Hah Hah magazeti pendwa ya Tanzania khatari sana. Wahariri wa magazeti ya Tanzania kurasa za michezo waendelee hivyo hivyo.
12 Jan 2019
Mabingwa wa Tanzania Bara Simba SC wameianza vyema hatua ya makundi ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika baada ya leo kuichapa JS Saoura ya Algeria mabao 3-0, mchezo ukipigwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Mara baada ya mchezo, Kocha wa JS Saoura Nabil Neghiz amevilaumu vyombo vya habari vya Tanzania akidai kuwa vimekuwa vikitoa taswira kuwa timu yenye uwezo kwenye kundi hilo ni Al Ahly pekee.
Kocha huyo pia amesema vyombo hivyo vimepotosha kauli aliyoitoa wakati jana na kuandika kinyume na aliyoyasema jambo ambalo anadai kuwa limechangia kuwapunguzia nguvu. Akizungumzia mchezo kocha huyo amesema Simba ni timu ngumu wakati timu yake bado ni changa hivyo iliingia kwenye mchezo huo kwa kuiheshimu huku akijipa moyo kuwa kupoteza mchezo wa leo hakutawakatisha tamaa kwakuwa bado kuna mechi nyingi mbele.
Source : Azam TV