Kitu alichofanya Yesu ambacho watumishi wa siku za mwisho wanakiogopa

Kitu alichofanya Yesu ambacho watumishi wa siku za mwisho wanakiogopa

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Kuulizwa maswali.

Yesu alikuwa haogopi kuulizwa maswali. Hata kama ni ya kijinga atatafuta namna ya kukujibu ili uache huo ujinga.

Watu wengi wanaelewa kwa njia ya maswali. Nimeona wengi wanapenda kuongea mambo yao ila hawana ujasiri wa kuwaacha wanaowasikiliza wahoji na kuuliza maswali ili waelewe kwa kina.

Hii tabia imelekea kuwa na waumini wenye uelewa finyu na mashabiki wasio na ujasiri kwa wanayoyaamini.

Hii tabia imesababisha kuwa na watumishi majasiri kwenye mimbari ila waoga sana kwenye uhalisia wa maisha.

Tujifunze kwa Yesu.

Sabato njema.
 
Ukiwauliza sana wanakuwa wakali, au kukuita msumbufu au mjuaji...

Mimi nikikuuliza swali ukanikwepa ukawa mkali basi... Nakushusha vyeo na nitakuamini kwa mashaka sana, hata kama ni mchungaji naweza kuama kanisa
 
Ukiwauliza sana wanakuwa wakali, au kukuita msumbufu au mjuaji...

Mimi nikikuuliza swali ukanikwepa ukawa mkali basi... Nakushusha vyeo na nitakuamini kwa mashaka sana, hata kama ni mchungaji naweza kuama kanisa
Yesu alijibu maswali. Yale ya kikorofi alijibu kikorofi.
Ya kejeli aliyapuuza. Ya mtu kutaka kuelewa ili aokolewe aliyajibu kwa kina na ufafanuzi wa juu. Hii hekima watumishi hawapaswi kuiepuka.
 
Kuulizwa maswali.
Yesu alikuwa haogopi kuulizwa maswali. Hata kama ni ya kijinga atatafuta namna ya kukujibu ili uache huo ujinga.

Watu wengi wanaelewa kwa njia ya maswali. Nimeona wengi wanapenda kuongea mambo yao ila hawana ujasiri wa kuwaacha wanaowasikiliza wahoji na kuuliza maswali ili waelewe kwa kina.

Hii tabia imelekea kuwa na waumini wenye uelewa finyu na mashabiki wasio na ujasiri kwa wanayoyaamini.

Hii tabia imesababisha kuwa na watumishi majasiri kwenye mimbari ila waoga sana kwenye uhalisia wa maisha.


Tujifunze kwa Yesu.

Sabato njema.
Bado siungi mkono hoja yako kwani watu(waamini na ww ukiwa mmojawapo) wanataka waulize maswali wakati wa Ibada au ndani ya muda wa kuabudu. Hao hao wenye kutaka kuuliza maswali wakipewa Fursa e.g. wakialikwa kwenye kongamano, vikao, semina au warsha hawajitokezi. Wanakuwa na madai ya kuwa eti wapo Busy.
Hao hao ni ndio wenye kupotosha Taarifa zinazotolewa katika matangazo rasmi siku ya kuabudu au Sala. Hawapo tayari kujitokeza au kutumia Taratibu zilizopo ili kuhoji,kuuliza maswali n.k. Wanakuwa na "vijiwe" na huwavuta watu kwa maneno ya kujikweza na kukosoa watu wengine(Hususan wachungaji) huwanyoshea vidole sio wachungaji tu lakini hata na viongozi wengine wa Kanisa au wale wanaohudhuria vizuri siku za kuabudu au sala kanisani kwa kudai wanazifahamu siri zao na mbinu wanazotumia kuwahadaa waamini. Hao ni Mafarisayo.
Kama kuna maswali:
1. Mfuate mchungaji au kiongozi mlengwa umuulize maswali ana kwa ana. Haifai na wala sio busara maswali yaulizwe ndani ya Ibada. Akikuambia hana nafasi omba appointment au
2. Andika Swali/Maswali na umkabidhi mchungaji au kiongozi mhusika na utake majibu ama verbally au kwa maandishi pia.
3. Usipende sana kuuliza maswali bali jaribu kutafuta majibu ww mwenyewe kwa kujisomea au hata kwenye mitandao.
4. Kumbuka mchungaji ni mtu kama ww i.e. anavionjo vyake na madhaifu yake. Wengine wanaweza kuonesha kukasirika au kuudhika na wengine kukuona ww ni msumbufu, mkorofi, una kimbelembele au mzabizabina na pengine mchungaji akajenga chuki dhidi yako.
Mwisho kumbuka hata Yesu maswali mengine aliyapotezea e.g. Pilato alimwuliza: " Je wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi? Yesu alimjibu kwamba wewe umesema kwamba mm ni mfalme wa ....Mat.27:11 - 66.
Tena inafaa kuzingatia kwamba kuruhusu mswali kunaweza kuamsha Roho ya mtafaruku ndani ya kanisa. Inafaa sana ujue kwamba Ibilisi (Shetani au Roho ya Uasi) anahudhuria sana sana kanisani na huwa yupo makini sana ili asipoteze nafasi mpenyo kuvuruga kundi. Ibilisi haendagi bar au kwenye madisco kwani kule wapo wawakilishi wake na wanapiga kazi vizuri.
Naomba niishie hapo- Ubarikiwe sana.
 
