Klabu ya Simba imetangaza kumsajili mshambuliaji Moses Phiri

Klabu ya Simba imetangaza kumsajili mshambuliaji Moses Phiri


Klabu ya Simba leo hii Juni 15, 2022 hatimaye imetangaza rasmi kumsajili mshambuliaji hatari Moses Phiri raia wa Zambia.

Phiri amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu hiyo ya Wekundu wa Msimbazi akitokea klabu ya Zanaco FC ya nchini Zambia.

"Moses Phiri ni Mnyama, Karibu kwenye familia ya timu kubwa Afrika Mashariki na kati" imeeleza kwa ufupi taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Twitter wa Simba SC.

Mshambuliaji huyo hatari ambaye ametua Msimbazi kuongeza chachu katika eneo la ushambuliaji, amekuwa bora sana ambapo ndani ya misimu miwili ameweza kufunga mabao 27 kwenye Ligi Kuu ya nchini Zambia.
Huu usajili ni moja ya pendekezo la kocha wenu mkuu wa msimu ujao? Au ni pendekezo la Matola?
 
Huu usajili ni moja ya pendekezo la kocha wenu mkuu wa msimu ujao? Au ni pendekezo la Matola?
Unataka ujibiwe ili upate nafasi ya kukosoa kwa sababu unauliza ilhali jibu unalo tayari kichwani mwako.

Hata hivyo...Frank Lampard alifanya usajili Chelsea, lakini alitimuliwa kwa matokeo mabaya, Thomas Tuchel akaja kunufaika kwa wachezaji wale wale kwa kuchukua ubingwa wa Ulaya kwa kumfunga Man City...!

Kwahivyo performance ya timu inaweza kuwa nzuri hata kama Kocha hajashirikishwa kwenye usajili, kwasababu kinachofanyiwa kazi ni repoti ya Kocha baada ya msimu kumalizika.

Kwahivyo yote mawili yawezekana kwa Klabu kusajili au Kocha kusajili
 
Msuva ndio nashindwa kuelewa kwann viongozi wasimu approach.Kikubwa Ni kumlipa tu hela ndefu Kama mchezaji wa kimataifa kama 15M na zaidi Hivi.Kuliko kwenda kubahatusha wachezaji wa kimataifa usio kua na uhakika nao
Yule tayari yupo kwenye Rada zetu.
 
Kwahiyo phiri ndio mchezaji wa ajabu katika soka la Africa? Wakisema watoke wafumania nyavu 20 bora kwa Caf huyo Phiri atakuwepo? Angalia hapa wafungaji bora wa Caf confederation cup. Sijamaanisha ni mchezaji mbaya, bali sio mchezaji wa kutikisa Africa kwa usajili. View attachment 2262199
SIMBA kuna wachezaji walimaliza na magoili zaidi ya matatu ila hapo kwenye list uchwara sijawaona, labda ndiomaana hata Phiri hayupo.
 
Unataka ujibiwe ili upate nafasi ya kukosoa kwa sababu unauliza ilhali jibu unalo tayari kichwani mwako.

Hata hivyo...Frank Lampard alifanya usajili Chelsea, lakini alitimuliwa kwa matokeo mabaya, Thomas Tuchel akaja kunufaika kwa wachezaji wale wale kwa kuchukua ubingwa wa Ulaya kwa kumfunga Man City...!

Kwahivyo performance ya timu inaweza kuwa nzuri hata kama Kocha hajashirikishwa kwenye usajili, kwasababu kinachofanyiwa kazi ni repoti ya Kocha baada ya msimu kumalizika.

Kwahivyo yote mawili yawezekana kwa Klabu kusajili au Kocha kusajili
Mkuu assumption yako doesn't hold water in Africa. Kwa sababu mkimleta Kocha Mpya akifeli issue ya kwanza kujitetea nayo ni ya kukuta wachezaji ambao yeye hakuhusika kuwasajili. Refer issue ya Pablo!
 
Nikikumbuka Mabegi haya mwili unachoka kabisa... [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
20220616_054034.jpg
 
Mkuu assumption yako doesn't hold water in Africa. Kwa sababu mkimleta Kocha Mpya akifeli issue ya kwanza kujitetea nayo ni ya kukuta wachezaji ambao yeye hakuhusika kuwasajili. Refer issue ya Pablo!
Kwa Afrika, hasa Afrika Mashariki hakuna Kocha anasema namtaka mchezaji fulani asajiliwe na akasajiliwa, kama ikitokea ni mara chache sana, kinachofanywa ni kutumia ripoti ya mwalimu baada ya msimu kumalizika.

Nakumbuka hivi karibuni Mwinyi Zahera wakati akiwa Kocha Mkuu Yanga, alishirikishwa kwenye usajili, je matokeo yalikuwaje..?!

Issue hapa awepo Kocha au asiwepo, je Mchezaji anayesajiliwa ni Top Class Player...!?
 
Bado mshambuliaji mwingine mkali kama Phili.

bado kiungo mkata kinyesi kama Lwanga/anatakiwa pale kati.

Tshabalala na show me the way wasaidiwe wale vijana washatumika sana wanaanza ku-flop.

Atafutwe center half mwingine wa uhakika alafu Inonga atumike namba nne,uchezaji wa namba tano wa Inonga kama mtu wa mwisho utaighalimu Simba huko mbeleni.

kocha wa viungo atafutwe mwingine injury za mara kwa mara shida ipo huko kwenye mazoezi ya viungo.
haya ni maoni tu wala sio lazima.

