Kocha Amunike awaondoa wachezaji wa Simba Taifa Stars kwa kuchelewa kuripoti kambini

Mbona wakati akitangaza kikosi alisema wachezaji wote anawahitaji Septemba mosi kwa ajili ya kujiandaa na mchezo hapo September 8 dhidi ya Uganda.

Ratiba gani hiyo? Chilunda, Himid, Banda?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, ratiba lazima iendane na kanuni za FIFA. Kuna minimum time ya kuwaruhusu. Lakini club ikiwa radhi wanawahi.
 
Coach alichaguliwa timu na TFF..baada ya kuona wakina Kihimbwa na Kimenya kafukuza uozo..mikia mpira sio taarabu..jitu limecheza world cup na kufunga magoli USA,Olympic limechukua gold medal.AFCON.CAF champions.. Limecheza Barcelona ya Spain sio Mbagala akapata injury ya goti....alafu mchezaji wa ovyo unaleta nyodo.Fukuza hata wa Yanga na Azam wakizingua...hii michezaji ndio maana tunashindwa kwenda AFCON miaka chungu kibao
 
acha hizo ushindi ni pamoja na nidhamu na sio kuijiona bila wewe timu haifiki kokote
Ushindi ni kiwango cha kutandaza kandanda, hayo mengine ni mbwembwe tu. Kuna wachezaji watukutu duniani lakini makocha walienda nao hivyo hivyo kwa kutambua mchango wao. Edmundo, Romario na Baloteli ni mfano tu wa wachezaji wasio na nidhamu ndani na nje ya uwanja, yaani red card ni muda wowote! Lakini hasara ya kuwakosa kikosini ni kubwa kuliko kuwa nao, na ndio maana makocha walikuwa wanawatumia hivyo hivyo kwenye vikosi vyao. Sasa itakuwa hawa waliochelewa kufika kambini, ukizingatia siku waliyotakiwa kuripoti kambini walikuwa na mechi iliyoisha saa 2.00 usiku! Mbona kambi bado inasubiri wachezaji kibao tu, watano waliopo Kigali na Yanga, akina Samata, Msuva, Ulimwengu, Banda, Farid, Chilunda na Mandawa, wote hao wapo nje bado hawajafika, eti unawafukuza wachezaji waliomaliza mechi saa 2 usiku !
 
Pomoja na hivyo mkuu, kumbuka akina Chilunda, Samatta, Mao, Msuva, Banda..Hawajaripoti na wachezaji wa Simba sio kwamba wamegoma wamechelewa tena masaa.

Tuangalie na upande wa pili, hiyo imo

Sent using Jamii Forums mobile app
kuna mmoja alichelewa dakika moja akatimuliwa lakini baadae alifunguliwa mlango akaingia naamini na hawa pia wataruhusiwa
 
Mwenye cv ya Amunike atuekee hapa naona kama tunazidi kupotea njia wakuu.Soka la Bongo limegeuka kuwa kama mchezo wa Kamari aisee hapa tutapata tabu sanaaaa
 
Amekosea kabla hajaanza!
Namsikitikia sana.

Atalijua kosa lake atakaponyunyiziwa mvua ya magoli na timu dhaifu kabisa!!

Hii misimamo mingine ni chumbani haifai sebuleni.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kocha anatuchokoza huyu sasa subiri tutaendelea kuzomea taifa stars
Timu ya taifa wachezaji wakiitwa lazima wapewe na posho za kuwafikisha kambini hilo halijazingatiwa kocha anakurupuka tu
Day one failure
Thubutuuuu..Waziri Lugola atawashughurikia mkikosa uzalendo
 
[emoji106]
 

Kuna uwezekano akili yako haikufai, kwanini wengine wawai kufika hao ndio walete kiburi? Au kwavile wanacheza Simba?
 
Acha ushabiki wa ajabu kama sababu zao hazina mashiko wachukuliwe hatua tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…