Kituko cha serikali ya CCM: Wanajenga Zahanati vijijini za kuombea kura si za kutatua changamoto za kiafya katika jamii

Kituko cha serikali ya CCM: Wanajenga Zahanati vijijini za kuombea kura si za kutatua changamoto za kiafya katika jamii

😂😂😂 mtu anaanzisha uzi kulalamikia ujenzi wa zahanati. Ndo hawa walipinga SGR sasa imeanza kaz wanaona aibu kupanda
hii dunia inashangaza sana ndrugu zango,

kwamba ni duara au mviringo, na ndiyo hayo sasa maajabu yake, dah! watu hawajui wanataka nini 🤣
 
hii dunia inashangaza sana ndrugu zango,

kwamba ni duara au mviringo, na ndiyo hayo sasa maajabu yake, dah! watu hawajui wanataka nini 🤣
hawa ndio wale majiran hawataki wote mfanikiwe ukinunua gari wanaanza kukuita freemanson yaani akili zao zimekaa kimaskini maskini tu
 
sasa unababaika na mpinga maendeleo gentleman?🐒

eti mtu anakasirika wananchi kujengewa zahanati ili kusudi wapate huduma za kiafi karibu na maeneo ya makazi yao, huo si ushirikina ndrugu zango 🤣

anachotaka ni nini sasa? kwamba zahanati isijengwe alaa? ujenzi wa mashule maabara na mabweni ya wanafunzi, mabarabara, mavituo ya afya, mazahanati na mahospitali, maviwanja ya ndege, maviwanja ya mpira n.k

ndio hasa siri ya kukubalika, kuaminika na ushindi wa kishindo wa CCM katika kila uchagizi 🐒
Siri halisi ya ushindi wa Fisiemu wanaijua bwana zenu kina Nape, Maafsa wa Polisi na Watendaji wa Serkali. Wewe na Luka ni vibaraka wapiga domo hamuwezi jua chochote sawa na Church goers tu hawajui chochote kuhusu Kanisa.
 
Nimepita Mwanza hivi karibuni nikaonyeshwa ile meli kubwa ya Mwanza HKT. Imekamilika kweli mbali na fittings ndogo ndogo zinazoendelea. Kituko cha karne, jengo la abiria bado yale yale mabati chakavu ya miaka nenda rudi, lakini mshangao zaidi gati la kupaki meli hiyo wakati wa kupakia abiria HALIPO.....Labda lijengwe fasta ili kuombea kura 😢
Hii yote ndio mipango inayopangwa kwenye ilani za chama kikongwe na wanasiasa wakongwe. 🤓
 
Nimepita Mwanza hivi karibuni nikaonyeshwa ile meli kubwa ya Mwanza HKT. Imekamilika kweli mbali na fittings ndogo ndogo zinazoendelea. Kituko cha karne, jengo la abiria bado yale yale mabati chakavu ya miaka nenda rudi, lakini mshangao zaidi gati la kupaki meli hiyo wakati wa kupakia abiria HALIPO.....Labda lijengwe fasta ili kuombea kura 😢
Hii yote ndio mipango inayopangwa kwenye ilani za chama kikongwe na wanasiasa wakongwe. 🤓
Nmenunua tv “55 nmeileta nyumban unataka nikuonyeshe na wall stand
 
Sasa karibu kila kijiji kina zahanani na kwenye kata kuna kituo cha afya.

Nadhani lengo la CCM ni kupata kura ili waendelee kutawala na si kutatua changamoto za wananchi ndani ya jamii.

Sasa zahanani ina watumishi wawili tu itaendeshwaje?

Kijijini kwetu huko ndani ya wiki moja lazima angalau siku 1 au zaidi zahanani ifungwe watumishi wako mjini kufuata dawa, kuhudhuria semina elekezi au kufuatilia majitaji yao ikiwa pamoja na mikopo.

Kuna kijiji zahanani ina mtumishi mmoja tu, awali walikuwa 3 mmoja kahama.

Huyu akiumwa na kwenda hospitali ya wilaya funguo za zahanani anamwachia mgambo.

Ndege moja kubwa ya abiria gharama yake ingeweza kuajiri na kuwalipa mshahara wauguzi, laboratory technician na madaktari kadhaa kwa muda wa mwaka mzima.

Ila serikali hii kipaumbele chake hakijulikani.

Leo hii am sure hata umuulize Waziri wa uchumi akuambie kuwa sasa kama nchi tuko kwenye sera gani hajui.

Muulize tuko kwenye Tanzania ya kilimo, Ufugaji, madini, Uvuvi, viwanda au biashara hajui .
Nadhani una matatizo mahala.

