KKKT : Maaskofu hatujagawanyika kuhusu Katiba

KKKT : Maaskofu hatujagawanyika kuhusu Katiba

Safi sana Askofu,hakika ww si mnafiki,Mungu ambariki Dr Bagoza,Bishop
 
acha ujinga wewe tamko linaendelea kusomwa makanisani Halafu unaleta ubishi WA kijinga hapa.kwa taarifa yako Katika Katika kabisa katoliki askofu WA jimbo au Hata paroko WA parokia anasikilizwa kuliko kardinali.maaskofu wanateuliwa na papa hivyo kardinali hana ubavu wa kuingilia majukumu yako ndiyo maana hana ubavu WA kuzuia tamko la maaskofu kusomwa makanisani anabaki kulalamika tu.

Wewe acha kutapika, katika kanisa katoliki kiongozi wa ngazi ya juu ni Papa, msaidizi ni cardinal, kiutaratibu wote hawa ni maaskofu katika ngazi za juu. Maaskofu wote Tanzania wanafanya kazi chini ya cardinal anayemuwakilisha papa katika nchi.nchi huwa na kiongozi mkuu wa kanisa mmoja. Maaskofu wote wanasikiliza yeye anaelekeza nini kiutendaji.
Suala la maamuzi ta TEC cardinal anaingia kama maaskofu wengine na hivyo hutoa ushauri na kiutaratibu huwa hapaswi kutoa amri isipokuwa hushauri tu. Sasa msimpake tope kiongozi huyu kwa umamuma wenu na ushabiki wa kihuni. Aliyekuambia cardinal hasikilizwi nani.
Aliyetia ruhusa kusoma walaka kanisani ni yeye na kama kiongozi wa kanisa angeamua kupunga kannisa lisishiriki kwenye walaka hakuna mtu angeusoma kwa kuwa tu amuamini.
Askifu mkuu marasusa pua angesema hapana hakuna askofu chini yake au muumini angevutana shati na yeye. Hawa maaskofu wote wanahekima ndi maana wamewaachia waumini waelimishwe bila kulazimishwa.
 
Askofu Benson Bagonza wa KKKT Dayosisi ya Karagwe amepinga vikali kauli ya serikali kwamba maaskofu wamegawanyika kuhusu Kura ya Hapana kwenye Katiba Mpya.

Askofu Bagonza ambaye ni mjumbe wa CCT ameonya kauli ya Samwel Sitta kwamba Serikali haitarudi nyuma kuhusu katiba mpya.

Askofu Bagonza ambaye ana msimamo thabiti amesema wapo maaskofu wa mfukoni wanaoandaliwa na Serikali ambao wanatumika kujibu hoja mbalimbali za kanisa.

Akizungumzia Kauli ya Kadinali Pengo kupingana na maaskofu wenzake, Askofu Bagonza amesema huo ni msimamo binafsi wa Kadinali Pengo na siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.

Askofu Bagonza amesema msimamo wa Kanisa Katoliki nchini unatolewa na TEC ambalo ni Baraza la Maaskofu Katoliki nchini.

Askofu Bagonza amesisitiza kwamba pamoja na msimamo binafsi wa Kadinali Pengo lakini ameruhusu Tamko la Maaskofu kusomwa katika Makanisa yote ya Jimbo lake la DSM.

Askofu Bagonza ameishangaa serikali kusema Kanisa halina haki ya kuwataka waumini kupiga kura ya Hapana.

Askofu Bagonza amesema.." Kama CCM na serikali yake wanawashawishi watu wapige kura ya Ndiyo, Ukawa wamewaeleza watu wao wasusie,iweje iwe tatizo kwa Jukwaa la Wakristo kuwaeleza wafuasi wao wapige kura ya Hapana?"...alihoji.
======================



Chanzo:
Mwananchi

Daaaah huyo askofu noma sana bonge la kichwa
 
Katika ibada ya pasaka iliyofanyika katika usharika wa Kayanga dayosisi ya Karagwe Baba Askofu Dr Benson Bagonza aliwatolea uvivu wavivu wa kufikiri kwa hoja zifuatazo:

1. Sisi makanisa tunapojenga shule mbona hatuambiwi tunaingilia kazi za serikali?

2. Tunapojenga miradi ya maji mbona hatuambiwi tunaingilia kazi za wizara ya maji?

3. Tupoombea mvua mbona hatuambiwi tunaingilia mamlaka ya hali ya hewa?

4. Tunaposifia serikali mbona hatulaumiwi, lakini tunapokosoa tunakaribia kupotezwa?

Akamalizia kwa kuwakumbusha kiapo cha mkristo "Nitaheshimu viongozi wangu wa dini katika yale wanayonionya na kunielekeza" Tafakari.
 
