wanaume bwana,
kwanini uwe na uamuzi wa mwisho?
kwa nini msiwe na uamuzi wa pamoja? kujadiliana kwa pamoja nini cha kufanya?
kwa nini msipange priority zenu pamoja?
kwa nini msishirikiane kwa pamoja?
mtabishana humuuu weeeeeeee, mtajiita vichwa aka taasisi huru weeee...
lakini mwisho wa siku nyumba yenye mafanikio ni ile inayosikilizana na kushirikiana kwa pamoja, ambayo kila mwanandoa anaweza kujieleza kwa uhuru
Nimwogope babu yangu tena!
Keshanambia maana yake,inatisha lol!
Mda huu kloro yuko mahakamani siunajua fildi yake ngoja akirudi na akaona hizi sera zako hapa utajuta,
Babu anakupoteza keshakula advance ya mahari yangu kwa Kloro!
Unalijua hilo???
Nitaarifa tu,Umeharibu,usingemwambia,ungemwacha kwanza,jamaa atajinyona na mlenda bure!
Canta bwana, yaani tunarudi kulekule haya ngoja nikuache hapa ukumbini ukiwa hujaelewa ila hata ODM anajua watu wazima hapa washaelewa lolKhaaaa,Babu?
Ongeza font tafadhali sijaelewa hapa umeandikaje lol!
Mkuu naona umeishikia bango hii ishu si kidogo. Huyu Canta ndiyo hajaelewa mi nishaongea na Kloro ameniambia anataka kurudi Brazil kuna mpango bado hajaumalizia hivyo mimi niendelee tu. Na ameshanipa mbinu zote za kung'oa huu mzigo. Wewe tulia angalia hii gemu inavyokwenda, lazima kieleweke si unaona mtoto ashaanza kuuliza maana ya jina...hehehe ngoja niishie hapa kwanza.Umeharibu,usingemwambia,ungemwacha kwanza,jamaa atajinyona na mlenda bure!
Mkuu naona umeishikia bango hii ishu si kidogo. Huyu Canta ndiyo hajaelewa mi nishaongea na Kloro ameniambia anataka kurudi Brazil kuna mpango bado hajaumalizia hivyo mimi niendelee tu. Na ameshanipa mbinu zote za kung'oa huu mzigo. Wewe tulia angalia hii gemu inavyokwenda, lazima kieleweke si unaona mtoto ashaanza kuuliza maana ya jina...hehehe ngoja niishie hapa kwanza.
BADILI TABIA,
Nadhani haujamwelewe vizuri kuhusu dhana ya kuwa na uamuzi wa mwisho. Kwanza nikubaliane na wewe kuhusu dhana shirikishi. Lakini ktk dhana hiyo lazima maamuzi yafikiwe, ushirikishwaji lazima kuwe na kiongozi wake ambapo sasa mtasema haya tumekubaliana na pale msipokubaliana ni vema kura ya turufu ikafanya kazi yake (Mwanaume), hapo ndio tunaposema mwanaume ni kichwa cha familia.
hehehehe watu wanadunda na style hii hii ya udikteta unayoielezea wewe na wametoka mbali sana tu.Mkishaamua kuwa pamoja kila kiitu either mume au mke alichochuma peke yake vyote ni vizuri kuwa owned kwa pamoja lakini ikianza mara oh hiki kilikuwa changu au ni changu hamfiki mbali!
Na maamuzi inategemea ni maamuzi gani ukisema mume ndo mwenye final say ina maana hata chakula mume ndo aamue kipikwe kipi siku hiyo! ni makubaliano tu na kupanga kwa pamoja incase kama kujenga nyumba au kununua kitu chochote cha thamani mwenye kipato kikubwa kati yenu atasema ni wakati muafaka wa kufanya hicho kitu kwani kitakuwa ndani ya uwezo wake na hope kitakuwa ndani ya priorities!
Hivyo sioni ubaya kushirikiana but most times men wanakuwa na sauti ndani ya nyumba kwani yeye ndo huwa na kipato kikubwa kuliko mke hivyo kuwa mwenye maamuzi ya mwisho.
Nashauri wanandoa kutokuwa rigid eti kitu fulani hakiwezi kufanyika hadi fulani atoe maamuzi! wengine hadi mtu akiumwa kwenye family lazima baba ndo atoe maamuzi ya kupelekwa hospital! na wengine hata chakula hakipakuliwi hata kama kiko tayari hadi baba arudi eti!
Huo ni udicteta hamfiki mbali kwa mtindo huu!
Kuna jamaa akichinjwa kuku akapikwa akaiva lazima akague finyango kama zipo yote!
hakuna mtu anaemilikiwa na mtu mwingineNimejiuliza wakati napitia uzi wa Cantalisia kuhusu jamaa alietoka nduki baada ya kugundua mpenzi wake ana mawe zaidi yake.Sasa swali linakuja,kwanza wanawake wanakubali kuwa mwanaume ni kichwa cha familia?(Kuwa kichwa kuna maana ya kutolea maamuzi ya mwisho jambo lolote linalohusu familia)kama wanakubali mwanaume ni kichwa kwa tafsiri hiyo,Je mwanamke anapoolewa akakutwa na mali aliyoichuma mwenyewe hii nayo itaingia katika usimamizi na maamuzi ya mwisho ya mume?(hapa nazungumzia maamuzi chanya sio ya kufuja mali)Yaani mke hatakua tena na kauli ya mwisho na namna ya kuendesha mali hiyo kwa sababu mwanamke huyo tayari anamilikiwa na mume ama mali ya mwanamke haitamhusu mume?Jambo hili huenda ndio sababu ya ugumu wa kuoa mwanamke mwenye mali!
Huu ni ukweli,lazima familia iwe na msemaji wa mwisho,na msemaji huyo ni baba!