Safari ni hatua na Watumishi 2 ni haba lakini sio sawa na kukosa kabisa.
 
Nadhani una matatizo mahala.

Safari ni hatua na Watumishi 2 ni haba lakini sio sawa na kukosa kabisa.
Kwahiyo kwa huo utahira wako unaona ni sawa kijijini chenye wakaazi 10000 kuhudumiwa na muuguzi 1 na C/O mmoja huku pesa mnazipeleka kwenye ndege ambazo zingenunuliwa na kampuni binafsi?
Kwasababu ndege ya serikali na binafsi bei ya nauli sawa. Mkafukuza Fast jet mkaleta mindege yenu na kuongeza nauli.
Enzi za fast jet mpaka maskini walipanda ndege
 
Kwahiyo kwa huo utahira wako unaona ni sawa kijijini chenye wakaazi 10000 kuhudumiwa na muuguzi 1 na C/O mmoja huku pesa mnazipeleka kwenye ndege ambazo zingenunuliwa na kampuni binafsi?
Kwasababu ndege ya serikali na binafsi bei ya nauli sawa. Mkafukuza Fast jet mkaleta mindege yenu na kuongeza nauli.
Enzi za fast jet mpaka maskini walipanda ndege
Wewe Kwa akili zako unaona ni sawa kukosa kabisa hata mtumishi 1 ?
 
Nmenunua tv “55 nmeileta nyumban unataka nikuonyeshe na wall stand
Kama TV yako ina ulazima wa kuwa na wall stand na haina mbadala ni lazima ukiinunua uonyeshe na hiyo wall stand na sehemu utakayoiweka kwenye matumizi yake.
 
Kama TV yako ina ulazima wa kuwa na wall stand na haina mbadala ni lazima ukiinunua uonyeshe na hiyo wall stand na sehemu utakayoiweka kwenye matumizi yake.
“Mradi wa Utekelezaji wa ujenzi, upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Mwanza Kaskazini unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 18.6 na utachukua miezi 18 kukamilika kwake ambapo hadi sasa umefikia Asilimia 30%.”
Hii ni kipande cha report juu ya maboresho ya eneo hilo. Mkosoaji amejaribu kuandika aonekane amekosoa bila kufanya tafiti yoyote.(ujinga). Wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi swala halikua ujenzi wa meli pekee bali upanuzi wa bandari unaohusisha hayo yote aliyokosoa.🤝
 
Sasa karibu kila kijiji kina zahanani na kwenye kata kuna kituo cha afya.

Nadhani lengo la CCM ni kupata kura ili waendelee kutawala na si kutatua changamoto za wananchi ndani ya jamii.

Sasa zahanani ina watumishi wawili tu itaendeshwaje?

Kijijini kwetu huko ndani ya wiki moja lazima angalau siku 1 au zaidi zahanani ifungwe watumishi wako mjini kufuata dawa, kuhudhuria semina elekezi au kufuatilia majitaji yao ikiwa pamoja na mikopo.

Kuna kijiji zahanani ina mtumishi mmoja tu, awali walikuwa 3 mmoja kahama.

Huyu akiumwa na kwenda hospitali ya wilaya funguo za zahanani anamwachia mgambo.

Ndege moja kubwa ya abiria gharama yake ingeweza kuajiri na kuwalipa mshahara wauguzi, laboratory technician na madaktari kadhaa kwa muda wa mwaka mzima.

Ila serikali hii kipaumbele chake hakijulikani.

Leo hii am sure hata umuulize Waziri wa uchumi akuambie kuwa sasa kama nchi tuko kwenye sera gani hajui.

Muulize tuko kwenye Tanzania ya kilimo, Ufugaji, madini, Uvuvi, viwanda au biashara hajui .
Unajua kuhusu MMAM na MMES??
 
“Mradi wa Utekelezaji wa ujenzi, upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Mwanza Kaskazini unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 18.6 na utachukua miezi 18 kukamilika kwake ambapo hadi sasa umefikia Asilimia 30%.”
Hii ni kipande cha report juu ya maboresho ya eneo hilo. Mkosoaji amejaribu kuandika aonekane amekosoa bila kufanya tafiti yoyote.(ujinga). Wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi swala halikua ujenzi wa meli pekee bali upanuzi wa bandari unaohusisha hayo yote aliyokosoa.🤝
Hicho ndio kituko cha karne sasa, kama kulikuwa na ujenzi wa meli, upanuzi na uboreshaji wa bandari ya Mwanza, mjinga ni yupi? aliyejenga meli iliyokamilika kitambo wakati bandari iko kwenye asilimia 30 au huyo aliyekosoa? 😳
 
Back
Top Bottom