Kocha Mwambusi: Kitendo alichokifanya Ntibazonkiza ni furaha ya kufunga goli

Wewe acha manyanga yasiyo na tija.
 
Huyu faza sometimes nilikua nakubali Sana filosofa zake ....

Ningekua kocha huyu ntibazonkiza sijui ,asingecheza mechi yoyote wala hata kukaa benchi tena mpaka aombe msamaha Kwa kitendo chake ... kwa benchi la ufundi,klabu na mashabiki ....
Sio kwa Makocha Wa Kiafrika Kaka, Haya Alikuwa anayaweza Mourinho na Ferguson Tu Mkuu
 
Hahah kwa hiyo kuna mchezaji katoka uwanjani baada ya kuweka kambani sababu furaha???

Ndio maana nimeacha kutazama ligi yetu acha tu kwenda uwanjani...
 
Kocha mechi 3 kaahinda 2 droo 1 bado mnamzarau acha aanze kazi huyo mzungu tuone
 
alitoa nyeti zake ndogo nje?

Picha iko wapi?
Boresha uzi .
 
Sappong ni mchezaji mzuri kuliko hao akina Nchimbi na Yacouba ana brain ya mpira hata kama hafungi.
Sarpong huyu huyu?

Basi hao kina Yacouba na Nchimbi watakua ni worse players in VPL kama mpaka wanapitwa na Sarpong.
 
Kwa hyo mtu akifunga goli akiwa na furaha anaomba kutolewa ?[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16].
Sijui maana ya UTOPOLO ila naona huu ndo UTOPOLO wenyewe
 
Kocha Mwambusi hivi Mchezaji anayefunga Goli huwa ananuna kama ilivyokuwa leo (jana) kwa Saido Ntibanzonkiza?

Kocha Mwambusi hivi Mchezaji anayefunga Goli (Saido Ntibanzonkiza) huwa anamfuata Kocha wake (Wewe) na Kukufokea, Kukubishia na kuelekea Vyumbani kwa Hasira?

Kocha Mwambusi hivi Mchezaji anayefunga Goli (Saido Ntibanzonkiza) kwa Furaha huwa anaanza Kujibizana hovyo na Wachezaji wenzake akina Kaseke, Nondo na Mukoko mpaka Kuwadharau?

Sikutaka Kusema kilichotokea na kama kawaida yangu Generalist huwa sipitwi na Jambo gumu pale nikitaka Ukweli wake na nashukuru mno kuwa nina Vyanzo vyangu vya uhakika huko Jangwani na Msimbazi (tena kwa wale walioko Jikoni kabisa) na nikija na Jambo hapa JamiiForums huwa silibahatishi.

UKWELI KAMILI NDANI YA YANGA

1. GSM imewagawa Wachezaji
2. Wachezaji wazawa Wanapuuzwa
3. Saido Ntibanzonkiza ana Dharau
4. Mwambusi unabagua Wachezaji
5. Wachezaji Wanarogana sana tu
6. Wachezaji wa Yanga hawapendani
7. Mishahara na Posho ni tatizo

Kesho nikiamka nitakuja na Exclusive ya kwanini Juzi Mchezaji na Kiungo mahiri wa Kinyarwanda Haruna Fadhili Hakizimana Niyonzima Yanga SC ilipocheza na Biashara United FC alipomaliza Kufuturu Tende Uwanjani akiwa amekaa pembeni ya Uwanja na Beki Bakari Nondo Mwamnyeto alipoamka alijibizana hovyo na Kit Manager wa Yanga SC huku akitukanana nae na akinyoosha kidole kwa Kocha Mwambusi.

Na nikimaliza nitakuja tena na Exclusive nyingine inayomhusu Kipa Metacha Boniface Mnata na kwanini hapangwi tena Yanga SC na Feisal Salum Fei Toto kutokupangwa kwa Maagizo kutoka Juu Uongozini na kwa GSM na Kocha Mwambusi kulazimishwa ampange Muangola Carlinho ( Kalinyo ) tu kwa sasa.

Tunajua kwanini leo ( jana ) ilikuwa iwe isiwe ni lazima mshinde kwani.

1. Mlitaka Kumuonyesha Kocha wenu mpya (asiyejua Kiingereza wala Kiswahili) Nasreddine Nabi kuwa mna Kikosi kizuri na asiogope kisha ajue kuwa ametua katika Timu bora wakati kumbe ametua katika MATATIZO MAJUNGU LAWAMA SHIDA YANGA SPORTS CLUB ambayo kwa Historia ya huyu Kocha akidumu Yanga SC miezi Kenda (Tisa) tu ijayo Generalist nitaogelea Kifua Wazi ( Kidali Poo ) kutoka Dar es Salaam hadi Zanzibar.

2. Ilikuwa ni lazima leo Mshinde kwa namna yoyote ile (tena kwa idadi kubwa tu ya Magoli) ili Kuwafurahisha Mashabiki wenu na Kuwatamanisha wajitokeze kwa wingi (Nyomi Kubwa) Siku ya Jumamosi ijayo pale mtakapocheza na Azam FC ( Simba SC B ) ambayo mtafungwa na Kuvurugana zaidi.

Soka la nchini lipo 'Kiganjani' mwangu.
 
Hahah kwa hiyo kuna mchezaji katoka uwanjani baada ya kuweka kambani sababu furaha???

Ndio maana nimeacha kutazama ligi yetu acha tu kwenda uwanjani...
Anafunga halafu ananuna na anatoka uwanjani.. Yaani yule Mrundi anajiona kama Messi
 
Ha ha ha,
Unaifunga Gwambina kisha unataka ufanyiwe Sub, siku ukiifunga Al Ahly si utataka utoke kabisa nje ya Uwanja ukapumzike mwaka mzima usicheze..!!
Hahah jamaa tutaenda kumfuata Chalinze hukooo...maana anaweza akatoka nduki na sio kutembea
 
Hii ya kwamba mtu akifunga kwa furaha anaomba atoke nje akafurahie ...inafikirisha. nawaza siku yanga tukishinda bao 8 labda wachezaji watanl ndo wamefunga hayo magoli halafu ndo tumekubaliana kuwa tukishinda ndo style yetu ya kushangilia.itakuaje?
 
Hahaha Genta kama Genta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…