Kitwana Selemani Kondo na Rais Benjamin William Mkapa Diamond Jubilee hall 2004

Kitwana Selemani Kondo na Rais Benjamin William Mkapa Diamond Jubilee hall 2004

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074


Katika mkusanyiko huu wa Waislam chini ya Muslim Development Fund (MDF) Mwenyekiti wake akiwa Mzee Kondo, Mzee Kitwana Kondo alisema kuwa nia ya MDF ni kuwa na Chuo Kikuu na kujenga shule nchi nzima.

Maneno haya Mzee Kondo anawaambia Waislam na Rais Mkapa mwaka wa 2004.

Ikiwa huijui historia ya Waislam katika kutafuta elimu maneno ya Mzee Kondo kwako ni kama vile Waislam ndiyo kwanza wametupa shuka chini wanaamka usingizini kitandani wanataka na wao sasa wajenge shule na Chuo Kikuu.

Haikuwa hivyo.

Ukweli ni kuwa Waislam walianza kujenga shule zao toka ukoloni.

Ukweli ni kuwa baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961 Waislam waliitisha Muslim Congress mwaka wa 1962 kujadili na kupanga upya mipango ya ujenzi wa shule na mwaka wa 1968 Waislam waliweka jiwe la msingi wa Chuo Kikuu.

Jiwe hili liliwekwa na Rais wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akishuhudiwa na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Tewa Said Tewa Rais wa EAMWS upande wa Tanganyika.

Wakati huo mwaka wa 1968 Rais Benjamin William Mkapa alikuwa Mhariri Mkuu wa magazeti ya TANU - The Nationalist na Uhuru.

Kitwana Kondo siku ile pale ukumbini anamueleza Rais Mkapa historia ambayo yeye Rais Mkapa si mgeni nayo kwani habari ya Waislam kujenga Chuo Kikuu ilikuwa habari kubwa mno na anaijua vyema kwani na ilichapwa na magazeti yake.

Si hilo tu magazeti haya ambayo yeye alikuwa Mhariri Mkuu yalikuwa mstari wa mbele kuandika mgogoro wa EAMWS uliosababisha EAMWS kuvunjwa na serikali na kuundwa BAKWATA.

Nilikuwa mmoja wa Waislam waliokuwa ndani ya ukumbi ule siku hii Rais Mkapa alipowapa Waislam majengo ya TANESCO Morogoro ili yawe Chuo Kikuu Cha Waislam.

Laiti EAMWS isingepigwa marufuku na serikali Waislam wangekuwa na Chuo Kikuu toka mwaka wa 1968.

Kuvunjwa kwa EAMWS na kuundwa BAKWATA ndiyo mwisho wa juhudi za Waislam kujenga shule na Chuo Kikuu walichokusudia.

Historia ya Waislam wa Tanzania katika juhudi ya kutafuta elimu ni ndefu na imejaa misukosuko mingi.

Hotuba hii ya Mzee Kondo imenikumbusha maneno ya Mufti Sheikh Hassan bin Ameir alipowaambia Waislam mara tu baada ya kupata uhuru kuwa, "Waislam tumeupigania uhuru hadi umepatikana sasa tujenge shule tujielimishe tutawale nchi pamoja na wenzetu."
 
Waislam tumeupigania uhuru hadi umepatikana sasa tujenge shule tujielimishe tutawale nchi pamoja na wenzetu."
Na Nyerere angesema "huu uhuru umepatikana kwa juhudi zangu mimi mzanaki" ingekuwaje hiyo mzee...

Hakuna kitu kibaya kama kupambania jambo na watu wanaojitazama kimakundi ya kikabila au kidini.
 
Mzee Mohamed Said najua wewe ni mpenzi wa mpira wa miguu Kwa kiasi chake na pia ni mpenzi wa mojawapo ya hizi timu za Kariakoo na najua timu unayoshabikia 😀😀.

Kwa miaka mingi kumekuwa na historia ikisemwasemwa timu fulani ilishiriki kuleta Uhuru na timu nyingine ya pale Kariakoo haikushiriki kwenye Uhuru. Binafsi naamini hili suala linahitaji kuwekewa sawa na historia sahihi kuandikwa.

Basi ukipata muda walau tuandikie makala fupi ya Ushiriki wa hizi timu katika mapigano ya Uhuru, ama Mchango wa waliokuwa Wanachama wa hivi vilabu katika mapigano ya Uhuru wa Tanganyika ikiwemo ufadhili katika TAA na baadaye TANU ili tuone hicho kinachosemwa na ukweli wake.

Asante tena Kwa jitihada zako za kutupa Elimu ya mambo mengi ambayo pengine hayapo katika Vitabu vyetu.
 
