Klabu ya Simba yamfungia Kessy

Kama ni kupiga hizo krosi ata Beckham alizipiga sana Man Utd lakini mwisho wa siku aliuzwa mpira ni zaidi ya krosi.
 

Hivi Polisi hawajaona kosa la jinai (Shambulio la mwili) dhidi ya huyo kipa wa Simba? Nilitegemea kusikia kawekwa ndani kwa kumpiga Kessy.

Nichukue fursa hii kumshauri Kessy aende Polisi akafungue RB ili huyo mtuhumiwa akamatwe na ashughulikiwe kwa mujibu wa Sheria. Hakuna mtu ndani ya Tanzania anayeruhusiwa kumpiga mtu mwingine. Mhe. Rais amekuwa akisisitiza kuheshimu sheria za nchi.
 
Kwanini msifukuze ol players
 
Mbona dogo tangu jana alishasema msimu ukiisha anahama timu
Na hatohudhuria mazoezi kuanzia sasa
 
Aende tu! Timu ilikuwa vizuri kwenye mechi na Toto.Yuko peke yake badala yakuondoa yeye anasubiri kumkanyaga mtu.Hii si nidhamu ya soka.Simba ni timu ya mfano hapa Tz,haipaswi kuwa na mtu asiyejua thamani yake ndani ya hii timu.
 
So bila maneno ya Muro ina maana Simba ingeshinda? Acheni kuwatupia lawama viongozi, mpira unachezwa na wachezaji
Mkuu mchezaji hata anapokuwa anafundishwa kunakuwa na somo la psychology kama hulijui hilo basi ndio ujue sasa
 
Japo kiwango na kipaji anacho, lakini hajui kwamba anachezea timu pekee yenye wachezaji ulaya.Simba inakuza vipaji vyenye nidhamu.Hivyo kama Yanga mnaona kaonewa msajilini tu hamna shida.Wapo wazuri kuliko yeye watapitia simba kwenda Ulaya.
 
Hongera sana mzee na huo ndio utani wa jadi wakati nyie kwenu ni kicheko sisi wenzenu ni masononeko,pia hongereni sana kwa kuwa na mtu kama jery muro kiufupi katumia nafasi yake vizuri sana
 
Muda si mrefu Manara atatuwekea historia ya Simba,kama uwanjani inacheza historia vile.
Mimi ni mwana msimbazi lkn huyu manara naona hii nafasi haiwezi,kwanza ni mtu mwepesi sana kum provoke
 
Haa haaaaaa. Hata mimi Nimemsifu sana murro kwa hili. Sasa Msimbazi kunawaka moto, wakati hakina mtu yeyote aliyeenda na kiberiti
Mkuu maneno ya muro ni ya kiweledi sana hasa yakikuta mtu ambaye uwezo wa kuyafanyia kazi ni mdogo kama manara,huwezi kuwa msemaji wa timu kubwa kama simba ukatawaliwa na hasira za hovyoooooooo
 
Huyo kipa bondia kaachwa bila hatua yoyote?
 
Mkuu naona unanitonesha vidonda,ila sasa sioni sababu ya kumpa lawama kesi kwani mbona washambuliaji hawakufunga goli likakataliwa?
 
Mkuu naona unanitonesha vidonda,ila sasa sioni sababu ya kumpa lawama kesi kwani mbona washambuliaji hawakufunga goli likakataliwa?
Mkuu Simba inatakiwa kusukwa upya kila Idara watoto wengi ninao waona hawako Makini, si katika safu ya Ushambuliaji tu ata viungo na zaidi Mabeki lazima watambue kila mechi ni muhimu lakini ukiangalia utoto ndio mwingi lazima viongozi nao wachukue hatua stahiki wakati wa kusajiri.
 
Sawa ndugu yangu lkn ujue huu sasa ndio tunafunga mwaka wa tano hatujui ubingwa na bado tunaendelea kutoa excuse kwa viongozi wetu huoni kuwa sasa ni muda muafaka tukawageukia kina dalali?
 
njoo Jangwani Kessy uokoe kipaji chako....


halafu vipi na isihaka si na yeye ana utovu wa nidhamu...vp wadau wa nyau sc hamumtemi nae? maana hii ndo fursa nzuri ya kujipatia wachezaji wenye vipaji bila kutumia hata nguvu nyingi wala gharama kubwa, maneno ya jerry tu yanatosha
 
Kwa hilo mmelamba dume,jery ni kiboko ya manara hiyo haina ubishi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…