RIGHT MARKER
Senior Member
- Apr 30, 2018
- 129
- 473
📖Mhadhara (71)✍️
Mbeya ni mkoa ambao unakabiriwa na matukio ya ajali za mara kwa mara. Maeneo ambayo ajali hutokea sana ni;
1. Mlima nyoka,
2. Mteremko wa Simike (Nzovwe), na
3. Mlima wa Mbalizi.
Licha ya ajali nyingi kutokea katika maeneo hayo hasa Mteremko wa Simike (Nzovwe), lakini mabus madogo (Coaster) yanayobeba abiria wa kutoka Mbeya mjini kwenda Tunduma na Ileje yanasimama kwa muda mrefu sana kwenye kituo kidogo (parking) cha Simike huku yakisubiri abiria. Kituo kidogo cha Simike kimekuwa ni stendi kuu ya mabus madogo (coaster) hali inayohatarisha usalama wa abiria.
Ifahamike kuwa eneo lile (Simike) ni eneo la kushusha na kuchukua abiria kisha kuondoka, na wala si eneo la kusubiria abiria kwa muda mrefu, lakini Coaster zinasimama Simike zaidi ya dakika 15. Wapiga debe wa eneo lile (Simike) wamechapisha mpaka T-shirts zao zisomekazo "Maafisa usafirishaji" kudhihirisha kuwa pale ni stendi ya mabus kama stendi nyingine. Wakati mwingine unakuta coaster imesimama vibaya yaani eneo la nyuma lote lipo barabarani mpaka malori yanapiga honi ya kumtaka dereva wa coaster asimamishe vizuri, ni hatari sana.
Mbali na kero hiyo ya kuhatarisha usalama wa abiria, kero nyingine ni wapiga debe wa eneo lile (Simike) ni wababe sana kwa abiria. Naomba mamlaka husika zote zitazame kero hizi kwa jicho la kumi ili kuepusha ajali za mara kwa mara zinazotokea katika Mkoa wa Mbeya.
RIGHT MARKER,
DAR ES SALAAM.
👁️Utalii wa JIJINI MBEYA.
Mbeya ni mkoa ambao unakabiriwa na matukio ya ajali za mara kwa mara. Maeneo ambayo ajali hutokea sana ni;
1. Mlima nyoka,
2. Mteremko wa Simike (Nzovwe), na
3. Mlima wa Mbalizi.
Licha ya ajali nyingi kutokea katika maeneo hayo hasa Mteremko wa Simike (Nzovwe), lakini mabus madogo (Coaster) yanayobeba abiria wa kutoka Mbeya mjini kwenda Tunduma na Ileje yanasimama kwa muda mrefu sana kwenye kituo kidogo (parking) cha Simike huku yakisubiri abiria. Kituo kidogo cha Simike kimekuwa ni stendi kuu ya mabus madogo (coaster) hali inayohatarisha usalama wa abiria.
Ifahamike kuwa eneo lile (Simike) ni eneo la kushusha na kuchukua abiria kisha kuondoka, na wala si eneo la kusubiria abiria kwa muda mrefu, lakini Coaster zinasimama Simike zaidi ya dakika 15. Wapiga debe wa eneo lile (Simike) wamechapisha mpaka T-shirts zao zisomekazo "Maafisa usafirishaji" kudhihirisha kuwa pale ni stendi ya mabus kama stendi nyingine. Wakati mwingine unakuta coaster imesimama vibaya yaani eneo la nyuma lote lipo barabarani mpaka malori yanapiga honi ya kumtaka dereva wa coaster asimamishe vizuri, ni hatari sana.
Mbali na kero hiyo ya kuhatarisha usalama wa abiria, kero nyingine ni wapiga debe wa eneo lile (Simike) ni wababe sana kwa abiria. Naomba mamlaka husika zote zitazame kero hizi kwa jicho la kumi ili kuepusha ajali za mara kwa mara zinazotokea katika Mkoa wa Mbeya.
RIGHT MARKER,
DAR ES SALAAM.
👁️Utalii wa JIJINI MBEYA.