Kocha wa dunia Mwinjuma kipaji ameua nani

Kocha wa dunia Mwinjuma kipaji ameua nani

scatter

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2013
Posts
1,667
Reaction score
926
Huyu jamaa nakumbuka aliteka sana kipindi cha nyuma katika soko la mziki wa dansi Yaani kusema kweli aliweza sana kuanzia mchinga sound mpaka kwenye bendi za Manyangau twanga sijui huyu jamaa yu wapi!
 
Kina nani maana kazi ya mziki inajieleza yenyewe kwa mashabiki
 
ngoja watakuja wajuzi wa mambo haya wataweka wazi.
 
Ninavyojua mimi wanamuziki wengi ha Tanzania hawawezi kusimama wenyewe.Yaani wamezoea kufanywa vibarua na vipaji vyao.
 
Kwahiyo huyu jamaa mganga ndio kamtoa
 
IMEANDIKWA: Ole wake amtegemea mwanadamu...ATALAANIWA..

nilimpenda saana huyu jamaaa na pia bado na mpenda..kama umri una mruhusu atubu kwa muumba arudi kazin .atatoka tuu
 
Ninavyojua mimi wanamuziki wengi ha Tanzania hawawezi kusimama wenyewe.Yaani wamezoea kufanywa vibarua na vipaji vyao.

Umegusa suala la msingi sana ndugu.
Vipaji vya wanamuziki vinatumiwa na wenye fedha. Unawakumbuka Mafahari watatu? (Choki, Banza, Muumini?). Hili suala la kutumika na wenye fedha ndilo linalomsumbua Hussein Jumbe pia. Enzi za akina Mpakanjia akina Jumbe na Muumini walikuwa na mbwembwe sana. Walihama kutoka bendi moja kwenda nyingine ili kuuza sauti zao. Muumini alisimama imara alipokuwa na support ya Mudhihir (Mchinga) na Asha Baraka (African Revolution). Alipoondoka huko akaaanzisha bendi yake (Double M Sound), then ikafa. Akaungana na Ally Choki kuuunda bendi nyingine (Double Extra) ambayo nayo haikudumu. Bendi hiyo ilikuwa na support ya Mohamed Mpakanjia (RIP). Baada ya hapo Muumini hakusimama tena, ila Choki bado wamo na bendi yake ya Extra Bongo. Muumini anaweza kusimama iwapo:-
  1. Ataacha kuimba nyimbo za majungu na malalamiko (walitukanana sana na Waziri Sonyo na Banza)
  2. Ataacha kutegemea msaada wa wenye nazo ili wamuinue. Atafute mtaji, anunue vifaa na kuendeleza kipaji chake ili asihamehame.
 
Idimi,

ni kweli usemayo ajiwekeze bila kuingia katika majungu na wenye pesa
 
Naomba kupata historia fupi ya huyu msanii hasa mwaka alioanza kuimba na nyimbo alizotoa kulingana na miaka. Kwa mwenye uelewa tafadhali
 
Huyu jamaa nakumbuka aliteka sana kipindi cha nyuma katika soko la mziki wa dansi Yaani kusema kweli aliweza sana kuanzia mchinga sound mpaka kwenye bendi za Manyangau twanga sijui huyu jamaa yu wapi!
Mkuu hakuna aliyeua kipaji ,bali kila kitabu na zama zake,hivi wapi umesikia kwa hivi sasa muziki wa bendi au bolingobolingo unashadidiwa hapa nchini Tanzania,hebu nitajie kama kuna bendi ambayo ipo na inajazaa nyomi kwa kupiga muziki wa bendi,hao Ngwasuma tu wapo chali,Twanga wapo chali,Msondo ndio usiseme,Sikinde wapo jina sasa huyo Mwinjuma atawikia wapi,uliza akina Ally Choki wapo wapi? Muziki wa wazee nani atausikiliza siku hizi wakati robo tatu ya Watanzania ni vijana,wanaohangaika na nyimbo za Tetema ,au Nyegezi halafu wewe usema Mwinjuma ,nani anamjua Mwinjuma katika kizazi cha sasa?Kwa kifupi hata Mchinga ifufuliwe au sijui Msondo ifufuke hakuna itakayokuwa maarufu,dunia imegeuka,hata hii Bongo fleva kuna siku itakuwa zilipendwa na Domo atasahaulika
 
Idimi,
Siafiki hizo sababu,sababu kubwa bni kuwa huo muziki wa akina Mwinjuma upo ICU na kizazi cha sasa ambacho ndio walio wengi wana aina yao ya muziki,kila kitabu na zama zake,hata isiwe majungu sijui kurogana lakini aina hiyo muziki wa akina Mwinjuma imeshakufa si hata kwenye vyombo vya habari hatusikii nani atasikiliza huo muziki wa wazee ,vijana ndio wengi na ndio wakati wa akina Domo kutamba kwa kuchezesha midomo jukwaani na kuimba tu Nyegezi au tetema wanaingiza mamilioni sasa wewe uimbe Mgumba wakati huu nani atakusikiliza na halafu muimbaji ni mzee kama Mwinjuma?
 
Back
Top Bottom