Kiwewe kimezipata nchi za kiarabu. Huku Iran akiahidi kuanza na vituo vya nyulia vya Israel. Viongozi wao wapigiana simu kama watoto

Kiwewe kimezipata nchi za kiarabu. Huku Iran akiahidi kuanza na vituo vya nyulia vya Israel. Viongozi wao wapigiana simu kama watoto

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Wakati maelfu ya wapalestina wakiuliwa kama kuku,viongozi wa nchi za kiarabu walipiga kimya na kula biriani zao wakiona hayo hayawahusu.

Hata diplomasia zao na kulaani kulikuwa kwa njia za kinafiki.

Baada ya kumfanya Netanyahu ajiamini kupiga apendapo na kuamua kuipiga Iran na Iran nayo kutofanya ajizi kwa kujibu pigo hilo kwa ujasiri mkubwa. Sasa viongozi wa nchi za kiarabu ndio wameanza kuamka na kuanza kupigiana simu wakiulizana nini kimetokea na nini wafanye.

Kiwewe hicho kimeongezeka sana tangu juzi baada ya kudhihirika Israel imekusudia kuficha aibu kwa kuamua kuipiga Iran huku na Iran nayo ikipandisha mori na kusema ikiguswa tena itajibu kwa nguvu kubwa na kwa kutumia silaha kali zaidi na kuahidi kuanza na vinu vya nyuklia vya Israel.

Simu zimekuwa hazsikae tena mezani kati ya wafalme wa UAE na Saudi Arabia.Kwa upande mwengine Qattar nayo imechanganyikiwa kwani ina askari 10,000 wa Marekani na kambi kubwa ya kijeshi ya nchi hiyo.

Katika mazungumzo yao hayo viongozi hao wamekuwa wakiijadili Jordan na hatari inayoinyemelea ya kuzidiwa na wimbi la vuguvugu kutoka Iran litakalotoa lango la Iran kuifikia Quds.

Israel-Iran conflict: Saudi, UAE warn of dangers of war spreading in region

 
Mnavyowasifia utafikiri, wao Hawkwell,I kupigwa na kitu kizito vile
 
Teh teh teh! Yaani utazani propaganda ya enzi ya vita vya ghuba. Umenikumbisha mtu alikuwa anaitwa Talik Aziz
 
Hawa Gulf C C wanawalipa wazungu kuwalinda na ndio maana mnaona uwepo wao kila mahali wakilindwa
Yote hiyo ni kumuogopa Iran
Saddam walimuuwa na ndio alikuwa mbabe maana baada ya wao kumuibia mafuta wakati walimuingiza kwenye vita na Iran
Aliahidi kuichukua mpaka Saudia
Alipoikamata Q8 kwa masaa 3 akaamua kupitiliza na kuingia Saudia maili kadhaa na majeshi ya Saudia yalikimbia na kuacha silaha nyuma (I was there) sio hadithi

Wairaq wakaamua kuweka mines kwenye ardhi ya Saudia
Wengi waliopita kutaka kutoroka walilipuka
Ni mengi yalitokea ila kwa sasa ni lazima waogope maana gharama za kulindwa na dau linapanda
Kuna usa,uk, France, Germany na mataifa mengine wanawalinda na hela zinawatoka haswa
Yaani watatozwa mpaka wakope
Iran hana utani aliahidi zamani na Israel na waarabu wanalijua hilo
Silaha wanazo na nguvu wanayo
Hapo ni kuwahonga tu maana sidhani kama kuna taifa linahitaji ugomvi wa kuangamizana
Siku hizi nchi kibao zina satellite angani kwa hiyo wote wanaangaliana tu
America akisogeza meli za kivita basi mchina, Russia wote wanaona hata India pia
Kila nchi ina rafiki wa kinafiki na wa ukweli ila wauza silaha ni wale wale kila mmoja anatengeneza
Ipo siku na buza mtatengeneza silaha muuze nje au mnasemaje
Acha tuendelee na unoko tu ndio tunaujua zaidi
 
Iran ashushe kipigo kuanzia kwa Israel na vibaraka wa kiarabu
 
Kitu ambacho Nina kiona katika huu ugovi wa middle East kati ya Israel na Palestine ni kama nchi baadhi ya nchi zakiarabu wamekubaliana katika vikao vyao vya ndani kuungana kisirisiri ili kupigana na Israel na wana vi fund baadhi ya vikundi ambavyo vimejitanaibisha wazazi kupigana na Israel huku wao wakiwa nyuma ya vukindi hivyo.
 
Back
Top Bottom