Yesu alijibu maswali. Yale ya kikorofi alijibu kikorofi.
Ya kejeli aliyapuuza. Ya mtu kutaka kuelewa ili aokolewe aliyajibu kwa kina na ufafanuzi wa juu. Hii hekima watumishi hawapaswi kuiepuka.
Yesu WA kwenye biblia alikua kizungumkuti mno👇

Yohana 14:8-9
Filipo akamwambia, Bwana, tuonyeshe Baba, na yatutosha. Yesu akamwambia, Je! nimekuwa pamoja nanyi siku hizi zote, nawe hujanijua, Filipo? Yeyote aliyeniona mimi amemwona Baba.
👇
Yohana 5:37
Naye Baba aliyenituma amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wowote, wala sura yake hamkuiona.
 
Bado siungi mkono hoja yako kwani watu(waamini na ww ukiwa mmojawapo) wanataka waulize maswali wakati wa Ibada au ndani ya muda wa kuabudu. Hao hao wenye kutaka kuuliza maswali wakipewa Fursa e.g. wakialikwa kwenye kongamano, vikao, semina au warsha hawajitokezi. Wanakuwa na madai ya kuwa eti wapo Busy.
Hao hao ni ndio wenye kupotosha Taarifa zinazotolewa katika matangazo rasmi siku ya kuabudu au Sala. Hawapo tayari kujitokeza au kutumia Taratibu zilizopo ili kuhoji,kuuliza maswali n.k. Wanakuwa na "vijiwe" na huwavuta watu kwa maneno ya kujikweza na kukosoa watu wengine(Hususan wachungaji) huwanyoshea vidole sio wachungaji tu lakini hata na viongozi wengine wa Kanisa au wale wanaohudhuria vizuri siku za kuabudu au sala kanisani kwa kudai wanazifahamu siri zao na mbinu wanazotumia kuwahadaa waamini. Hao ni Mafarisayo.
Kama kuna maswali:
1. Mfuate mchungaji au kiongozi mlengwa umuulize maswali ana kwa ana. Haifai na wala sio busara maswali yaulizwe ndani ya Ibada. Akikuambia hana nafasi omba appointment au
2. Andika Swali/Maswali na umkabidhi mchungaji au kiongozi mhusika na utake majibu ama verbally au kwa maandishi pia.
3. Usipende sana kuuliza maswali bali jaribu kutafuta majibu ww mwenyewe kwa kujisomea au hata kwenye mitandao.
4. Kumbuka mchungaji ni mtu kama ww i.e. anavionjo vyake na madhaifu yake. Wengine wanaweza kuonesha kukasirika au kuudhika na wengine kukuona ww ni msumbufu, mkorofi, una kimbelembele au mzabizabina na pengine mchungaji akajenga chuki dhidi yako.
Mwisho kumbuka hata Yesu maswali mengine aliyapotezea e.g. Pilato alimwuliza: " Je wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi? Yesu alimjibu kwamba wewe umesema kwamba mm ni mfalme wa ....Mat.27:11 - 66.
Tena inafaa kuzingatia kwamba kuruhusu mswali kunaweza kuamsha Roho ya mtafaruku ndani ya kanisa. Inafaa sana ujue kwamba Ibilisi (Shetani au Roho ya Uasi) anahudhuria sana sana kanisani na huwa yupo makini sana ili asipoteze nafasi mpenyo kuvuruga kundi. Ibilisi haendagi bar au kwenye madisco kwani kule wapo wawakilishi wake na wanapiga kazi vizuri.
Naomba niishie hapo- Ubarikiwe sana.
Umeandika vizuri.
Kuna vipindi vya mafundisho ambavyo zamani watu walipata nafasi ya kuuliza na kujengwa.
Semina nyingi hawaachi nafasi ya mtu kuuliza ili aelewe ambavyo hakuelewa.

Hao wenye nia ovu nao ni wengi sana. Hawataki kutumia platform za kuuliza.
 
Yesu WA kwenye biblia alikua kizungumkuti mno👇

Yohana 14:8-9
Filipo akamwambia, Bwana, tuonyeshe Baba, na yatutosha. Yesu akamwambia, Je! nimekuwa pamoja nanyi siku hizi zote, nawe hujanijua, Filipo? Yeyote aliyeniona mimi amemwona Baba.
👇
Yohana 5:37
Naye Baba aliyenituma amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wowote, wala sura yake hamkuiona.
Alikuwa anamajibu ya kuvuruga mifumo tuliyojizoeza ili tupate mindset mpya za umilele.
 