Kwa kapombe yule israh mwenda yuko vizuri sana akiwa fiti ila ni injury saaana yule mtoto, bado nafasi anayo ya kumsaidia shomary kwenye game nyingi tu,
Kwa upande wa Shabalala anaitajika beki mwingine yule Gadiel kazi imemshinda misimu mitatu hana kipya cha ziada
Pale kati kwenye beki yes inonga anaitaji mtu wa uakika zaid tena awe ball player mwenye pass Accuracy,long ball hata asipokua na kasi basi awe na akili nyingi sana Onyango sio ball palyer kabisa pass10 zinafika 3 hii ni dhahama kwa center back kupoteza mipira ovyo
 
Japo usajili ni kamari lakini hapa nawapongeza Simba kwa kumsajili Moses Phiri. Kuwika au kutokuwika kwa mchezaji hii ipo duniani kote tena unakuta mchezaji kasajiliwa kwa gharama kubwa sana halafu anafika anakuwa kituko kabisa wakati alikotoka alikuwa anawika vibaya sana mfano mzuri ni Chikwende na Yikpe.

Lakini kwa takwimu na baadhi ya mechi nilizomuona Phiri akicheza kwa kweli ni mchezaji mzuri na zaidi ya yote anaweza kucheza karibia nafasi zote pale mbele winga zote na katikati tena kwa usahihi mkubwa achilia mbali mashuti yake makali nje ya kumi na nane ambayo yanalenga goli kwa usahihi.
 
Bado mshambuliaji mwingine mkali kama Phili.

bado kiungo mkata kinyesi kama Lwanga/anatakiwa pale kati.

Tshabalala na show me the way wasaidiwe wale vijana washatumika sana wanaanza ku-flop.

Atafutwe center half mwingine wa uhakika alafu Inonga atumike namba nne,uchezaji wa namba tano wa Inonga kama mtu wa mwisho utaighalimu Simba huko mbeleni.

kocha wa viungo atafutwe mwingine injury za mara kwa mara shida ipo huko kwenye mazoezi ya viungo.
haya ni maoni tu wala sio lazima.

Simba Sisi Ni wagumu sana Kuwaachia Baadhi ya Wachezaji Kwenda Kwasababu kuna watu wananufaika pale na Wale wachezaji.

Lakini kiukweli kama tunataka kushindana tena kimataifa basi tuna wachezaji zaidi ya 10 ya kuwaacha, na kutafuta mbala wake.

Kapombe ameshachoka yule ni binadamu kucheza Dakika 90 kila mechi kwa ubora ule ule ni uongo.

Mohamed Hussein Amechoka

Mugalu kwa sasa sio Hadhi ya simba kwa sababu ameshindwa kuonesha kile alichokuwa nacho leo mzuri kesho mbaya.

Kagere msimuu huu benchi la Ufundi limeua Kiwango chake tumpe mkono wa Kwa Heri.

Bocco, Arudi Azam Akajipange tukimuhitaji tutamchukua.

Tadeo Lwanga Tumshukuru kwa Yote aje hata yule UDOH tulie mfanyia majaribio, Ni hasara sana kuwa na Mchezaji wa Nje anaye Kaa Benchi.

Bwalya Naye tumuage tumchukue mtu atakaye kipiga zaidi ya Bwalya na kumpa changamoto chama za kujiuliza.

Nyoni, Mkude, Hassan Dilunga tuwaage
 
Simba Sisi Ni wagumu sana Kuwaachia Baadhi ya Wachezaji Kwenda Kwasababu kuna watu wananufaika pale na Wale wachezaji.

Lakini kiukweli kama tunataka kushindana tena kimataifa basi tuna wachezaji zaidi ya 10 ya kuwaacha, na kutafuta mbala wake.

Kapombe ameshachoka yule ni binadamu kucheza Dakika 90 kila mechi kwa ubora ule ule ni uongo.

Mohamed Hussein Amechoka

Mugalu kwa sasa sio Hadhi ya simba kwa sababu ameshindwa kuonesha kile alichokuwa nacho leo mzuri kesho mbaya.

Kagere msimuu huu benchi la Ufundi limeua Kiwango chake tumpe mkono wa Kwa Heri.

Bocco, Arudi Azam Akajipange tukimuhitaji tutamchukua.

Tadeo Lwanga Tumshukuru kwa Yote aje hata yule UDOH tulie mfanyia majaribio, Ni hasara sana kuwa na Mchezaji wa Nje anaye Kaa Benchi.

Bwalya Naye tumuage tumchukue mtu atakaye kipiga zaidi ya Bwalya na kumpa changamoto chama za kujiuliza.

Nyoni, Mkude, Hassan Dilunga tuwaage
Kama kweli tunataka kuvuka pale tunapoishia yaani robo fainali ya michuano ya CAF

Lazima Simba SC ije kivingine kabisa kwenye usajili.

Naunga mkono hoja, Boko abaki kupewa majukumu mengine, Na Mkude si mbaya akabakia na wapewe mkono wa shukrani akina

Gadiel
Israel
Nyoni
Wawa
Dilunga
Mhilu
Lwanga
Kagere
Mugalu
Bwalya
Morrison

Kama tunafanya fair tusilalamike tunapoishia..!
 
Back
Top Bottom