Kocha Mwinyi Zahera aachia ngazi Yanga. Mkwasa kuinoa kwa muda

Kocha Mwinyi Zahera aachia ngazi Yanga. Mkwasa kuinoa kwa muda

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Yanga imevunja mkataba na kocha wake Mwinyi Zahera pamoja na benchi zima la ufundi sambamba na kuvunja kamati ya mashindano.

Zahera ametimuliwa na klabu hiyo wakati mwenyewe ameendelea na kazi yake kama kawaida.

Zahera leo asubuhi amefika mazoezini kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini na kuendelea na majukumu yake wakati timu yake ikijiandaa na mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Ndanda ya Mtwara.
****

Mwenyekiti wa Yanga, Mshindo Msolla amemtangaza Charles Boniface Mkwassa kuwa kocha wa muda wa Yanga akichukua nafasi ya Mwinyi Zahera kwa muda wa wiki mbili
 
Nimecoment hapo juu kutokana na heading !! Nilivyosoma content nimeona wewe ni shabiki wa mikia Fc maana kama uelekeo upi ambao Yanga Africans tumepoteza kwa msimu huuu !! Ila Zahera OUT
Habari za hivi punde zinasema Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera ameachia ngazi Yanga baada ya timu kupoteza uelekeo.
 
Sio kweli na viongozi wengi wa yanga wameanza kuamini kuwa mfumo wa yanga kiuendeshaji ndio tatizo, na mpaka sasa wanaona ni bora waingie katika mfumi wa hisa kama simba.
Sijui siku wakiingia katika mfumo wa hisa ndugu yangu Shadeeya utajisikiaje maana sio kwa maneno yale kutoka kwa wananchi kwamba yanga ni ya wananchi haiwezi kumilikiwa na kikundi cha watu.
 
Yanga watajutia ilikiwa inatakiwa wakae nae tu wamshape vizuri ukiangalia kilichomponza zaidi Zahera ni lopolopo sana kama yeye ndio msemaji wa vyura na hana staha anamkosoa mchezaji wake sehemu yeyote hata kama ni mbele ya waandishi wa habari lazima timu imshinde
 
Sio kweli na viongozi wengi wa yanga wameanza kuamini kuwa mfumo wa yanga kiuendeshaji ndio tatizo, na mpaka sasa wanaona ni bora waingie katika mfumi wa hisa kama simba.
Sijui siku wakiingia katika mfumo wa hisa ndugu yangu Shadeeya utajisikiaje maana sio kwa maneno yale kutoka kwa wananchi kwamba yanga ni ya wananchi haiwezi kumilikiwa na kikundi cha watu.
Tusubirie mpaka ije kuwa hivyo Mkuu.

Japo nitaumia sababu na mie ni sehemu ya wawekezaji kwenye timu ya Wananchi. Teh teh. 🤪🤪🙈
 
Inabidi waangalie tatizo lipo wapi, lakini bila kujua chanzo watafukuza kila atakuja.
 
Nimecoment hapo juu kutokana na heading !! Nilivyosoma content nimeona wewe ni shabiki wa mikia Fc maana kama uelekeo upi ambao Yanga Africans tumepoteza kwa msimu huuu !! Ila Zahera OUT
Bundi katua mto jangwani..zahera bado yupo kajaa tele...
 
Back
Top Bottom