Uchaguzi 2020 Kituko: Tundu Lissu na CHADEMA wanaamini mkoloni angetoa ''haki'' waafrika wasiongemkataa

Uchaguzi 2020 Kituko: Tundu Lissu na CHADEMA wanaamini mkoloni angetoa ''haki'' waafrika wasiongemkataa

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2016
Posts
17,506
Reaction score
16,003
Ndugu zangu,

Nikiwa katikati ya shughuli zangu nimesikia kituko toka kwa Lissu na wafuasi wa CHADEMA eti..''pamoja na maendeleo aliyoleta mjerumani alikataliwa na waafrika sababu hakutenda haki'' kwa lugha rahisi ni kuwa mjerumani angetenda hiyo ''haki'' Lissu na wenzake wangefurahia tu angebaki kutawala.

Sijashangaa kwani hata CHADEMA wenyewe wanaamini ni bora leo Robert Amsterdam awe rais wa Tanzania sababu atawapa ''haki'' kuliko Rais Magufuli kwani hatawapa ''haki'' hata kama ataboresha miundombinu. Hii ni akili yenye kukumbatia ukoloni mambo leo na kuhusudu utumwa. Eti waafrika tusijitawale kisa mzungu anatenda ''haki'', duh!

Nimalize tu kwa kusema Tanzania ni ya watanzania haitatawaliwa na mtumwa wa wakoloni wala aliyewatuma.

Embu fikiria kama watu aina ya Lissu wangekuwepo kipindi cha kudai uhuru halafu mzungu akawapa ''haki'' tungekuwa huru??
 
Wewe ni Nani Hadi uisemee Tanzania na watanzania milioni 56+ wanaojitambua na kujielewa? Au unadhani Tanzania ni familia yako?

Hebu niondolee uzalendo uchwara hapa kwani huijui Tanzania ilikotoka na inakotaka kwenda!
 
Sasa mkoloni mweusi aibu na haya hana hata hela ya rambirambi analamba. Mkoloni mweusi anaiba Trillion 1.5 bila huruma na hicho kiasi kimewekwa wazi inaaminika jamaa kalamba Zaid ya trilioni 10. Bora mkoloni mweupe
 
Kasome history upya.mandela alifungwa kwa sababu gani.nyerere na wenzake walipigania nini,maumau,majimaji war etc.Lissu is right madam
 
Lissu na Chadema wanapigania uhuru na haki sawa kwa wote , kuthamini utu wa mtu,uchaguzi huru.Ndio sababu umati mkubwa unawafuata bila kuwa na vikundi vya wasanii.

Pammoja Magufuli kufanya miradi mikubwa ya kitaifa kwa muda mfupi lakini kukosekana uhuru wa vyama vya upinzani kufanya siasa imeitia dosari serikali yake.
Magufuli bado ana nafasi ya kujirekebisha na kuongezewa miaka mingine mingine,akipunguza siasa za kibabe.
Yawezekana waliomzunguka wanamwogopa sana,na hilo ndio tatizo.
 
Kipimo hicho Cha uzalendo,Sina hakika Kama ni uzalendo usio halisi ama ni Uzalendo halisi
 
Afrika Kusini ilikuwa nchi huru[wengine wanaita wa bandia] wakati Mzee Mandela na wenzake wako gerezani.

Kilichokuwa kinapiganiwa pale ni HAKI kwamba mfumo wa utawala uliokuwepo ulikuwa hautoi haki sawa kwa raia wote wa Afrika Kusini.

Zanzibar ilipata uhuru toka kwa Muingereza tarehe 10 Disemba 1963 lakini kulikuwa na figisu-figisu wakati wa uchaguzi na masuala ya ubaguzi na hivyo kusababisha mapinduzi ya tarehe 12 January 1964.

Tatizo la wana-CCM ni kutokusoma. Hili ni tatizo la Mwenyekiti wao, mpaka huku ngazi za chini na hawa watetezi wa chama kwenye mitandao.
 
Kwenye ukweli usemwe,,maana ukweli utatuweka huru,,,,,,,,,,,,,,,,,,,Hakuna watu wabaya kuliko mabeberu kama viongozi hawa wa Afrika,,,,Tusipende kuweka visingizio vya ubeberu katika udhaifu wa viongozi wetu,,,,, Hivi beberu ndiye kaharibu soko la zao la korosho,,hivi beberu ndiye kaharibu soko la mbaazi,,,,,hivi beberu ndiye kashindwa kufanya uwekezaji kwenye kilimo, kwa miaka 50 ,badala yake amesema mjenge Reli kwenda Mwanza ,, badala ya kuelekea Mbeya ,,Zambia na Congo ya,,Lubumbashi Kwenye mizigo mingi kuliko huko Congo ya kisangani?

Hivi huyo beberu ndiye anayefanya mpigine risasi kwa sababu tu ya hoja za Demokrasia na Haki za binadamu,, Ndugu yangu,,..Duniani nchi nyingi zimesonga mbele sana Kimaendeleo mbele ya huyo unayemwita beberu/Ubeberu,,,,,,South Korea, Malaysia, Singapore, Hong-kong, Taiwan, Thailand, China, India, Vietnam, UAE

Tatizo letu ni viongozi wanaojifanya Miungu watu kwa sababu tu ya kuwa Maraisi wa nchi,,,,,Hawataki demokrasia ya kweli, hawataki haki za binadamu zitamalaki, wabinafsi, wachoyo, wana roho mbaya,,,,,,,,na Makatili,,,,Nchi haiongozwi kwa majaribio,,,,
Hivi kuna shida gani kwa kiongozi kuruhusu uhuru wa kidemokrasia katika kuchagua viongozi ndani ya nchi yake,,na kama watu wanampenda na kuamini ayafanyayo si watampa nafasi tena,,,kwanini wanataka kung'ang'ania madarakani wakati tunawaona hakuna cha maana wanachoweza kufanya ili kulivusha taifa kwenye maendeleo makubwa ya kama Singapore?

