Kituo hicho kimeanzishwa kwa pamoja na kampuni ya Unicom ya Hunan na Shirika la kuhimiza ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya China na Afrika la mkoa wa Hunan, na kinalenga kutoa huduma za dijitali na TEHAMA kwa kampuni za China barani Afrika, ili kuchangia maendeleo yenye ubora ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya pande hizo mbili.