Mzee Mohamed Said najua wewe ni mpenzi wa mpira wa miguu Kwa kiasi chake na pia ni mpenzi wa mojawapo ya hizi timu za Kariakoo na najua timu unayoshabikia 😀😀.

Kwa miaka mingi kumekuwa na historia ikisemwasemwa timu fulani ilishiriki kuleta Uhuru na timu nyingine ya pale Kariakoo haikushiriki kwenye Uhuru. Binafsi naamini hili suala linahitaji kuwekewa sawa na historia sahihi kuandikwa.

Basi ukipata muda walau tuandikie makala fupi ya Ushiriki wa hizi timu katika mapigano ya Uhuru, ama Mchango wa waliokuwa Wanachama wa hivi vilabu katika mapigano ya Uhuru wa Tanganyika ikiwemo ufadhili katika TAA na baadaye TANU ili tuone hicho kinachosemwa na ukweli wake.

Asante tena Kwa jitihada zako za kutupa Elimu ya mambo mengi ambayo pengine hayapo katika Vitabu vyetu.
Huyu mzee ni Kolo mwenzio hawezi kusema ukweli.Yanga ilikuwa bega kwa bega na AA na baadaye TAA na kwa Zanzibar,African Assoiation na baadaye TANU .Nasaba hii haijesha hadi kuna watu leo huihusisha na CCM ingawa maendeleo hayana chama.
 
Huyu mzee ni Kolo mwenzio hawezi kusema ukweli.Yanga ilikuwa bega kwa bega na AA na baadaye TAA na kwa Zanzibar,African Assoiation na baadaye TANU .Nasaba hii haijesha hadi kuna watu leo huihusisha na CCM ingawa maendeleo hayana chama.
😀😀😀😀 Hayo wayasema wewe. Mie nasubiria afungue Uzi maalumu wa mapambano ya Uhuru na Ushirikinwa Vilabu vyetu.

Hapa ngoja tuendelee kudurusu kuhusu Chuo Kikuu Cha Waislamu Morogoro na MDF , sijui walifunhua Sekondari ngapi kama kama walivyodhamiria 😃😃
 
Mzee Mohamed Said najua wewe ni mpenzi wa mpira wa miguu Kwa kiasi chake na pia ni mpenzi wa mojawapo ya hizi timu za Kariakoo na najua timu unayoshabikia 😀😀.

Kwa miaka mingi kumekuwa na historia ikisemwasemwa timu fulani ilishiriki kuleta Uhuru na timu nyingine ya pale Kariakoo haikushiriki kwenye Uhuru. Binafsi naamini hili suala linahitaji kuwekewa sawa na historia sahihi kuandikwa.

Basi ukipata muda walau tuandikie makala fupi ya Ushiriki wa hizi timu katika mapigano ya Uhuru, ama Mchango wa waliokuwa Wanachama wa hivi vilabu katika mapigano ya Uhuru wa Tanganyika ikiwemo ufadhili katika TAA na baadaye TANU ili tuone hicho kinachosemwa na ukweli wake.

Asante tena Kwa jitihada zako za kutupa Elimu ya mambo mengi ambayo pengine hayapo katika Vitabu vyetu.
Chama...
Katika kitabu cha Abdul Sykes nimeeleza historia hiyo.

Tuvute subira In Shaa Allah nitaeleza.
 
Mzee Said haoni hata aibu kuandika haya. Yaani waislamu waliotaka kujenga chuo, wakaishia kupewa chuo cha umma (chuo cha Tanesco) buree na leo ni zaidi ya miaka 20 chuo chenyewe kimedumaa na kuwa na utoaji wa elimu duni huenda kuliko chuo kikuu chochote hapa Tanzania.
Uislamu na elimu dunia wapi na wapi?

Poor mzee wangu Said.
 
Na Nyerere angesema "huu uhuru umepatikana kwa juhudi zangu mimi mzanaki" ingekuwaje hiyo mzee...

Hakuna kitu kibaya kama kupambania jambo na watu wanaojitazama kimakundi ya kikabila au kidini.
vipi maendeleo kuletwa na chama cha kijani
 


Katika mkusanyiko huu wa Waislam chini ya Muslim Development Fund (MDF) Mwenyekiti wake akiwa Mzee Kondo, Mzee Kitwana Kondo alisema kuwa nia ya MDF ni kuwa na Chuo Kikuu na kujenga shule nchi nzima.

Maneno haya Mzee Kondo anawaambia Waislam na Rais Mkapa mwaka wa 2004.

Ikiwa huijui historia ya Waislam katika kutafuta elimu maneno ya Mzee Kondo kwako ni kama vile Waislam ndiyo kwanza wametupa shuka chini wanaamka usingizini kitandani wanataka na wao sasa wajenge shule na Chuo Kikuu.

