Klabu ya Simba yapangiwa TP Mazembe kwenye robo fainali Ligi ya Mabingwa Africa

Simba kama kila mchezaji atawajibika ktk nafasi yake kama inavyotakiwa lolote linawezekana. Cha msingi ni kujituma na kujua kilichowapeleka uwanjani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kimazingira Simba kuanza Nyumbani ni faida sana,imagine mfano mechi za Simba na As Vita zingekuwa mtoano,Simba kashapigwa 5 first leg,mechi ya pili taifa mpaka dk ya 80 matokeo ni 1-1 unadhani Simba wangeendelea kutafuta goli kwa nguvu vile walivyofanya?Lakini kama ni first leg wangekazana vilevile

Bora kama kufa tukafie moja kwa moja ugenini kuliko kukatishwa tamaa tangu mechi ya awali,muhimu tushinde hapa kwetu angalau 2-0 then huko Lubumbashi tutapigana kwa hali yoyote kutenda maajabu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mtu alikula 8........Ngoja tusuhbilie tuone
TP Mazembe ya sasa sio kama ya miaka minne iliyopita ya Samata. Hao Club Africaine walijichanganya wenyewe wakapigwa 8 pale Lubumbashi. Ukweli ni kwamba Mazembe haina tena wachezaji wa kuweza kuwafunga waarabu nyumbani na ugenini. Sasa hivi wanawategemea Kamboure na Mputu (34). Huyu Mputu alimkimbia Samata na kwenda Angola, amerejea baada ya Samata kuondoka, lakini sio yule wa kiwango cha mwaka 2011 wakati Mazembe walipokuja Tanzania. Mazembe ya sasa hata ubingwa wa Congo imevuliwa na AS Vita, na kwa taarifa yako mwezi uliopita tu imechezea kichapo 3-0 kwa AS Vita katika ligi kuu ya Congo. Hata katika play offs kombe la mabingwa waliitoa kwa taabu ZESCO ya Lwandamina, kule Lubumbashi Mazembe walishinda 1-0, na Zambia wakatoka sare 1-1. Hii ZESCO kombe la shirikisho ikapangwa kundi moja na Nkana (ambayo ilitolewa na Simba) na imekuwa ya mwisho, wakati Nkana ipo robo fainali.
Simba wakikaza wanaweza itoa Mazembe
 
Roho ya mtima nyongo na uzalendo ni vitu viwili tofauti,huwezi kuwa mzalendo na roho yako hiyo ya mtima nyongo.Hivyo nakuunga mkono uendelee kubaki Timu Roho mbaya,unaendana nayo

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaaa. Mmeshaanza kupanic mapema lol.

Ukiwa nayo roho nzuri na Uzalendo wewe inatosha Mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…