Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

napenda sana elimu ya wanyama aisee safi sana wachangiaji wote na mleta mada
 

duuh! mkuu hiyo ID yako!!!!?
 
samahani hao nyoka kwa dar wanapatikana maeneo gani? nisijeenda kununua kiwanja kumbe ndio chimbo lao
 
samahani hao nyoka kwa dar wanapatikana maeneo gani? nisijeenda kununua kiwanja kumbe ndio chimbo lao

Dalali asikudanganye ukanunua kiwanja pale kariakoo weee,wapo wengi kishenzi. (utani) kwa maeneo mengi ya Dar hawapo na hiyo ni kutokana na pilikapilika maana wale wanahitaji sehemu tulivu.
 
Mtoa mada umechanganya madesa,black mamba sio koboko.hawa ni nyoka wawili tofauti,hebu jaribu kutafti tena

We ndo umekosea, mtoa maada yuko sahihi, BM ni koboko au nyanda za juu wanamwita Nyamhando.
 
Kwetu tunamwita enchwera. Huwa haumi ovyo ovyo ils anajihami sana na mate yake! Anapenda kutemea usoni machoni...

Mkuu huyo cobra, ni muoga kiasi ndo maana anapenda kujihami na kurusha mate, ila huyu mdudu mamba mweusi harembi ukiingia kumi na name zake anakushoot tena yeye ndo anakufuata
 

Ebana ni kweli makere nilisikia kua wapo lakini nimekaa miaka kama 2,lakini sijawahi kumuona nimeona vifutu wengi sana aiseee...daaahh...
 
Akikutana na nyegere(honey burger) hizo sifa zoote anaweka mfukoni.ila binadamu ukifanikiwa kumuua utakuwa umeacha kazi umefanya kazi..hatari aloo.

Nilimuona anakimbizwa na Nyegere kama vile kibaka, mtini anae, ardhini anaye, kwenye mawe anaye, mpaka akamdaka na kumtafuna kikatili !
 
Umenifurahisha sana. Anawika kama jogoo. Tufanye biashara, ukimwona nistue nije nimkamate nataka niwafuge hao.
 



Naomba rudi shule kidogo....Koboko hawezi kuwika hata simu moja, hao wanaowika ni nyoka wa aina zingine ama wa kimazingira tu lakini si koboko.
 
thread nzur. wakishaanza kupost hawa first Yr mpaka 4th yrs wa miaka hii. hivyo. ona wanaleta utani wa kipichu hapa.

kila mtu anaifagilia thread. wangese wana anza yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…