Kitu gani cha ajabu ulichokifanya utotoni?

Kitu gani cha ajabu ulichokifanya utotoni?

Nsumbanzunya

Senior Member
Joined
Jun 13, 2014
Posts
177
Reaction score
42
Mi kwa upande wangu sikupenda kuvaa viatu kabisa na nilikuwa na rafiki yangu ye ilikuwa ni kupigana yaani ikipita wiki bila kupigana tutajiuliza kunani.vipi wewe hebu tupia .....
 
Mm nilikuw sipend kuimbiwa tena kufanyiwa sherehe ndo kabisaa niliwahi kimbia suprise ya birthday party
Watoto full kunikimbiza
 
mimi mda wote nilikuwa nacheza madangi tu(umama) ,nilikuwa najifanya mi ndo baba,wanaume wenzangu wote watoto,wengine walikuwa jogoo kazi yao ilikuwa kuwika, si unajua raha ya kuwa baba unaagiza tu akija mgeni mwambieni baba na mama wamelala ,mda wote nikula raha tu,jamani utoto raha.
 
mi bana nilikua nalia bila sababu dah! ikitokea nikakimbia ghafla nikaanguka kama uliniona na nikajua kwamba umeniona nikianguka basi ntalia kwa nguvu mtaa mzima wajue nimelia..
#kulia_kwa_kugalagala
 
Kimamaaaa watoto wa AR enz hizo wamenisoma,nlikuwa siog had niambiwe utaenda kazn kwa baba!au nitapelekwa kanisani
 
me wakati mdogo nilikua nachelewa kutoka shule coz nilikua tukiruhusiwa tu kurudi home natafuta viboko naanza kuchapa majani na miti njiani huku naisemesha km wanafunzi...kufika home late
 
Nimewahi choma nyumba. Kulikuwa na ndugu yetu tunaishi naye, aliniudhi hivyo nilichofanya ni kumlia timing ametoka, nilichukua baadhi ya nguo zake chumbani nikazipiga kibiriti, zilipopamba moto, nilizitupia hivyo hivyo chini ya uvungu na kusepa. Kurudi mida ya saa tisa, nyumba nyang'anyang'a, na baadhi ya vitu vimeungua. Ilikuwa balaa.
 
Sisi tulikuwa tukitoka shule tunatafuta kimpira kidogo au mbegu ya parachichi tunaenda tukicheza kupigana matobo had tunafika
 
nilikunya class

Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha!!!!! umenikumbusha mbali sana kwani nami ilikuwa ni kawaida yangu kuachia darasani hasa tunapotawanyishwa shuleni saa 6 mchana au saa 12 jioni. Umenigusa sana
 
Back
Top Bottom