Kitu gani kilikushangaza ulipofika Dar kwa mara ya kwanza.

Sijafikaga uko dar ila nasikiaga jojo inaitwa bigji na express zinaitwa daladala,alafu nasikiaga maji ya ziwa la dar yanakuaga na machumvi mengi na masamaki wake ni kama manyoka fulani.
 
Nakumbuka nlipata shida sana kwenye tren, ndo ulikuwa usafiri pekee rahisi wa kuja dar, nlikuwa naogopa hata kutembea nikihofia nikitembea ama kuchungulia dirishani tren itaanguka.hasa ikikata kona ikalalia upande
 
Dah nyie acheni wakuu Dar ya zamani ilikuwa na hadhi kwa watu wa mkoa. Nilikuwa nikirudi watu wanataka niwasimlie stori za akina Maxi na Zembwela halafu na kiswahili changu cha Kidaslamu haha nilikuwa nawakalisha.
hahahaa kazi kweli kweli ...
 
Mimi vilinishangaza vingi sana lakini kikubwa zaidi kuliko vyote ni wanaume wa dar wachovu sana.....kuna jamaa alijikwaa kidgo tu wakati tunacheza Mpira.

Huwezi amini jamaa alilia kinoma kama mwanamke na mtaa mzima ukaongozana nae kumpeleka hospitali..... Tena walikodi taksi mbili.

Nilikwazika sana sio siri.....na lijamaa lipo comfortable kabisa yani
 
Kwakweli nilipofika maeneo ya mbezi ndo naingia dar nilishtuka kuona hali ya hewa imekuwa nzito na nilivozoea
Ikabidi nijikaze lakini nikasema.sitaishi dar hata iweje.
Kumbe yalikuwa mawazo ya kitoto now niko mjini hapa naenjoy though kuna changamoto kama za tracfic jam na joto ila nimezoea sasa
 
Siku ya kwanza watu wanapadis sana Dar lakini wakipazoea wanaita kwao MKOA
 
kukatisha ng'ambo ya Barbara ilikuwa mtihani na vile magari yalivyo mengi ilikuwa mtihani kwangu
 
Nilishangaa kuona watu wanakunywa maji kwenye mfuko almaarufu kama kandoro badaya ya kwenye chupa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…