kulipwa pesa zao leo sababu kubwa ni huo mfumo wanaotaka kuutukia.

Ila kuna bango moja limenifurahisha linasema "HATUDANGANYIKI NA VIJISENTI VYENU"
Ahsante kwa taarifa mkuu BornTown.

Inasikitisha lakini ndivyo ilivyo! Tanzania zaidi ya unavyoijua
 
Jamani wananchi msikubaliane na lolote , huyo bwana msanii, tumieni kura zenu vizuri 2010 kumadabisha, manyanyaso kwa wananchi yamezidi. Kwanini mlipwe kwa sheria ya 1967 na kunasheria mpya ya malipo 2002? Wizi mtu, wanatafuta hela za campaign 2010 wawanunulie kanga na kofia kwa hela zenu, zichukueni au ********** ila angalia ametoka safari hivyo amechoka.
 
Kusema ukweli hii nchi inamaudhi sana wakati mwingine unaweza kukasirishwa ukajiuliza hivi hii nchi yenye sifa kwa wenzetu wanayo yafanya hi ya haki. Mfano hawa jirani zangu hapa kipawa wanataka kuwalipa fidia ya mwaka 1967 !!!!! kweli hii hi haki maana wakati sheria ya mwaka 67 inatungwa laki moja ya pesa ilikuwa ni nyingi sana mtu waweza nunu hata na gari ukajenga nyumba yako na balance ikabaki kubwa tu ya kutunza heshima mtaani.

Karne hii ya sasa mfuko mmoja wa simenti unauzwa sh. 14500/ ukitaka kujenga nyumba ya vyumba viwili vya kulala na kajisebule potelea mbali kule posta tukakuweka nje na kuzungushia magunia n kikawa cha passport size.
uje upewe shilingi laki 5 utazifanya nini?
 
pole SINKALA, kama nakuona vile unalia kuna bomu limeanguka mbele yako au nakufananisha?
 
Mambo ya Mbeya, Mawe na Kuzomewa ....Leo tena kazuiwa

I am Smelling French Revolution very soon than later, wananchi tumechoka!
 
lakini watalipwaje kwa sheria mpya wakati uamuzi umefanyika kwa sheria ya zamani? wenye kufahamu sheria nifafanulieni tafadhali...

kwasababu walijafanyiwa tena tasmni upya nadhani ilikuwa mwaka jana mwanzoni na kama walikuwa wanlijua hilo kwania kipindi kile (awamu ya kwanza) waliposema wanataka kupanua kiwanja hawakuwalipa kipindi kilekile waje wawatese weeeee halafu waseme wanwalipa now hii sio haki.
geuza upande wapili wa shilingi ungekuwa wewe ungefanyaje??
 
Yaani Afrika yatupasa kumwomba MUNGU sana atuponye na hii laana iliyoko juu la bara letu. Unyonyaji na dhuluma kila mahali. Maana kama kuna sheria mpya iweje wawalipe kwa sheria ya mwaka 1967 ambapo USD 1 ilikuwa sawa na Ths 1 kama si 2 Tshs. (mwenye takwimu sahihi anisahihishe). Ina maana watapunjwa kwa kama 650% hadi 1300 % hivi. Huu ni wizi mkubwa unaotaka kufanywa na serikali isiyojali watu wake. May GOD forbid.
 
Back
Top Bottom