Kitu gani ulikutana nacho au kukifanya kwenye Interview ukajua ushakosa Kazi

Kitu gani ulikutana nacho au kukifanya kwenye Interview ukajua ushakosa Kazi

Ulishawahi kuona yale Mazingira ya kushindwa jambo au kukosa fursa kabla hata hujaipata, basi kuna wakati unaweza kujikuta umefeli Interview hata kabla ya kupewa Majibu na Kampuni husika

Umeshawahi kupatwa na hali hii? Nini kilitokea?
Dah interview yangu ya kwanza kuingia oral na nikakandwa (TFS), nilijichanganya sana kwenye swali la explain about yourself.. ... sitakagi hata kukumbuka... Basi kutokana na kuwa nilikuwa sijui vizur namna ya kulijibu hili swali nikaanza pale kutaja jina langu freshi, sasa kwenye elimu sasa ndo nilipojichanganya nazani, nikaanza elimu yangu ni Chuo kikuu nimesoma Bachelor of nini nini hapo, ambapo safari hii ilianzia mwaka X darasa la kwanza na kumaliza mwaka X darasa la saba, baada ya hapo mwaka X nikajiunga na secondary mwaka X mpaka mwaka X , then nikajiunga Advance shule X mwaka X mpaka mwaka X , then baada ya hapo nikajiunga na Chuo mwaka X na kumaliza mwaka X ... yaan sikusema kuwa nina skills flan, na experience flan flan.. ni kama tu nilikuwa nawahadthia hadithi yangu na sio kama vile proffesional flan... Basi kazi ile siku ipata japokuwa nilipiga fresh written plus maswal mengine yote ya oral niliyajibu vizuri... baada ya kutoitwa kazini ndo nikajajua namna ilinibidi nilijibu swali hili ambalo huwa linaonekana simpo Kumbee sio.
 
kuponyokwa na ushuzi katikati ya interview ila uzuri nikapata ile kazi ila kila siku ikawa nikiongea tu nakumbushwa lile shuzi maana nilikuwa nimekula zangu samaki mmoja anapatikana Ukerewe anaitwa NGELE ni balaa shuzi lake halina tofauti na mnukanuka
 
Mwaka 2003 niiitwa interview ya taasisi ya kuzuia rushwa (PCB). Nikasafiri toka mkoani, kufika pale maswali mawili niliyoulizwa nikajua nimeyakosa pale pale ukiacha mengine niliyokuwa nikibahatisha bahatisha.
Swali la 1 lilikuwa niseme ni tukio gani kubwa lilitokea mwaka 1922 na likapelekea kubadilisha mustakabali mzima wa historia ya nchi yetu, nikajibu ni kuasisiwa kwa Tanganyika African Association (TAA) kumbe ilikuwa ni kuzaliwa kwa Mwl J. K. Nyerere
Swali la 2 ilitakiwa nieleze ugonjwa wa anthrax, nikajichanganya nikawaambia unatokana na mashambulizi ya mabomu huko mashariki ya kati.
Yaani alipo zaliwa JKN tuu mustakabali mzima wa nchi hii ukabadilika 😄 hii nchi kweli ngumu aisee
 
Kipindi fln niliwahi kufanya interview pale EATV kazi ya video editing, nlkuwa nna diploma in Tv and video production ila uzoefu sina tofauti na sasa hv nna experience.

Sasa kuna mdada yeye ndie HR pale ndio alikuwa ananifanyia interview, baada ya maswali kadhaa akauliza kwa sasa unafanya kazi gani? Nikamjibu kuwa niko mtaani nauza maandazi 😂 Dah yule mdada akajibu haya sawa kwaheri jinsi alivyojibu nikajua hapa tayari nmeyakanyaga.

Wanangu, experience ya ulichosomea ni muhimu mno n bora ukajitolee mahali kuliko kukaa mtaani tuu.

Nashukuru mwaka mmoja badae kupitia Taesa nilipata internship kwenye Tv flan kubwa sana hapa Tv na sasa hv mm n freelancer pale.
 
wakubwa sisi wa road huku acha tu unajua pikipiki hizi kubwa bwana za matairi manne ata wewe unaesoma apa unajua ila bwana interview wakaniwekea na mzigo kilichotokea bohora baada kuona nimewasha nikapiga moshi tatu paaap paaap paaap hahaha nikapewa location ya mzigo na kazi kabisa daah sitosahau
 
wakubwa sisi wa road huku acha tu unajua pikipiki hizi kubwa bwana za matairi manne ata wewe unaesoma apa unajua ila bwana interview wakaniwekea na mzigo kilichotokea bohora baada kuona nimewasha nikapiga moshi tatu paaap paaap paaap hahaha nikapewa location ya mzigo na kazi kabisa daah sitosahau
Hahah bohora akakupa kazi hahh, Moshi Tatu tu.
 
Kipindi hiko nimeenda kigoma town shirika flani
Nikaulizwa swali la kufikirishaa
kipindi nafikiria nkatazama chini
LA haula One of Interviewer amevaa soksi imetoboka matobo yamekaa kama
G o o g l e
Nikachekaaa
Dah, nimecheka sana Mkuu.

Nafikiri hata wangekuuliza unacheka nini bado usingeweza kuwajibu,
 
Back
Top Bottom