Kituo kipya cha mabasi Dar kuanza kutumika Desemba 20

Kituo kipya cha mabasi Dar kuanza kutumika Desemba 20

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhandisi Joseph Nyamhanga, amewataka viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhakikisha Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani cha Mbezi Luis, kuanza kutumika ifikapo Desemba 20, 2020.

Ametoa maagizo hayo leo Desemba 7, 2020, alipotembelea mradi huo kuangalia maendeleo yake ambao kwa sasa umefikia asilimia 92-95, akieleza kuwa kazi ndogondogo zilizosalia zimalizike katika kipindi hiki kifupi ili kituo hicho kianze kutumika.

“Kituo kikuu cha mabasi kipya cha Mbezi Luis kiwe tayari kimeanza kufanya kazi, hatua ambayo itapunguza msongamano katika kituo cha Ubungo hususani katika kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka,”amesema.

Akitoa taarifa fupi ya maendeleo ya mradi huo, meneja mradi huo, Dkt. Godwin Maro, amesema ujenzi umefikia katika hatua za mwisho na kinaweza kuanza kutumika muda wowote ingawa changamoto ni barabara inayotakiwa kuingiza magari kituoni hapo ambayo kwa mujibu wa meneja wa Tanroads Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Ngassa Julius, itakamilika kabla ya Desemba 20 kama ilivyoagizwa ili kituo kianze kutumika rasmi.
 
Sijui sisi wa gongo la mboto daladala zitakuwepo za kutupeleka kwetu, nama tulizoea ubungo unasogea tu pale sogas unadandia daladala


Kutakuwa na dala dala za makampuni mfano shabiby kutoka dom akifika mbezi louis anashusha abiria afu wanaingia kwny dala dala ya shabiby then wanapelekwa mpaka gomz mbagala temeke n.k

Hii ishu inafanyika pia Tanga maana stand kuu iko nje sana ya mji.
 
Sijui sisi wa gongo la mboto daladala zitakuwepo za kutupeleka kwetu, nama tulizoea ubungo unasogea tu pale sogas unadandia daladala
Mbona sikuzote daladala zipo zakutoka G/mboto mpaka Mbezi Via M/mawili fare 600tu...so Hilo halinashaka mkuu Kwanza itakua kwasisi wa Goms imeturahisishia Sana tu maana hakuna Tena kero za mafoleni mkuu...!
 
Kutakuwa na dala dala za makampuni mfano shabiby kutoka dom akifika mbezi louis anashusha abiria afu wanaingia kwny dala dala ya shabiby then wanapelekwa mpaka gomz mbagala temeke n.k

Hii ishu inafanyika pia Tanga maana stand kuu iko nje sana ya mji.
Ikiwa hivi basi ni vizuri
 
Kutakuwa na dala dala za makampuni mfano shabiby kutoka dom akifika mbezi louis anashusha abiria afu wanaingia kwny dala dala ya shabiby then wanapelekwa mpaka gomz mbagala temeke n.k

Hii ishu inafanyika pia Tanga maana stand kuu iko nje sana ya mji.

True niliona tanga huu utaratibu
 
Kama naiona vile foleni katika barabara ya kuelekea Gongo la Mboto kupitia Kinyerezi itakavyokuwa pasua kichwa.
 
Sijui sisi wa gongo la mboto daladala zitakuwepo za kutupeleka kwetu, nama tulizoea ubungo unasogea tu pale sogas unadandia daladala
Mbona sikuzote daladala zipo zakutoka G/mboto mpaka Mbezi Via M/mawili fare 600tu...so Hilo halinashaka mkuu Kwanza itakua kwasisi wa Goms imeturahisishia Sana tu maana hakuna Tena kero za mafoleni mkuu...!
Zinakopak daladala Kuna umbali toka terminal
 
Sijui sisi wa gongo la mboto daladala zitakuwepo za kutupeleka kwetu, nama tulizoea ubungo unasogea tu pale sogas unadandia daladala
sio gomz tu kuna mbagala kigamboni na maeneo yote kwakwele inabidi watazame raia wanafikae huko kuwai usafiri wa saa 12 asubuhi

pia ukishuka saa 2 usiku unafijaje home
 
Kutakuwa na dala dala za makampuni mfano shabiby kutoka dom akifika mbezi louis anashusha abiria afu wanaingia kwny dala dala ya shabiby then wanapelekwa mpaka gomz mbagala temeke n.k

Hii ishu inafanyika pia Tanga maana stand kuu iko nje sana ya mji.
acha uongo, tanga yenyewe wanaofanya hivyo ni tashreef tu nao pia wanapigwa vita na watu wa daladala sana
 
Back
Top Bottom