Kitu gani umewahi kuona ukaamini uchawi upo?

Kitu gani umewahi kuona ukaamini uchawi upo?

Mm nakushauri nenda google andika hiyo ndege iliyopotea usome habari yake then uje hapa,,
Alfu Kingine kama hutaki kuamini unasema ni Fiction,, hivi mtu anakwambia vita ya kwanz ilipigana wewe unaminije Kuwa hiyo vita ilikuwepo na wakat wewe hukuwepo isipokua tu unaisoma na wew unamini why usiseme hiyo ni habari, acha kuonyesha kwa jinsi gan kichwa chako hakifanyi kazi,, tarifa huwa zinarekodiwa kwa ajili ya kizaz na kizazi kama kumbukumb ya vizaz vijavyo basi kama hiyo huamini
Pole sanaa
ignore cause ignorance
kupuuza kunasababisha Ujinga.

Achana nae mjinga huyo.
 
Kwani unaamua ku reduce message yangu.
sikusema mafanikio yanahitaji commitment discipline and consistency kitu ambacho wengi hatupo radhi kufanya.
Most of us we can't embrace disruption I bet even you.

Yaani mpaka sasa hujathibitisha mtu aliyefanikiwa kwa uchawi ILA mimi nimekuonyesha mifano kibao.

Ukishafanya kazi hapo si uchawi tena kuna bidhaa ambayo inanunulika na watu.
au kama upo kazini kuna skills ambayo inahitajika hiyo sehemu na wewe unayo.
Mbona hivi vitu ni simple kuelewa

Embu ni convince kuna mtu kafanikiwa kwa uchawi ambaye sote tunamfahamu?

Au wewe unazungumzia luck? Na umesoma The richest man in babylon inasema nini kuhusu luck?

Usihangaike kunielewesha nahitaji uthibitisho wa mtu kafanikiwa sababu ya uchawi wake na si kufanya KAZI?
Nipo wilaya ya Mbarali ambapo shughuli kuu ni kilimo Cha mpunga. Ekari Moja ukiihudumia vzuri kabisa inaweza kukutolea gunia 25-28 za debe Tisa. Ila Kuna miamba inakutolea Hadi 40 ukizingatia kwamba kanuni za ulimaji ni zile zile hakuna mpya Yani unachofanya wewe na Mimi nafanya vilevile au kukuzidi kabisa.
Mara nyingi Hawa jamaa unakuta wanakuwa wa mwisho kutoa mazao Yao shambani, mtatoa woooote yeye anakuwa wa mwisho. Hii kitu sikuwahigi kuielewa but ukiwaza vizuri unaona kabisa kwamba Kuna namna nyuma ya pazia, nayo ni hallucination??

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
kuna watu wa kuitwa Wavidunda hao.... Morogoro hukooo... wanaishi juu milimani udzungwa... pembeni ya Bwawa la Umeme Kidatu! Jamaa walizuia Mradi wa Ujengaji wa Bwawa... mpk Nyerere akaingilia kati.... Mpk leo Jamaa wanashushwa kutoka Milimani kwa Magari ya TANESCO kila Alhamis kwenda Mnadani na Jioni wanarudishwa bureeee! Uchawi upo!
Nawajua wale si wanaishi kidodi pale, zamani wakati naenda ifoza likizo za primary nilikuwa nashangaa makaburi yapo sebleni. Yaani ukifungua mlango ule unaotazama road unashangaa kaburi holoo badala ya makochi aua viti.
 
Nipo wilaya ya Mbarali ambapo shughuli kuu ni kilimo Cha mpunga. Ekari Moja ukiihudumia vzuri kabisa inaweza kukutolea gunia 25-28 za debe Tisa. Ila Kuna miamba inakutolea Hadi 40 ukizingatia kwamba kanuni za ulimaji ni zile zile hakuna mpya Yani unachofanya wewe na Mimi nafanya vilevile au kukuzidi kabisa.
Mara nyingi Hawa jamaa unakuta wanakuwa wa mwisho kutoa mazao Yao shambani, mtatoa woooote yeye anakuwa wa mwisho. Hii kitu sikuwahigi kuielewa but ukiwaza vizuri unaona kabisa kwamba Kuna namna nyuma ya pazia, nayo ni hallucination??

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app

Umejielezea vzuri ILA umeniangusha kusema kuna namna nyuma ya pazia!

Ulipaswa uthibitishe namna nyuma ya pazia kwa kutupa positive link up na wao kupata mazao mengi zaidi ya wengine regardless wamefata kanuni Sawa.

Shida ninapowashinda ni mimi naelezea jinsi mtu anavyofanikiwa kwa kufanya kazi.

Siwezi kuelezea kilimo sina experience nayo

Njia rahisi ya wewe kuprove wrong nachoongea ni kunipa sababu shida mnaishia kusema nyuma ya pazia.
 
