Hiyo noma, sisi zamani ilikua ukipigwa tuu tobo wanawahi kwanza watu kama wawili hivi pale kwenye mt ili kuulinda usiende kugusu, hapo unaweza ukakimbizwa siku nzimaTobo bao ukipigwa tobo unakula makofi mpaka ukaguse mti
Zilikua nyeusi hiviKama huna kiwango kama watu hawatoshi we ndo unachaguliwa ila ujue hawachelewi kukufanya sub au unakaa kipa.
Kama we ni mwenye mpira na siyo mbabe kumaliza mechi unadaka mpira unatoka nduki kuelekea nyumbani.
Kama huna namba lazima unifanye rafiki wa mwenye mpira kinafki.
Wenye hasira ambao hawakupata nafasi mpira ukitoka badala ya kurudisha wanauongezea spidi uende mbali wachukue wenyewe.
Aisee kulikuwaga na raba za kike zinaitwa LOSSO zinakamba unafunga hadi juu ya henka,mi nilikuwa naiba za dada yangu naenda kupiga nazo mpira
Sent using Jamii Forums mobile app
Wazee wa dochi veleee 😂😂😂
Aisee wewe ni hatariBaada ya fainali ya world cup 2006.kesho yake nilipiga penati panenka kama ya zidane jana yake.huwa sisahau hili tukio.kuna babu alinizawadia 10000.
Unazingua boss uliwezajeBaada ya fainali ya world cup 2006.kesho yake nilipiga penati panenka kama ya zidane jana yake.huwa sisahau hili tukio.kuna babu alinizawadia 10000.
Baada ya kutoa kucha sana nikaachana na dochiHahaha! Mimi nilitoa kucha ya dole gumba la kulia kama mara tatu hivi hadi nakua.
Ilikuwa kawaida tu na sikuwahi kufanyia mazoezi.ile mikasi ya ronaldo alipokuwa man u !tumeipiga sana kitaa.pia mwaka 96 nikiwa kama na miaka 8 hivi niliwahi kufunga goli kama la paul gasgoine (gaza).kesho yake tu baada ya kutazama mechi ya uingereza na scotland.kiufupi tungekuwa na mfumo mzuri wa soka kama wenzetu huenda ningekuwa nimestaafu na kina drogba muda huu.na si mimi tu.tanzania kuna vipaji vingi vimepotea.nimewahi kuona wachezaji wazuri sana mtaani .sasa hivi mateja.wanywa gongo.huwa roho inaniumaga sana nikikutana nao .
[emoji23][emoji23][emoji23]Timu inayoanza kufungwa wanavua mashati