Kocha mpya Simba ni lazima aendane na falsafa ya timu

Kumbukeni tu kocha yoyote yule mpya lazima apewe muda wa kuijenga timu na kuimplement mfumo wake.
 
Msimpangie cha kufanya,tuliwashauri mumuache mgunda anawafaa mkadharau
 
Kweli Tanzania ina mashabiki Maandazi sana. Kila MTU Anajidai Anajua mpira na kujifanya coach.

Huyu coach Aachwe Atengeneze timu. Tuache kuishi kwa mazoea.

Ndio maana timu za waarabu zinafanya vizuri kwenye Mashindano makubwa, kitokana na falsafa ya mpira wa kasi Ambao coach wa Simba Anataka kuileta kwenye timu.

Nakumbuka Sven Alipokuja Simba baadhi ya mashabiki Maandazi walianza kumzodoa wakisema wanamtaka Bw Uchebe. Lakini baada ya muda Pira biriani tulianza kuliona.

Ifikie maali makocha waachwe wafanye kazi Leo Arsenal wasinge mvumilia Arteta Leo timu yao isingekua inaongoza ligi.

Tumpe muda kocha maana hata ukimsikiliza Ana MALENGO makubwa na Simba. Ushamba wa kumtegemea chama ndio akiwa hayupo timu inastrago kupata matokeo kutokana na hakuna mfumo mzuri wa kutengeneza nafasi
 
Hii falsafa imeanzishwa na nani na mwaka gani? Imepitishwa na kikao gani na kwa lengo lipi?
Kabla ya Chama ambaye ndo dhahiri unamaanisha timu ijengwe juu yake, timu ilikuwa inajengwa juu ya kiungo gani?
 
Ulipoandika BASERONA umemaliza mjadala Mkuu. Wewe ni Mburula huna unalojua.
 
Mzamiru tatizo umri, binafsi sijui kwanini Okwa hakuwahi kupewa nafasi ya kucheza mpira Simba, sijalewa kabisa..
Tatizo kelele za mashabiki, au la alipigwa misumari na wahuni
 
We ndio hovyo kabisa.Kumbuka mada hii ni kwa vile alimtoa Chama mapema mno.

Kama hutaki nyamaza tu

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Chama hana ukubwa huo - simba ni kubwa sana
 
Kosa ni la kocha au waliotoa kibarua cha kocha katikati ya msimu?

Kocha yoyote anapopewa timu, mwanzoni ni lazima anatumia muda kutafuta mfumo sahihi, wakati huo huo akiwa na kazi ya kutafuta matokeo...

Si jambo rahisi haswa inapokuwa ni katikati ya ligi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…