William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,400
Anasema suluhisho la matatizo yetu ni kubadilisha mfumo wa kiuchumi ambao unaruhusu wachache kumiliki mabilioni ya pesa huku walio wengi hawana kitu. Halafu hapo hapo anasema hayo mapesa yanayomilikiwa na wachache sio yao bali, ni ya Serikali. Tatizo la kutoelewa au labda kushindwa kujieleza linajitokeza hapa. Kama wachache wanamiliki pesa zisizo kuwa zao basi hilo ni tatizo la ufisadi, tatizo la wizi, na sio tatizo la mfumo wa Uchumi. Utabadilisha mfumo, na hata ukafufua Azimio la Arusha, lakini kama kujapigana na ufisadi, mfumo wako mpya labda ndio utakuongezea matatizo maana utazidi kujichanganya. Sasa hivi Watanzania tumechanganyikwa juu ya mfumo wa Siasa na Uchumi tunaofuata, kati ya Ujamaa na Kujitegemea au Ubepari unaoruhusu njia kuu za uchumi kumilikiwa na wachache. Kubadili mfumo wa Kiuchumi peke yake hakuwezi kutatua ufisadi
Msiwaone hivi hawa viongozi wa CCM ambao wako nje ya chungu! Anne Kilango kama alikuwa rafiki wa kupika na kupakua wa Sophia Simba mnatagemea kwamba naye si mmoja wao? Subirini JK ampe uwaziri muone atakavyobadilika! Hawa wenzetu wakiishaingizwa kwenye chungu kwa kupewa uwaziri wanabadilika kabisaaaa na kama ilivyo ada wanaanza kutetea yale yale waliyokuwa wakiyapinga walipokuwa nje! Tanzania itajengwa na Wazalendo wenye Moyo wa dhati!
Nimemaliza kusikiliza, nikaenda moja kwa moja kuangalia CV yake kwenye web ya bunge. She talks the talk ila kuna vishimo vingi kwenye hiyo interview, anaonekana yuko naive kweli au yupo hapo kupiga debe tu. Na unavyosema FMES kwamba hataki uwaziri, well, unaweza usiwe waziri ukawa mpiga spin tu wakati na wewe unafaidika. This is my opinion, sio kwamba yuko hivyo.
MKJJ, asante kwa interview. Nimependa, yuko very articulate, na kama FMES unasema anachukua digrii ya uchumi, itamsaidia sana. Lakini kama ndio anamalizia halafu analysis yake ya mambo ndio hii, na mnapigia debe huyu ndo mmoja wa wakombozi wa Tanzania, then am sorry, I see no bright future. I mean, kiongozi makini huwezi ukakaa ukafananisha apartheid na matatizo yetu. I am sorry, but she was wishy washy. Her kind of language can win her votes though with Tanzanians in the villages!!
The woman has potential, but longway to go, and I would love for her to reach that potential that can move Tanzania.
Hiyo ya apartheid ni cha mtoto. Alichonimaliza ni kum-quote JK. Nadhani Mkandara kawahi kumaliza hapo kila kitu. Na ndio maana tunasema aidha ni naive, au kapandikizwa apige debe. Nitakuwa wa kwanza kumwomba msamaha aki prove otherwise. The woman has potential, but longway to go, and I would love for her to reach that potential that can move Tanzania.
So far, the way i see it, she is just a politician playing her cards! We really are desperate for a genuine leader aren't we?
1. Mama Kilango ni mbunge alianza kwa kupewa bure ubunge na sasa ni mbunge wa kuchaguliwa, ni vitu viwili tofauti na ni very important kwenye ku-determine msimamo wa mbunge bungeni, the point hapa ni kwamba tufike mahali bongo katiba ibadilishwe tusiwe na wabunge wa bure tena!
2. Mama ni former mwalimu wa Kisutu Sekondari, accountant ATC, Senior Accountant Gulf Air, Successful Business Woman on her own rights, na sasa mbunge wa Same East, makamu wa mwenyekiti kamati ya bunge Miundo Mbinu, mwenyekiti kamati ya bunge ya Ethics kwa viongozi wa taifa, ameweza on her own kufungua maduka makubwa ya nguo between Dodoma, Darsalama na Same, na vifaa vya ujenzi kwa kuleta bidhaa hizo kutoka USA na Europe, lakini hana nadharia ya sayansi, uchumi na mahusiano ya jamii? Pleeeeease jamani ma-professor wa JF damn!
3. Urais wa Tanzania? hivi kuna mahali popote kwenye interview ambapo amesema kuwa anahitaji ana mpango wa kugombea urais wa Tanzania? Ina maana all this nasty comments ni kwa sababu kuna wanaodhani kuwa atagaombea urais au? Kuacha Mwalimu ni nani mwingine aliwahi kuwa na hizo qualification za urais kama zinavyotakiwa hapa JF?
Ninaomba ksuema hivi, Mama Kilango anahitaji some adjustments touch ups hapa na pale kwenye view zake on important ishus za taifa, lakini sioni anything serious ambacho akiamua kugombea urais kinaweza kumzuia, kwanza ni haki yake kama Mtanzania, na kama anatimiza the most important qualification yetu CCM ya kuwa na angalau First Degree that is all what counts watakaoamua ni wananchi, na record lakini sisi wananchi wa Tanzania ndio tutakaoamua kulingana na safu ya wagombea na records zao period, personal problems za watu hazita-count kwenye taifa kama zinavyo lazimishwa hapa JF, hapana!
Mimi ninamtakia mafanikiio mema na safari njema ambayo ninajua kuwa itakuwa ni ndefu sana, maana kwa maoni mengi ninyoyaona hapa ni kwamba tayari amerithi maadui na marafiki, ninaamini kuwa anlijua hilo kwa karibu sana!
Ahsante Wakuu!