Hivi kweli unataka kutuambia kwamba huo ubeberu ndiyo uliofanya Gadafi afiche zaidi ya Tillioni 80 Ulaya na Marekani
Hivi kweli ni huo ubeberu Uliofanya Gadafi akaifanya Libya kama nchi aliyorithi kutoka kwa wazazi wake, na kuwafanya wananchi wake kama wanyama/Watumwa? Au wewe kwa uelewa wako nchi ni mali ya nani
Tatizo la Congo ni wakongo wenyewe,,,,

Tunaweza kutoboa,, na kufanikisha taifa kuwa la maendeleo na haki,,,cha muhimu tusiabudu viongozi, kwa sababu viongozi hawawi malaika kwa kupata uongozi,,,ni binadamu wale wale kama sisi na wanamapungufu makubwa kama tuliyonayo, sisi(concept of check and balance comes in because of our human weakness) ,ndio maana watu lazima wawakosoe viongozi wao,,,Demokrasia ya kweli ikiruhusiwa itakuwa neema kwa taifa na kwa maendeleo ya nchi yetu,,,,,Ubeberu si mbaya ukifananisha na viongozi wa Afrika,,
Demokrasia ya kweli, haki za binadamu, uongozi wa sheria zilizo bora, uimara wa mihimili ya serikali katika kucheck na kubalance, Mfumo wa Utawala wa Westiminister (Parliamentary Government),

Vyama imara vya upinzani vyenye uwezo wa kucheck na kubalance ndio tunu pekee za kuipeleka Afrika dunia ya kwanza mahali bora katika miaka michache ijayo (Kwa hili Ghana inaonyesha njia chini ya Raisi Mwanasheria /Wakili Akufo Nana ADDO, Otherwise mtaendelea kumtafuta mchawi wa maendeleo ya Afrika,,,mtamsingizia Beberu, mtasingizia laana, mtasingizia resorce Curse (laana ya mali nyingi) Mtasingizia udikteta, Mtasingizia hali ya hewa, mtasingizia Word Bank na IMF,, mtasingizia Mchina,,,na viongozi wenu watakuwa hawawajibiki kwa kisingizio cha huyo huyo beberu,,, viongozi wenu watakuwa wanaiba mali zenu na kuzipeleka Ulaya,, mkiuliza kwanini hampigi hatua ,,watasingizia huyo huyo beberu,,,,,,kazi kwenu,,,,,,hata Mwalimu Nyerere kiongozi wenu aliposema ili tuendelee,,hakusema tupambane na beberu,,,, na kwamba kama yupo hatuwezi kuendelea. Tanzania siyo kisiwa,,itashirikiana na wenzake ili kupiga hatua za kimaendeleo,,,hata wakati wa utawala wa Kilwa empire,,ilishirikana na mataifa mengine na kupiga hatua kubwa,,,,Akili mukichwa nimemaliza....Mungu akusaidie,,akupe maarifa,,na aendelee kukufunua ubongo ili uijue kweli,,na kweli ikuweke huru.
 
Bora ya mkoloni kuliko ccm,alileta ajira tele mashambani na viwandani,elimu Bora,afya Bora,kosa lake kuwanyima haki watz.
 
Kwani ukoloni ulikomeshwa kwasababu gani? Haki sio kwasababu ya rangi au maendeleo. Nenda kasome vitabu vya Nyerere.
Kwasababu waafrika walitaka kujitawala wakaproof failure hawawezi kujitawala
 
Ndugu zangu,

Nikiwa katikati ya shughuli zangu nimesikia kituko toka kwa Lissu na wafuasi wa CHADEMA eti..''pamoja na maendeleo aliyoleta mjerumani alikataliwa na waafrika sababu hakutenda haki'' kwa lugha rahisi ni kuwa mjerumani angetenda hiyo ''haki'' Lissu na wenzake wangefurahia tu angebaki kutawala.

Sijashangaa kwani hata CHADEMA wenyewe wanaamini ni bora leo Robert Amsterdam awe rais wa Tanzania sababu atawapa ''haki'' kuliko Rais Magufuli kwani hatawapa ''haki'' hata kama ataboresha miundombinu. Hii ni akili yenye kukumbatia ukoloni mambo leo na kuhusudu utumwa. Eti waafrika tusijitawale kisa mzungu anatenda ''haki'', duh!

Nimalize tu kwa kusema Tanzania ni ya watanzania haitatawaliwa na mtumwa wa wakoloni wala aliyewatuma.

Embu fikiria kama watu aina ya Lissu wangekuwepo kipindi cha kudai uhuru halafu mzungu akawapa ''haki'' tungekuwa huru??
Nimeshangaa sana chama kama Chadema hakina wanasiasa wanaojua nini maana ya uhuru. Nini maana ya sovreignty. Na kwa mantiki hiyo wanaona wawe huru kutukana majukwaani lakini wasiwe na uhuru wa kujitawala.
 
Sasa mkoloni mweusi aibu na haya hana hata hela ya rambirambi analamba. Mkoloni mweusi anaiba Trillion 1.5 bila huruma na hicho kiasi kimewekwa wazi inaaminika jamaa kalamba Zaid ya trilioni 10. Bora mkoloni mweupe
Zilizotumika bukoba hazilingani na jumla ya pesa za maafa zilizochangwa, bukoba wanasubiria chenji zao wajenge nyumba za kisasa
 
Back
Top Bottom