kitovu cha mtoto kimeharibu ndoa

kitovu cha mtoto kimeharibu ndoa

Magical power

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2022
Posts
2,158
Reaction score
5,626
kitovu cha mtoto kimeharibu ndoa

Kaka angu magical power, nimeamua kuikimbia ndoa ili nimuokoe mwanangu naona walikuwa na nia mbaya juu ya mtoto. Kaka hata kujifungua tu kidogo nifie hospital nikasaidiwa na mkunga kwa uzoefu wake aliywesha dawa fulani ya kienyeji kwaa uzoefu wake alisema nisingeweza kujifungua salama alipoona dalili za kufa yaani uchungu unakuja na kupoa siku tatu akaona anisaidie dawa ya kienyeji nikanyw nikajifungua ila mtoto alikuwa amechoka sana

Simu za ukweni zilikuwa nyingi kuliko muda wote wa ujauzito za mama mkwe na bibi mzaa mama mkwe. Walipoambiwa nimejifungua wakauliza mama na yeye mzima walipoambiwa mzima ila mtoto hana nguvu wakamwambia atakuwa huyo mtoto amekufa niliumia sana😢

Kaka Mungu akampigania mwanangu akawa hai na akaanza kukua sasa ishu ikahamia kwenye kitovu yaani wakasema kitovu na beseni lake viende kwa bibi yake mume wangu
Sikutaka kuonesha kukataa kwasababu niliogopa sana wasije kumkata kitovu mtoto kabla ya wakati nikawa makini sana kuhusu kitovu. Siku moja jioni mume wangu hayupo kikakatika kitovu nikakichukua nikatupa chooni alipofika nikamwambia kitovu kimekatika akaniomba nikamwambia nimekutupa chooni akanipiga akitaka kitovu cha mtoto akawapigia Bibi na mama ake wakaniandama wakasema bila kitovu kuwapa hakuna ndoa na mtoto wao.

Wakanipa masaa nitoe kitovu niwape. Usiku nikaamka kumuosha mtoto beseni lake sikuliona nikaanza kulitafuta nikalikuta kwenye mfuko limevunjwavunjwa limefichwa alitume kwao, nami nikalihamisha alipoliweka hilo beseni leo ameenda kazini nami nikachukua vitu vyangu na vya mtoto niko njiani kwenda kwetu nimuokoe mtoto na beseni nimelichukua

Kaka Magical power nimefanya kosa kweli naomba uniambie
 
Mkishaona kijana ana kazi, nyumba na gari nzuri mambo mengine ya msingi huwa hamuangalii mwisho wa siku mnaishia kuingia familia za kichawi ngoja Mshana Jr aje akuambie umuhimu na nguvu ya kitovu cha mtoto.
 
Kitu ambacho siku zote watu wanshauriwa na hawataki kuelewa ni USIPENDE KUWAAMBIA.WATU HABARI ZAKO. Ukiwa mjamzito, kama usipowaambia watu wa kwenu haitakudhuru basi usiwaambie kabisa, jifiche sana wao waje kukutana na mtoto.

Sasa mtu anaenda kujifungua anatangazia umma kwanini asifanyiwe michezo ya hovyo na vimbwanga.
 
Back
Top Bottom