Haikuwa hivyo.

Ukweli ni kuwa Waislam walianza kujenga shule zao toka ukoloni.

Ukweli ni kuwa baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961 Waislam waliitisha Muslim Congress mwaka wa 1962 kujadili na kupanga upya mipango ya ujenzi wa shule na mwaka wa 1968 Waislam waliweka jiwe la msingi wa Chuo Kikuu.

Jiwe hili liliwekwa na Rais wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akishuhudiwa na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Tewa Said Tewa Rais wa EAMWS upande wa Tanganyika.

Wakati huo mwaka wa 1968 Rais Benjamin William Mkapa alikuwa Mhariri Mkuu wa magazeti ya TANU - The Nationalist na Uhuru.

Kitwana Kondo siku ile pale ukumbini anamueleza Rais Mkapa historia ambayo yeye Rais Mkapa si mgeni nayo kwani habari ya Waislam kujenga Chuo Kikuu ilikuwa habari kubwa mno na anaijua vyema kwani na ilichapwa na magazeti yake.

Si hilo tu magazeti haya ambayo yeye alikuwa Mhariri Mkuu yalikuwa mstari wa mbele kuandika mgogoro wa EAMWS uliosababisha EAMWS kuvunjwa na serikali na kuundwa BAKWATA.

Nilikuwa mmoja wa Waislam waliokuwa ndani ya ukumbi ule siku hii Rais Mkapa alipowapa Waislam majengo ya TANESCO Morogoro ili yawe Chuo Kikuu Cha Waislam.

Laiti EAMWS isingepigwa marufuku na serikali Waislam wangekuwa na Chuo Kikuu toka mwaka wa 1968.

Kuvunjwa kwa EAMWS na kuundwa BAKWATA ndiyo mwisho wa juhudi za Waislam kujenga shule na Chuo Kikuu walichokusudia.

Historia ya Waislam wa Tanzania katika juhudi ya kutafuta elimu ni ndefu na imejaa misukosuko mingi.

Hotuba hii ya Mzee Kondo imenikumbusha maneno ya Mufti Sheikh Hassan bin Ameir alipowaambia Waislam mara tu baada ya kupata uhuru kuwa, "Waislam tumeupigania uhuru hadi umepatikana sasa tujenge shule tujielimishe tutawale nchi pamoja na wenzetu."

Benjamin Mkapa alivyopata urais, Kitwana Kondo alitaka kumuona kumpa pongezi.

Mkapa akakataa, akimwambia Kitwana Kondo anunue ukurasa kwenye gazeti la serikali na kutoa pongezi huko.

Cha ajabu, Sir Andy Chande sio tu hakukataliwa kumpa pongezi Mkapa, bali pia alitoa pongezi ya bakhshish ya Range Rover Vogue lililokuwa liki park nyumbani kwa Mkapa pale Sea View.

Alikubaliwa bila shida na hakupewa sharti la kuchapisha pongezi kwenye gazeti la serikali.
 
Benjamin Mkapa alivyopata urais, Kitwana Kondo alitaka kumuona kumpa pongezi.

Mkapa akakataa, akimwambia Kitwana Kondo anunue ukurasa kwenye gazeti la serikali na kutoa pongezi huko.

Cha ajabu, Sir Andy Chande sio tu hakukataliwa kumpa pongezi Mkapa, bali pia alitoa pongezi ya bakhshish ya Range Rover Vogue lililokuwa liki park nyumbani kwa Mkapa pale Sea View.

Alikubaliwa bila shida na hakupewa sharti la kuchapisha pongezi kwenye gazeti la serikali.
Sababu ilikuwa nini kwa Andy Chande?
 
Sababu ilikuwa nini kwa Andy Chande?
Mkapa alikuwa ana watu wake, business/intellectual types, akikupenda kakupenda hata watu wakisemaje hasikii.

Andy Chande alikuwa mtu ambaye Nyerere alimpenda sana, licha ya kutaifisha National Milling (kiwanda kilichokuwa cha Andy Chande), Mzee Chande hakumuwekea kinyongo Nyerere wala kuondoka Tanzania. Aliendelea kufanya kazi na Nyerere akiwa mwenyekiti wa bidi nyingi sana. Mkapa alimuheshinu sana Andy Chande kwa hilo.

The Range Rover Vogue did nit hurt his chances either.

Mimi nilikuwa nacheka sana nikienda pale Sea View na kuliona lile Range Rover, halafu namsikia Rais Mkapa anavyokemea rushwa mpaka kuunda Tume ya Warioba.

I guess he thought of himself as a special case.

Rex Mkapa, son of Julius Kaizari Nyerere.
 
Back
Top Bottom