Hivi masheikh ubwabwa wao hawatoi matamko kama haya kwa nini lakini?
 
"Siasa ni njia ya kufanya maamuzi katika taifa, mji au hata dunia nzima (siasa ya kimataifa). Sehemu muhimu ya siasa ni majadilianao kati ya watu mbalimbali wenye nguvu au mamlaka. Katika demokrasia kila mtu ana kiasi fulani cha nguvu, kwa hiyo siasa ya demokrasia ina maana ya watu wote kuchangia maamuzi..."

kwa maana hiyo ya siasa, na kama kila mtu ataelewa hivyo, hakuna ubaya kwa mtu yoyote kujihusisha na siasa. watawala wengi wa tanzania wanadhani siasa ni vyama tu, au wakuu wa serikali tu, la hasha!

or see Politics
 
Hivi masheikh ubwabwa wao hawatoi matamko kama haya kwa nini lakini?

Tusiwadhalilishe hawa masheikh,tutafute tatizo la hawa watu kuitwa masheikh. Nimekuwa nikifuatilia mambo ya islam na hilo ni jambo ambalo baadhi linalowakosanisha na BAKWATA. Tatizo ni watu bora,wenye uelewa kukataliwa kila wanapojitokeza ktk chaguzi za uongozi. Angalia ubora wa sheikh mkuu?
 
Katika ibada ya pasaka iliyofanyika katika usharika wa Kayanga dayosisi ya Karagwe Baba Askofu Dr Benson Bagonza aliwatolea uvivu wavivu wa kufikiri kwa hoja zifuatazo:

1. Sisi makanisa tunapojenga shule mbona hatuambiwi tunaingilia kazi za serikali?

2. Tunapojenga miradi ya maji mbona hatuambiwi tunaingilia kazi za wizara ya maji?

3. Tupoombea mvua mbona hatuambiwi tunaingilia mamlaka ya hali ya hewa?

4. Tunaposifia serikali mbona hatulaumiwi, lakini tunapokosoa tunakaribia kupotezwa?
Hoja hapa ni kuwa dini ni yetu sisi wananchi,viongozi wa dini ni sehemu ya viongozi katika jamii yetu hivyo siasa na dini ni chanda na pete.
 
Kuweka usanii wa kuandaa maaskofu feki hakusaidii kujenga taifa imara.
 
Hoja hapa ni kuwa dini ni yetu sisi wananchi,viongozi wa dini ni sehemu ya viongozi katika jamii yetu hivyo siasa na dini ni chanda na pete.


Mpeni Kaisari vilivyo vyake KAISARI na Mpeni Mungu vilivyo vyake Mungu, Huwezi kuwatumikia mabwana wawili??????!!!!!!!!!!!!!!!!!! chagua kuwa moto au vuguvugu!!! kama bado hujanielewa baadaye utanielewa tu!
 
"Siasa ni njia ya kufanya maamuzi katika taifa, mji au hata dunia nzima (siasa ya kimataifa). Sehemu muhimu ya siasa ni majadilianao kati ya watu mbalimbali wenye nguvu au mamlaka. Katika demokrasia kila mtu ana kiasi fulani cha nguvu, kwa hiyo siasa ya demokrasia ina maana ya watu wote kuchangia maamuzi..."

kwa maana hiyo ya siasa, na kama kila mtu ataelewa hivyo, hakuna ubaya kwa mtu yoyote kujihusisha na siasa. watawala wengi wa tanzania wanadhani siasa ni vyama tu, au wakuu wa serikali tu, la hasha!

or see Politics

Mmmmmmmm!!
 
Kuweka usanii wa kuandaa maaskofu feki hakusaidii kujenga taifa imara.

Goodrich ulitaka iweje?nani anaweka maaskofu feki? unajua kazi ya uaskofu inatokea wapi? na hao maaskofu feki unaowasema wanamuongoza nani nataka majibu acha kukurupuka!!!!
 
Back
Top Bottom