Klabu ya Simba yathibitisha kukamilisha usajili wa mshambuliaji Habibu Kyombo

Hivi huyu si alikuwa mamelod ilikuwaje akarudi bongo
 
hii ndio mishabiki ya hovyo,haijui kama usajili ni biashara. ulitakaje? akae kimya aseme tunasajili mchezaji wa kawaida, halafu watu wakalipie Simba App? ficha upumbavu wako
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya Habib Kiyombo wa Mbao Fc na huyu aliyesajiliwa simba. Anyway, makocha wake wamsaidie kurejea kwenye kiwango chake cha awali.

Kiukweli huyu wa sasa, ni wa kawaida sana.

By the way, na Kichuya naye mnamtambulisha lini?
Kiyombo mechi 15 goli 6, assist 9. Mayele mech 30 goli 16 assist 4, angalia viungo wanaomzunguka mayele halafu njoo kwa kiyombo. Je umejifunza nn hapo
 
Kiyombo mechi 15 goli 6, assist 9 .Mayele mech 30 goli 16 assist 4, angalia viungo wanaomzunguka mayele halafu njoo kwa kiyombo. Je umejifunza nn hapo
Utakuwa hujanielewa bila shaka. Mimi nimemlinganisha Habib Kiyombo wa Mbao Fc na huyu Habib Kiyombo wa sasa, aliyesajiliwa simba.

Sikumfananisha huyo Habib Kiyombo na mchezaji yeyote yule wa ligi kuu.
 
Kiyombo mechi 15 goli 6, assist 9 .Mayele mech 30 goli 16 assist 4, angalia viungo wanaomzunguka mayele halafu njoo kwa kiyombo. Je umejifunza nn hapo
Shida yetu tumetanguloza mno ushabiki bila kujali uhalisia! Leo hii Mpole amepambana na timu yake ya kawaida hadi kuibuka kidedea lakini bado watu wanamuona Mayele ni kama Malaika wakati ukiangalia daraja la wachezaji waliomzunguka Mayele na wale waliomzunguka Mpole unaona ni kwa namna gani kijana wetu alipambana. Tujifunze kuthamini vya kwetu
 
Utakuwa hujanielewa bila shaka. Mimi nimemlinganisha Habib Kiyombo wa Mbao Fc na huyu Habib Kiyombo wa sasa, aliyesajiliwa simba.
Sikumfananisha huyo Habib Kiyombo na mchezaji yeyote yule wa ligi kuu.
Habibu wa sasa wewe umemuona wapi? huyo wa Mbao ulimuona kwa sababu aliifunga Yanga
 
Natofautiana nawe kabisa,Mayele ni mchezaji wa pekee huwezi mlinganisha na Mpole.

Ukizungumzia viuongo waliomzunguka,zungumzia na mabeki wanavyomkaba Mayele.

Mayele anafunga katika mazingira magumu sana huwezi kumlinganisha na akina Mpole.
 
Halafu huu uzi umejaa watu wa Simba mnaojua jinsi tulivyokwama kifedha na hivyo naona mmebakiza pesa ya kutafutia kiki mitandaoni huku wapinzani wakifanya kweli kwenye usajili
 
Mo amekua muoga sanankuweka pesa zake chini 🀣🀣🀣
 
Mashabiki wa simba wamekua wanyonge sana baada ya huu usajili hadi kuna mmoja imebidi nimnunulie glucose sukari ilishuka sana kwa majonzi ya usajili.
 
"Yote 9, hii mainstream imejaa mabogus"

Mashabiki maandazi.

Nakumbuka Hata msimu jana tuliwamenga sana Yanga eti wamesajili wakongo wanataka kuanzisha band ya mziki!! Lakini hao hao wakongo ndo wamekiwasha hatari

Tusubiri muda utaongea!!!
 
🀣🀣🀣🀣🀣 maweee...
 
hii ndio mishabiki ya hovyo,haijui kama usajili ni biashara. ulitakaje? akae kimya aseme tunasajili mchezaji wa kawaida, halafu watu wakalipie Simba App? ficha upumbavu wako
Stress zitawauwa kutete ujinga! Unalipia Simba App mnasubiri kutangaziwa Habibu Kyombo then after few seconds inawekwa kwenye social medias nyingine tena bure.! Upuuzi mtupu.
 
Klabu ya Simba yenye maskani yake mitaa ya Msimbazi Jijini Dar es salaam, leo Julai 9, 2022 imethibitisha kukamilisha usajili wa mshambuliaji Habibu Kyombo kwa mkataba wa miaka miwil...

Simba Ina tatizo. Huyu ataishia kukaa benchi msimu mzima. Sijui hakuna scouting. Hawajajifunza kwa Yusuf Mhilu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…