Kitu gani kilikushangaza ulipofika Dar kwa mara ya kwanza.

Kitu gani kilikushangaza ulipofika Dar kwa mara ya kwanza.

Nilipofika Dar mara ya kwanza nilishangaa nipo na mwenyeji wangu kwenye kituo cha daladala hakuna gari hata moja ila kuna mpiga debe anaitia abiria "Segereaaaa, segereaaaa, segereaaaa"

Nilishangaa nikauliza nikaambia hao wanaitwa mateja.
 
First time kufika Dar stendi ilikuwa Kisutu enzi zile barabara ya kariakoo ilikuwa vumbi tupu mvua zikinyesha vumbi linageuka uji mwepesi. Tukatoka kisutu kuja kariakoo kwa mguu, eneo la msimbazi kilichonishangaza ni antena za televishen kwenye maghorofa zilikuwa nyingi kupitiliza, vimesimikwa vimlingoti kama 200 kwenye ghorofa moja. Baadae tukapanda chai maharage kwenda masaki.
Halafu bado mnasema serikali tukufu ya ccm haijafanya kitu kwa miaka yote tangu tupate uhuru.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
 
Back
Top Bottom