Inakuaje niko sahihi kwa kitu ambacho si cha kweli ikiwa uhalisia ni kwamba wewe gari unalo na si kwamba hauna gari kama ambavyo mimi navyosema?

Kanuni ni hii

"Everyone is innocent until proven guilty"
Thibitisha kuna mtu kafanikiwa kwa uchawi?
 
[emoji16][emoji16] hata mimi nilipokuwa kijana mdogo kama wewe, nilikuwa siamini kuhusiana na uchawi, nilikuwa silali hadi usiku wa manane, mda mwingine najificha nje labda kama ntaona kitu chochote, sijawahi kuona chochote, nilipotembea sasa huko duniani, nmekutana na mambo ambayo sikuyaona hapo kabla. Bado naendelea na uchunguzi kama ni uchawi au hallucination, japo kuna moja, unamwacha mtu nyumbani halafu unamkuta mbele ya safari, hii haikuwa hallucinations. Sidhani kama huo moyo wa kuwarekodi utaupata zaidi ya kufungulia turbo.
[emoji38]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nipe mfano.. halisi Sasa...hela zinapotea ndio. Uchawi umeingiaje Sasa? Kwani hela hazipotei? Zinapotea. So uchawi umetoka wapi.
Inaonyesha ndio mara ya kwanza hata kusikia kuhusu chuma ulete, hujui hata naongelea nini, ndio maana nasema mnapinga kitu ambacho hata hamkielewi.
 
Last born wetu aliumwa sana mika ile, yaani aliumwa sana. Mwisho mama akaamua aende kwa kaka yake Dar hapo sinza ili amuunganishe na jirani yake aende muhimbili. Bahati nzuri alimungqnisha na Dr mwingine aliyekuwa anafanya Tumaini hosp ile iliyokuwa karibu na diamond hall pale. Pale alichomwa sindano nyingi tuu na madawa kibao miezi mitatu mtoto akapona vizuri. Baadae wakafunga safari wakarudi home miye teena na kiherehere changu nikachukua wembe nikamnyoa nywele. Maana nywele zikuwa nyekunduku km mtu kapaka ina. Nilimnyolea nje basi upepo ulipokuwa unapuliza kwenye kile kiapara yakaanza kutoka pamba, pamba kabisa. Nilitoka nduki mpk ndani kwa Mama na Baba nikasema oneni mtoto anatoka pamba/sufi kichwani. Baba akasema hii hatari.Nilizikusanyq zile pamba nikasema akikua ntamuonyesha sasa ni mika 27 imepita na dogo yupo njema ni injinia huko Soudia anapiga kazi.
Pamba bado unazo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uchawi upo ndugu zangu.

Kuna rafiki yangu mmoja alikuwa anagombea kiwanja cha babu yake yeye na mjomba wake, dogo babu yake alimkatia eneo kubwa tu na akafanikiwa kujenga.

mjomba wake akajiapiza wewe dogo si babu yako anakupenda sana sasa utaona.

Hivi sasa dogo ni kichaa dah, yaani inasikitisha watu wameangaika sana kumtibu lakini wapi ukumuona utamuonea huruma.
Nicheki dm tumsaidie huyo ndg yako
 
Mwili hujitibu wenyewe, soma biology o level utanishkuru. unaweza usinywe dawa na upone. Kunywa maji mengi it's also a healing mechanism. Hamna uchawi hapa. Anything else?
Nimekuuliza unajua tiba ya kutumia maji tu ya kunywa? Badala ya kujibu unaanza kusema mara mwili unajitibu wenyewe mara hakuna uchawi, mbona unakuwa kama umewehuka?

Umewahi kusikia tiba kwa kutibu maradhi mbalimbali kwa kutumia maji tu ya kunywa?
 
Kanuni ni hii

"Everyone is innocent until proven guilty"
Thibitisha kuna mtu kafanikiwa kwa uchawi?
Kwahiyo hata wewe unayesema hakuna uchawi yawezakuwa uchawi upo kweli?

Ok wewe umeweza kuthibitisha mafanikio ya mtu kwa sababu ya kufanya kazi tu? Hebu tuweke uchawi pembeni, kuna watu tunawaona wanafanya kazi na wana maendeleo ila unawezakukuta nyuma ya pazia kuna ujambazi au rushwa na ukwepaji kulipa kodi. Je nikisema huyu mtu mafanikio yake ni huko kukwepa kulipa kodi nitakuwa nakosea?
 
Anayeamini uwepo wa Mungu na anayeamini uwepo wa uchawi WOTE wapo kundi moja la Metafizikia!
Unadhani bas wanakuelewa. Watu wamesoma kwenye GS haya mambo ila hawajui coz wanasomea vyeti. Mtu unasoma ufanye mtihani ufaulu ukitoka hapo hata mdogo wako kumsaidia huwezi...ndo shida ya watanzania. Afu mnalaumu elimu jau
 
Back
Top Bottom