Klabu ya Simba yathibitisha kukamilisha usajili wa mshambuliaji Habibu Kyombo

Utakuwa hujanielewa bila shaka. Mimi nimemlinganisha Habib Kiyombo wa Mbao Fc na huyu Habib Kiyombo wa sasa, aliyesajiliwa simba.
Sikumfananisha huyo Habib Kiyombo na mchezaji yeyote yule wa ligi kuu.
Huyu wa Mbeya Kwanza takwimu zake ni nzuri zaidi kuliko yule wa Mbao FC. Kumbuka wasomi huwa tunaagalia rate ama percentage
 
Yule dogo ni bonge la mchezaji ni vile mmejaa ushamba hamjui hata ubora wa mtu.
Sijawahi kuona mchezaji ambaye mipira yake ya adhabu au kona ina hatari kama Calinhos hapa nchini.
Nakuunga mkono Mkuu, Yule alikua mchezaji wa kweli toka nimeanza kufuatilia mpira sijawahi kuona kipaji kama kile, basi sikujua kwanini aliachwa!
 
Kweli kabisa wenzetu wamefanya usajili wa maana sanaaaa kila mchezaji waliemsajili ni kisu[emoji22][emoji22]
Halafu huu uzi umejaa watu wa Simba mnaojua jinsi tulivyokwama kifedha na hivyo naona mmebakiza pesa ya kutafutia kiki mitandaoni huku wapinzani wakifanya kweli kwenye usajili
 
Natofautiana nawe kabisa,Mayele ni mchezaji wa pekee huwezi mlinganisha na Mpole.
Ukizungumzia viuongo waliomzunguka,zungumzia na mabeki wanavyomkaba Mayele.
Mayele anafunga katika mazingira magumu sana huwezi kumlinganisha na akina Mpole.
mazingira magumu vp
au magoli yanapunguzwa ukubwa ?
 
Simba Ina tatizo. Huyu ataishia kukaa benchi msimu mzima. Sijui hakuna scouting. Hawajajifunza kwa Yusuf Mhilu.
Kuhusu Usajili wa Kyombo.

Strikers wa Simba ..

1. Mugalu
2. Kagere
3. John Bocco

Unaposajili ni lazima ulete Jembe linalozidi wachezaji waliopo, au atleast kulingana nao.

Je Kyombo ana quality ya kuwazidi hao strikers wa sasa waliopo Simba? - JIBU BAKI NALO

Je hivi Simba wapo serious, Kama kweli walitaka Top perfomer wa kusimama pale mbele afungeli magoli..

Why wasingemchukua GEORGE MPOLE?

Hivi Kyombo na George Mpole nani amekiwasha sana Msimu huu? JIBU BAKI NALO.

Nini hicho ambacho Simba wamekiona kwa Habib Kyombo ambacho Mashabiki wa kawaida kabisa wa mpira hawajakiona?

Hivi nyie Simba hamuoni kuwa huu usajili mashabiki wenu wenyewe hawajaridhika nao?
 
Ipo siku Ahmedy Ally atapigwa mawe na mashabiki wa Simba, yaani usajili huu ndo wa kusimamisha Afrika.? Amewaweka mashabiki kwenye tension kubwa sana, kumbe ni mchezaji ambaye wameenda kugombaniana na Singida.? Wonders shall never end[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
"Yote 9, hii mainstream imejaa mabogus"

Mashabiki maandazi.

Nakumbuka Hata msimu jana tuliwamenga sana Yanga eti wamesajili wakongo wanataka kuanzisha band ya mziki!! Lakini hao hao wakongo ndo wamekiwasha hatari

Tusubiri muda utaongea!!!
Usisahau hata misimu iliyopita Yanga walibeza kuwa Simba SC imesajili Wazee lakini walichofanya kwa misimu minne kila mmoja ameona.

Kwahivyo kufanya mambo kwa kutaka kila mmoja alidhikie hiyo haipo.
 
Kiyombo mechi 15 goli 6, assist 9. Mayele mech 30 goli 16 assist 4, angalia viungo wanaomzunguka mayele halafu njoo kwa kiyombo. Je umejifunza nn hapo
Ukiangalia takwimu kati ya Mugulu na Kyombo bora kyombo
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya Habib Kiyombo wa Mbao Fc na huyu aliyesajiliwa simba. Anyway, makocha wake wamsaidie kurejea kwenye kiwango chake cha awali.

Kiukweli huyu wa sasa, ni wa kawaida sana.

By the way, na Kichuya naye mnamtambulisha lini?
Hili la Yanga kusajili wachezaji 2 wa kigeni kambole magoli 2 mechi 48 , morisoni mechi 22 magoli 0 na huyu aliyesajili mchezaji mzawa mechi 12 magoli 6?
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya Habib Kiyombo wa Mbao Fc na huyu aliyesajiliwa simba. Anyway, makocha wake wamsaidie kurejea kwenye kiwango chake cha awali.

Kiukweli huyu wa sasa, ni wa kawaida sana.

By the way, na Kichuya naye mnamtambulisha lini?
Hili la Yanga kusajili wachezaji 2 wa kigeni kambole magoli 2 mechi 48 , morisoni mechi 22 magoli 0 na huyu aliyesajili mchezaji mzawa mechi 12 magoli 6 unalizungumziaje mkuu? Au kwakuwa wako Yanga utakuja na utetezi ?
 
Hili la Yanga kusajili wachezaji 2 wa kigeni kambole magoli 2 mechi 48 , morisoni mechi 22 magoli 0 na huyu aliyesajili mchezaji mzawa mechi 12 magoli 6?
Bado hamjanisoma kabisa. Kiyombo ni mchezaji mzuri! Ila majeraha yamemrudisha sana nyuma.

Na ndiyo maana nikasema makocha wake wapya wana jukumu zito la kumrejeshea makali yake ya awali.
 
Umeongea fact mkuu, tumekalili wachezaji wa nje ndio wanafaa, type ya kina Mugalu
 
Dah....roho yangu nahisi Kama bado haijaridhika!

Nilikuwa na matumaini makubwa leo tunawakera utopolo! Anyway ngoja tuone.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…