Kiwanda gani naweza fungua/anzisha kwa gharama ya millioni nne?

mkuu, Alibaba wengi wanaweka display price, na wanaifanya iwe chini ili ikuvutie wewe kutembelea duka lao (ni sawa na kariakoo maduka ya ghorofani wanatangaza bidhaa bei ya chini, ila ukipanda unakuta bei tofauti, huna jinsi unajikuta unanunua tu au kuangalia bidhaa nyingine duka hilo).
Dola 800 kwa production line nzima ni NGUMU .Ni kitu hakiwezekani.
Pia tujue pia , Bei inayoonekana Alibaba ama ni display price tu. au FOB na ukipiga CBM za kila mashine na kuculculate gharama za kuzisafirisha unakuta mpaka umezifikisha mashine mkononi kwako bei inakuwa juu ghali (kitu ambacho watanzania wengi wanataka mashine nzuri ila za bei ya chini[emoji16]).
Pia bei zinapoweka kwenye range 500-5500 hapo haimaanishi kwamba 5500 ndiyo production line nzima. Pengine huenda hiyo ndiyo bei ya mashine moja ambayo ndiyo ya bei ya juu katika production line nzima.
Hivyo ili kujua bei ya production line nzima ni lazima ufanye mawasiliano na muuzaji akupe PI.
 
Hawa ni wauzaji wanaoaminika.....site yao inaitwaje
Tembelea ukurasa wa facebook/instagram, jina ni: thebridgetz & thebridgegulio.
Physical address ni DSM. Kinondoni mkwajuni nyuma ya ccm, lilipo tawi la timu ya simba (nje utaona bendera ya simba). Hapo ndipo ilipo THE BRIDGE
 

Mkuu ushapata kiwanda au bado ?
 
Anzisha kiwanda cha kutengeneza juice ya miwa tuu
 
Labda cha kukamua juice ya miwa
 
Tengeneza machinjio yako ndogo ya kisasa ya kuweza kuchinja ng'ombe watano tu kwa siku baada ya hapo utaendelea kupanua kiwanda chako

I am just worried, lazima kutakuwa na utaratibu mrefu sana wa aina hii ya kiwanda
 
what an idea....safi hii mkuu ukikomaa nayo inakutoa anza taratibu ifanye iwe long term goal
 
Kushona nguo,na hasa ukizingatia cherehani moja ni kiwanda. Na msimu wa sikukuu ndio huu tena. Changamkia fursa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…