Klabu bingwa Ulaya: Je, Barcelona itafanikiwa kupindua matokeo?

Klabu bingwa Ulaya: Je, Barcelona itafanikiwa kupindua matokeo?

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
IMG_20210310_104250_508.png


Baada ya kupokea kichapo kizito cha goli 4-1 kutoka kwa PSG katika Dimba la Camp Nou, Barcelona leo inatupa tena karata yake ya pili kuvaana na PSG ikiwa nyumbani katika uwanja wa Parc des Princes.

Huu ni mchezo wa marudiano wa hatua ya mtoano ambapo katika mchezo wa kwanza Kylian Mbappè aling'ara baada kuweka kambani goli tatu (hat trick).

Ili kuweza kuendelea kwenye hatua inayofuata Barcelona inahitaji kufunga goli 4-0 au zaidi.

Barcelona imekuwa katika kiwango kizuri na haijapoteza mchezo tangu Februari 16 ilipopoteza mbele ya PSG, huku miamba hiyo ya Ufaransa ikishinda michezo mitatu mfululizo.

Kwingineko takwimu zinaonesha kuwa Liverpool haijawahi kutolewa kwenye mashindano ya Ulaya kwenye hatua ya mtoano baada ya kushinda mchezo wa kwanza wa ugenini.

Baada ya kutoa kichapo cha gi 2-0 kwa RB Leipzig katika uwanja wake wa nyumbani, Liverpool imekuwa na wakati mgumu baada ya kupoteza michezo mitatu na kushinda mmoja tu dhidi ya Sheffield United.
 
Sioni Barcelona hata akipata tu ushindi (wowote) usiku wa leo.
 
Jamani sisi kama Barcelona sio kama Utopolo fc hatutaki kujitia pressure, sisi hatuendi kupindua matokeo ila tinaenda kucheza kuonesha ukubwa wa brand ya Barca kuliko ya PSG. Hatuna mbwembwe za kusema lazima tupindue matokeo. Tutacheza kuwaheshimu Hawa vijana wa Paris. Ila kama watakaa viby tunapindua meza mlangoni pao. Tulishakubaliana sisi Barcelona msimu huu sio washindani kwenye UEFA. Ila tutaendelea kulinda heshima yetu kwenye hii michuano
 
Jamani sisi kama Barcelona sio kama Utopolo fc hatutaki kujitia pressure, sisi hatuendi kupindua matokeo ila tinaenda kucheza kuonesha ukubwa wa brand ya Barca kuliko ya PSG. Hatuna mbwembwe za kusema lazima tupindue matokeo. Tutacheza kuwaheshimu Hawa vijana wa Paris. Ila kama watakaa viby tunapindua meza mlangoni pao. Tulishakubaliana sisi Barcelona msimu huu sio washindani kwenye UEFA. Ila tutaendelea kulinda heshima yetu kwenye hii michuano
Mkuu kwa heshima na taadhima ninayo furaha kukutaarifu kuwa leo ndio mwisho wa timu yenu katika haya mashindano.
 
Mkuu kwa heshima na taadhima ninayo furaha kukutaarifu kuwa leo ndio mwisho wa timu yenu katika haya mashindano.
Mkuu sisi mwaka huu hatuna shida tunajijua, sisi sio kama hawa Utopolo fc kujitutumua wakati hali yetu tunaijui. Ila tunaenda kutetea heshima ya brand kubwa ya Barca kwenye mashindano haya. Tutawaheshimu Hawa watoto wa Paris
 
Psg anaongoza goli moja baada ya kupata mkwaju wa penalty uliopigwa na mbappe
 
Haya sasa messi na mugalu wanaongea lugha moja leo
 
Messi hana wa kumsaidia pale, kila kitu yeye tu. So kupata ushindi ni ngumu mno....Raisi afanye kuisuka upya timu. Huu ndio wakati wake kabla MESSI/Mwalimu hajastaafu, vijana wacheze chini ya Messi wapate IDEAS na kujifunza mengi kutoka kwake....hii ni fursa kubwa sana.



 
Back
Top Bottom