Alikuwa anamajibu ya kuvuruga mifumo tuliyojizoeza ili tupate mindset mpya za umilele.
Si hivyo tuu; bali alichuchumalia kuondoa dhulma iliyojikita katika uendeshaji wa Mifumo halali iliyokuwepo iliyokubalika na Jamii, lakini wajanja wakawa wanajinufaisha kibinafsi ndani yake.e.g. Hekalu lilikuwa ni kwa ajili ya sala (Kihalali)lakini wajanja wakaligeuza ni mahali pa biashara (soko) kinyume na malengo ya kuwepo kwa hekalu hilo - Yesu aliwacharaza viboko wahusika na kupindua meza zao. Na kama hilo halikutosha wajanja hao hao wakajiwekea mfumo wa kulipa kodi lakini mumohumo kwenye kodi dhuluma (Fine)ikawepo ongezeko la riba(rejea Zakayo alivyokiri kwamba "kama nimemdhulumu mtu namrudishia...") ukichelewesha kodi; halafu rejea swali la mtego aliloulizwa Yesu kama ni halali kulipa kodi na jinsi Yesu alivyowafumba mdomo kwa jibu alilotoa (Mat.22:15- 46)
Alionesha kwa vitendo msamaha, upendo bila masharti e.g. Akiwa amewambwa juu ya msalaba na wahalifu wawili (ie. alichanganywa nao pale ili watu waone kwamba huyu nae ni miongoni mwa wahalifu) lakini akiwa katika hali hiyo aliweza kumwambia yule mwizi sugu aliyesulubiwa pamoja naye kwamba Hakika leo utakuwa pamoja nami.....Luka 23:42- 43 maana yake Yesu aliombwa na hakuweka longolongo eti karudishe vitu ulivyoiba au uliwaibia kina nani, mara ngapi na nini....
 
Si hivyo tuu; bali alichuchumalia kuondoa dhulma iliyojikita katika uendeshaji wa Mifumo halali iliyokuwepo iliyokubalika na Jamii, lakini wajanja wakawa wanajinufaisha kibinafsi ndani yake.e.g. Hekalu lilikuwa ni kwa ajili ya sala (Kihalali)lakini wajanja wakaligeuza ni mahali pa biashara (soko) kinyume na malengo ya kuwepo kwa hekalu hilo - Yesu aliwacharaza viboko wahusika na kupindua meza zao. Na kama hilo halikutosha wajanja hao hao wakajiwekea mfumo wa kulipa kodi lakini mumohumo kwenye kodi dhuluma (Fine)ikawepo ongezeko la riba(rejea Zakayo alivyokiri kwamba "kama nimemdhulumu mtu namrudishia...") ukichelewesha kodi; halafu rejea swali la mtego aliloulizwa Yesu kama ni halali kulipa kodi na jinsi Yesu alivyowafumba mdomo kwa jibu alilotoa (Mat.22:15- 46)
Alionesha kwa vitendo msamaha, upendo bila masharti e.g. Akiwa amewambwa juu ya msalaba na wahalifu wawili (ie. alichanganywa nao pale ili watu waone kwamba huyu nae ni miongoni mwa wahalifu) lakini akiwa katika hali hiyo aliweza kumwambia yule mwizi sugu aliyesulubiwa pamoja naye kwamba Hakika leo utakuwa pamoja nami.....Luka 23:42- 43 maana yake Yesu aliombwa na hakuweka longolongo eti karudishe vitu ulivyoiba au uliwaibia kina nani, mara ngapi na nini....
Amina sana.
 
Yesu WA kwenye biblia alikua kizungumkuti mno[emoji116]

Yohana 14:8-9
Filipo akamwambia, Bwana, tuonyeshe Baba, na yatutosha. Yesu akamwambia, Je! nimekuwa pamoja nanyi siku hizi zote, nawe hujanijua, Filipo? Yeyote aliyeniona mimi amemwona Baba.
[emoji116]
Yohana 5:37
Naye Baba aliyenituma amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wowote, wala sura yake hamkuiona.
Ndio ujifunze kutenganisha Kati ya Ubinadamu wa Yesu na Uungu wake kupitia kauli zake. Tofautisha anapojielezea kama binadamu na anapojielezea kama Mungu. Vinginevyo kichwa kitavurugika hicho[emoji1787]
 
Kuulizwa maswali.

Yesu alikuwa haogopi kuulizwa maswali. Hata kama ni ya kijinga atatafuta namna ya kukujibu ili uache huo ujinga.

Watu wengi wanaelewa kwa njia ya maswali. Nimeona wengi wanapenda kuongea mambo yao ila hawana ujasiri wa kuwaacha wanaowasikiliza wahoji na kuuliza maswali ili waelewe kwa kina.

Hii tabia imelekea kuwa na waumini wenye uelewa finyu na mashabiki wasio na ujasiri kwa wanayoyaamini.

Hii tabia imesababisha kuwa na watumishi majasiri kwenye mimbari ila waoga sana kwenye uhalisia wa maisha.

Tujifunze kwa Yesu.

Sabato njema.
[emoji120][emoji120]
 
Back
Top Bottom